BAADA YA KUIFUMUA ETHIOPIA, NGORONGORO KUIVAA KENYA KESHO

Baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Ethiopia jana kwenye mechi ya ufunguzi ya Michuano ya CECAFA U20 Challenge Cup inayoendelea nchini Uganda, timu ya Taifa ya Tanzania, ‘Ngorongoro Heroes’ kesho itashuka dimbani kuikabili Kenya.

Mchezo huo ambao utaanza saa 7 mchana unatarajiwa kuwa mkali baada ya Kenya kuifunga Zanzibar mabao 5-0 katika mechi yake ya ufunguzi iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Kituo cha Ufundi cha Fufa.

Kocha Mkuu wa Ngorongoro Heroes, Zubeiry Katwila amesema kwa namna alivyoitazama Kenya vijana wake wanatakiwa kucheza kwa kujituma zaidi ili kuweza kupata ushindi wa pili na kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo. “Tumewaona Kenya, ni timu nzuri. Uzuri ni kwamba hata wachezaji pia walikuwepo uwanjani na kuona wapinzani wetu wamefanya kitu gani. Utakuwa ni mchezo mzuri na wa ushindani, tunaimani timu yetu itafanya vizuri,” alisema Katwila.

Kwa upande wake beki wa kati wa timu hiyo, Oscar Masai, amesema tayari mwalimu wao amewapa mbinu sahihi za kuikabili Kenya hapo kesho, huku akisisitiza kuwa hali ya wachezaji ni nzuri na wamejipanga kushindana. “Kama wachezaji tuko vizuri, tunashukuru kwamba tulianza mechi ya kwanza kwa matokeo bora, tunatamani kuendeleza hicho. Kuhusu Kenya, Mwalimu aliwaona vizuri na ametuambia nini cha kufanya hapo kesho,” alisema Masai ambaye ni mchezaji wa Azam FC.

Naye straika wa timu hiyo, Andrew Simchimba aliyefunga mabao matatu ‘Hat Trick’ kwenye mechi dhidi ya Ethiopia, amesema anatamani kuendelea na kiwango chake bora alichoanza nacho katika mashindano hayo ili kuweza kuisaidia timu.

@tanfootball @serengetiboystz

Credit : @giftmacha_official
#wapedasokaupdates

Rekodi.ya Lampard ndani ya chelsea

13 – Chelsea Mpaka Sasa wamecheza mechi Sita za Premier wakifunga Magoli 12, Wakifungwa Magoli 13.

✍️ Baada ya game Sita za mwanzoni mwa Msimu kwa The Blues kufungwa Magoli 13 Ni idadi kubwa Zaidi kwa Upande wao na kwa Mara ya kwanza… Mara ya Mwisho kwa wao kuruhusu kufungwa Magoli mengi Katika Ligi Ni Msimu wa 1978-79 (pia Magoli 13) – Taarifa tu Kwa Msimu huo Chelsea iliburuza mkia Msimu ulipofikia tamati Katika Daraja la kwanza Kipindi hicho, Katika Mechi 42 za Ligi, Ushindi 5, Sare 10, Vipigo 27, Magoli ya Kufunga 44 na magoli ya Kufungwa 92 (20pts)… Liverpool ilimaliza Bingwa Msimu Huo ukiwa Ni Ubingwa wa 11 Kati ya Mara zote 18 😃😃

✍️ Mpaka Sasa Katika Premier league wapo nafasi ya 11 na pointi zao 8… Pointi 10 nyuma ya Vinara wa Ligi, Liverpool na pointi Sita Mbele ya Watford wanaoburuza Mkia 🙄🙄!.
#PremierLeague #Chelsea
@Harunlugoyah

Kevin De Bruyne afanya balaa zito EPL

✍️ Kiungo wa Klabu ya @ManCity, Kevin De Bruyne Baada ya Mechi Sita za mwanzoni mwa Msimu huu, ndio Mchezaji ambaye katengeneza Nafasi nyingi Zaidi za Magoli langoni mwa timu pinzani… Akifanya hivyo Mara 27 Ikiwa Ni idadi kubwa Zaidi ya Wachezaji wote ndani Premier league Msimu Huu..

✍️ Wakati KDB Akiwa kinara, Wachezaji wengine walio tengeneza Nafasi nyingi Zaidi kuelekea lango la timu pinzani Msimu Huu Ni..
⚽ Trent Alexander-Arnold – 23 “Liverpool”.
⚽ Pascal Gross – 15 “Brighton”.
⚽ 15 – Riyad Mahrez “Man City”, Manuel Lanzini ” West Ham” & Gylfi Sigurdsson “Everton”.
#PremierLeague #PLUpdates
@Harunlugoyah

CECAFA U20FT | Eritrea 3-3 Sudan‬

‪CECAFA U20 Challenge Cup Result‬ ‪FT | Eritrea 3-3 Sudan‬
‪⚽️Mewael Tefsai Yosief 10’‬
‪⚽️Mohammed Abbas Namir 40’‬
‪⚽️Shihab Eldeen Siddiq Abdalrahman 45’‬
‪⚽️Robel Teklem Michael (pen) 55’‬
‪⚽️Ali Suleiman Ibrahim 72’‬
‪⚽️Musab Kurdman Elfaki (pen) 90’‬
Via ‪#kawowoupdates #cecafau20

BENCHI LA UFUNDI STARS LAWAOMBA RADHI WATANZANIA

Baada ya kukubali kipigo cha bao moja nyumbani dhidi ya Sudan jana benchi la ufundi la timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ limewaomba radhi Watanzania kwa kilichotokea.

Stars ambayo katika mchezo wa jana ilitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini ilishindwa kuzitumia itapaswa kushinda kuanzia mabao mawili ili kufuzu fainali hizo ambazo zitafanyika nchini Ivory Coast.

Kocha msaidizi wa timu hiyo, Juma Mgunda amewataka Watanzania kutokukatia tamaa kipigo hicho na waendelee kuiamini kwakua wanaweza kupindua matokeo ugenini.

Mgunda amekiri kuwa walitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini hawakuweza kuzitumia na wamelichukua jambo hilo kama changamoto na wanaamini wataweza kulifanyia kazi mchezo ujao. “Kwanza nichukue nafasi hii kuwaomba radhi Watanzania kwa kilichotokea, hakuna aliyetarajia. Tunajua mna uchungu hata sisi na wachezaji tupo kwenye hali hiyo lakini ninacho waomba muwe na uvumilivu na msikate tamaa na timu yenu. Tunaweza kufanya vizuri katika mchezo wa marudiano ugenini,” alisema Mgunda.

@tanfootball @taifastars_

#wapendasokaupdates

Design a site like this with WordPress.com
Get started