

MEXICO KUPIGA MNADA NDEGE YA RAIS ILI KUDHIBITI UHAMIAJI HARAMU
–
Rais wa Mexico, Andres Manuel Lopez ametangaza kupiga mnada ndege ya Rais na fedha zitakazopatikana zitatumika kusaidia jitihada za kudhibiti uhamiaji haramu
–
Hatua hiyo imekuja baada ya Mexico na Marekani kufikia makubaliano ili kuepuka vikwazo vya kiuchumi na ongezeko la kodi katika biashara ya nchi hizo mbili ambapo Mexico iliahidi kuongeza vikosi mipakani kudhibiti wahamiaji haramu kwenda Marekani
–
Ndege hiyo aina ya Boeing 787 Dreamliner ilinunuliwa mwaka 2016 kwa dola milioni 218 lakini sasa inaweza kuuzwa kwa kiasi kisichopungua dola milioni 150 na imeanza kupigwa mnada miezi michache iliyopita ikiwa California, Marekani
–
Sehemu ya fedha zitakazopatikana zitatumika kupeleka vikosi vya wanajeshi 60,000 mpakani kwa ajili ya kusaidia kudhibiti uhamiaji haramu













