
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya UD Songo leo hautakuwa mwepesi lakini muhimu kwao ni kupata matokeo mazuri ugenini
Mida ya saa 11 jioni kwa saa za hapa Tanzania, Simba itashuka dimbani huko Beira Msumbiji kucheza na UD Songo ukiwa ni mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa hatua ya awali

Mbelgiji huyo amesema wanawaheshimu wapinzani wao ambao watakuwa nyumbani katika mchezo huo
“Tuna heshima kubwa kwa wapinzani wetu, na tunajua utakuwa mchezo mgumu. Tuna michezo miwili, kesho (leo) na mwingine Dar na lengo ni kufuzu hatua inayofata,” amesema
Matokeo ya ushindi au sare kwa Simba yatakuwa ni matokeo mazuri kuelekea mchezo wa marudiano ambao utapigwa ‘machinjioni’ uwanja wa Taifa

– England – Premier League.





















