
–

Wawakilishi wa Tanzania katika Michuano ya Kombe La Shirikisho Afrika, Klabu ya KMC FC Imethibitisha kushiriki kwao katika Mashindano ya CECAFA Kagame Cup 2019 yatakayofanyika kuanzia mwezi Ujao huko Kigali, Rwanda.
.
– KMC wamesema kuwa watatumia Mashindano hayo ya kikanda kufanya Maandalizi yao kabla ya kuanza kwa game zao za Kimataifa… KMC ambayo kwasasa haina Kocha Mkuu inatarajia kumtangaza kocha mpya siku yoyote kuanzia Wiki Ijayo ambapo Wamepokea CV za makocha kutoka Sehemu Mbalimbali Afrika na Ulaya Kama Afrika Kusini, Botswana, Ureno, Ubelgiji na Ufaransa..
.
– KMC Baada ya Kuthibitisha kuwepo Kagame Cup, inakuwa timu ya Pili kutoka Tanzania pamoja na Azam FC… Ikumbukwe Yanga SC na Simba SC zilitangaza kutishiriki Michuano hii.
#cecafa #CECAFAKagameCup
@Sokawaytz