TUMPE MUDA NDAYILAGIJE ATIMIZE MAJUKUM YAKE

Jina la Ndayilagije ni miongoni mwa majina maarufu miongoni mwa watu wa mpira Tanzania!!
Umaaruf wake haujaja hivi hivi bali kuna kazi kubwa ilifanyika mpaka kufikia hapa alipo

Njia alizopitia Ndayilagije ni njia alizopitia Idd seleman au Kwassi kufikia kuwa watu maarufu!! Ndayilagije alianza kujijengea jina msim wa 2016/17 kwa kuifikisha Mbao fc fainali ya shirikisho na kupoteza mbele ya Simba pale Jamhuri stadium Dodoma na kufungwa goli 2-1

Ndayilagije ndiye aliyetuletea kina Jamal Mwambeleko, Pius Buswita, Habib Kayombo, Benjamini Haule, Mveyekule, David Mwassa, Asante Kwasi, Ndikumana, Maganga, hakuna asiyejua balaa la hawa wachezaji na ile mbao isiyoshikika hakuna asiyejua kama huyu ndiye kocha aliyefanya CCM KIRUMBA kuwa sehem hatari kwa hizi tim zetu kubwa hapa Tanzania

Ndayilagije alikuwa na jicho la kuona mchezaji na kutambua ubora na uwezo wake na alikuwa na uwezo wa kumfanya mchezaji mdogo kuwa star hicho ni kipaji na si kila mtu anacho na aliweza kuunganisha wachezaji wa kawaida na kutengeneza tim ya ushindi

Baada ya hapo akatimkia zake KMC na pia huko aliendeleza kila alichoishia nacho Mbao akatengeneza KMC kuwa tim tishio na kuogopewa na kuifanikisha kushika nafasi ya nne kwenye ligi yetu na akaunganisha wachezaji moderate na kuwafanya kuwa tishio na style yake ilikuwa ile ile aliyotoka nayo Mbao

Leo Ndailagije ni Kocha mkubwa Tanzania ukiwaondoa AUSSEMS NA ZAHERA na anachokifanya sasa ni muendelezo wa alichokianza kwanye soka letu

Leo kumekuwa na kelele nyingi kumhusu Ndayilagije baada ya kufungwa na Sudan hapo jana mijadala ni mingi na mpaka inafikia kipindi watu wanadoubt uwezo wa Ndayilagije daaa huu ni upotevu wa fikra, nguvu na akili naweza sema hivyo

Ndayilagije ni mwajiriwa wa Azam yupo Stars kama deiwaka na anakabidhiwa Stars ikiwa kwenye mashindano na mbaya zaidi huku akiwa na majukum makubwa ya klab yake na mkumbuke Azam inashiriki shirikisho Afrika hana muda wa kupumzika kila siku yupo kazini akitoka Azam yupo Stars

Leo watanzania waliokuwa wanamtukana Amunike ndio hao hao wanaomtukana Ndayilagije na kusema bora Amunike daaa shukrani ya punda mateke

Inaendelea
✍🏻 @karimkondo

Eto’o kwangu mchezaji bora na salah.na sadio.mane

✍🏻 Legendary wa Cameroon 🇨🇲, Inter Milan na FC BARCELONA, Samuel Eto’o Jana Kabla ya utoaji wa Tuzo za FIFA Upande wa Mchezaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Aliulizwa kwake Ni yupi Bora Kati ya walio ingia Tatu Bora, Kwa maana ya, Mshindi wa Tuzo hiyo, Lionel Messi pamoja na Virjil Van Dijk aliyekamata nafasi ya Pili na tatu alishika Cristiano Ronaldo..

🗣 ETO’O Alijibu “Mchezaji Bora kwa Upande wangu Ni Mmoja Kati ya, Mohamed Salah au Sadio Mané, Lakini wote hawapo hapa”.. 🙌🏻.

✍️ Wachezaji hao Bora wa Eto’o walimaliza nyuma ya hao Wachezaji walioingia tatu Bora, yaani Sadio Mané Nafasi ya Nne huku Nyota wa Misri, Mohamed Salah akishika Nafasi ya tatu..
#TheBestAwards #TheBest #FIFAAwards
@Harunlugoyah

Kikosi bora cha dunia chawekwa hadharani

✍️ Sergio Ramos Ndio Beki wa kwanza na Mchezaji wa kwanza kabisa Kutoka Nchini Hispania katika historia kutajwa Katika Kikosi Bora Cha Mwaka Cha FIFA “FIFPro #WorldXI” Kwa misimu 10 tofauti… Na hiki ndio Kikosi Bora kilichotangazwa…
#FIFPRO XI 2019:
🇧🇷 Alisson
🇪🇸 Ramos
🇳🇱 De Ligt
🇳🇱 Van Dijk
🇧🇷 Marcelo
🇭🇷 Modrić
🇧🇪 Hazard
🇳🇱 De Jong
🇦🇷 Messi
🇵🇹 Ronaldo
🇫🇷 Mbappé

Tuzo za FIFA THE BEST 2019 kutolewa leo

Tuzo za FIFA THE BEST 2019 zitatolewa leo pale Milan, Italia kuanzia majira ya saa 3.30 usiku.

Baada ya Van Dijik kunyakua tuzo ya mchezaji bora UEFA, beki huyu ameingia tena kwenye 3 bora ya wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa FIFA2019 (wanaume), akishindana na wakali wa tuzo hizi, Lionel Messi na Ronaldo

Inaweza kuwa shavu kwa beki Van Dijik au lolote linaweza kutokea Messi ama Ronaldo akachukua? Itajulikana baadaye pale Milan.

Afisa habari na.muhamasishaji yanga sc watambulishwa rasmi

Kaimu Katibu Mkuu wa klabu ya @yangasc Dismas Ten hii leo amewatambulisha rasmi Ndugu HASSAN BUMBULI kuwa ni Afisa habari na Ndugu ANTONIO NUGAZ kuwa ni Afisa muhasishaji wa Klabu ya Yanga na kuwashukuru viongozi hao kuamua kwa moyo kuitumikia klabu hiyo.
:
Hongera @antonionugaz @hassan_bumbuli

Design a site like this with WordPress.com
Get started