LIGI KUU BARA KURUDI KUWA NA TIMU 16 MSIMU WA 2021/22‬ –

Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amesema hayo ikiwa bado siku 1 kuanza kwa msimu wa 2019/20‬

‪Amesema msimu huu (2019/20) kutakuwa na timu 20 na msimu wa 2020/21 kutakuwa na timu 18‬

Wambura amesema kwa msimu huu zitashuka timu nne moja kwa moja daraja la kwanza, zitakazo kuwa nafasi ya 17, 18, 19 na 20 huku timu zilizoshika nafasi ya 15 na 16 zikicheza mchujo na mbili za daraja la kwanza

Aidha, utaratibu wa kupanda Ligi Kuu kwa timu za daraja la kwanza utakuwa vile vile kwa vinara wa makundi yao mawili kupanda moja kwa moja huku watakaomaliza nafasi ya pili kwenye kila kundi wakicheza mchujo

@habarizamichezo

Mbao yamteua said khamis jr kuwa nahidha

Uongozi wa timu ya Mbao FC umemteua Said Khamis Jr kuwa nahodha mpya, akichukua nafasi ya David Mwassa aliyejiunga na Lipuli

Katibu wa Mbao, Daniel Naila amesema Khamis Jr atasaidiana na Babilas Chitembe na wamefikia uamuzi huo, baada ya kuridhishwa na uwezo wa wawili hao

Mbali ya Mwassa, wachezaji wengine walioikimbia Mbao FC ni Hashim Mussa (Mwadui), Metacha Mnata (Yanga), Kelvin Igendelezi (Pamba ), Vincent Philipo (Lipuli), David Mwangosi, Erick Murilo, Abdulkarim Hamim (Alliance) na Amos Charles (KMC)

@habarizamichezo

BODI YA LIGI KUU BARA YAFANYA MABADILIKO KATIKA UENDESHAJI –

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara imesema imebadilisha baadhi ya mfumo wa uendeshaji wa masuala mbalimbali ikiwemo suala la mavazi ya makocha, ambapo kocha atatimuliwa uwanjani endapo atavaa vibaya

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amesema kuwa mabadiliko hayo yanaendana na mpango wa kuboresha ligi

Masuala yaliyoangaliwa zaidi ni kuhusu suala zima la wachezaji wa kigeni ambapo hawatapewa leseni za kucheza hadi wapatiwe vibali vya makazi na kazi, pia wachezaji wote wa kigeni watakaosajiliwa msimu ujao lazima wawe wanacheza timu za Taifa au ligi kuu nchini mwao

Klabu zote za ligi kuu zinatakiwa zisajili wachezaji watatu kutoka U-20 na wapatiwe nafasi ya kucheza

Pia katika mabadiliko hayo, timu mwenyeji ndiye atakayetakiwa kuandaa gari la wagonjwa katika mchezo husika pamoja na waokota mipira na iwapo timu mwenyeji haitafanya hivyo itapokonywa pointi na makatibu wake kupewa adhabu

Manara atoa neno.kuelekea mechi za klabu bingwa na shirilisho tanzania

Tunahitaji tulinde heshima ya nchi yetu, Tunajua kama mwaka wa jana na miaka mingine ya nyuma huko tulipigana vita, Mwaka wa jana ilienda mbali zaidi kiasi cha kushirikiana na timu za nje, Sisi tumesema tuyaache ya nyuma tugange yajayo tuungane mkono “.-

Haya na maneno ya @hajismanara akitoa hamasa kwa timu za Tanzania na mashabiki kuungana nakuwa kitu kimoja pindi timu zetu za Tanzania zinaposhiriki michuano ya Kimataifa barani Africa …kwa Lengo la kuzisaidia timu hizi zifanye vizuri katika mashindano hayo.makubwa

@habarizamichezo

Jeshi la.simba la.kamilika sasa UD songo hachomoki

Jeshi kamili la kikosi cha Simba linamekamilika kuelekea mechi yao ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya UD Songo itakayopigwa keshokuwa Jumapili Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada ya wachezaji watatu waliokuwa majeruhi kurejea kujifua na wenzao.

Simba iliwapoteza wachezaji wake watatu; kipa Aishi Manula, mshambuliaji Ibrahim Ajibu, na mshambuliaji Mbrazil Wilker Henrique da Silva waliokuwa majeruhi, lakini sasa wamerejea kikosini kujifua na wenzao.

Wakati wachezaji hao wakirejea, Meneja wa timu hiyo, Patrick Rweyemamu amesema kwamba chumba cha majeruhi amebaki nahodha John Bocco, ambaye aliumia wakati wakishinda 4-2 na kutwaa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC wiki iliyopita.

“Ajibu, Manula na Wilker da Silva wamereja na wanajifua na wenzao, kilichobaki sasa ni uamuzi wa Kocha Mkuu Patrick Aussems, kuamua atampanga nani kuelekea mechi yetu ya marudiano Jumapili,” alisema Rweyemamu.

Hata hivyo, licha ya nyota hao kurejea kutokana na ubora wa kila mchezaji anayepata nafasi kuonyesha uwezo mkubwa, Aussems atalazimika kuchanga karata yake vizuri ya nani aanze katika kikosi hicho.

Kipa Beno Kakolanya, ameonyesha ubora wa hali ya juu tangu alipoanza kuidakia timu hiyo dhidi ya Power Dyanamos kwenye mechi ya Simba Day na kuiongoza kushinda 3-1, kisha wakatoka sare tasa dhidi ya UD Songo ugenini kabla ya kuiongoza kushinda 4-2 dhidi ya Azam FC kwenye Ngao ya Jamii.

Ni wazi, Manula anaweza kusubiri kwa muda kabla ya kumshawishi Aussems hasa ukizingatia anahitaji kujiweka fiti zaidi kutokana na kutokea chumba cha majeruhi, lakini pia Ajibu na Da Silva wana kazi ya kufanya katika nafasi zao.

Ajibu na Da Silva wanapaswa kuonyesha ubora wa hali ya juu wakati huu Bocco akiwa majeruhi, kwani tayari hakuna kati yao anayeweza kumweka benchi kwa sasa, Sharaf Eldin Shiboub ama Clatous Chama au hata Hassan Dilunga ‘HD’.

Upana wa kikosi cha Simba umeanza kuonekana mapema hususan idara ya kiungo mshambuliaji kutokana na uwezo mkubwa unaoonyeshwa na wachezaji wa nafasi hizo.

Simba keshokutwa itahitaji ushindi wa aina yoyote ili kuweza kusonga mbele katika mchuano hiyo ambayo msimu uliopita iliishia robo fainali kufuatia kutolewa na TP Mazembe ya DR Congo kwa jumla ya mabao 4-1.

Kama Simba itasonga mbele ama UD Songo, itakuna na mshindi kati ya FC Platinum ya Zimbabwe na Nyasa Bullets ya Malawi ambayo kesho itakuwa ugenini ikisaka matokeo baada ya mechi ya awali kulazimishwa sare tasa nyumbani

Nipashe

KMC kuivaa As kigali leo uwanja wa taifa

Wawakilishi wa Tanzania katika michuani ya shirikisho balani Africa.KMC Leo siku ya ijumaa inashuka dimbani uwanja wa taifa kucheza mchezo wa marudiana na As kigali kutokea nchini rwanda ..

Mchezo huo unatarajiwa kuanza majira ya saa 9:00 jioni..katika uwanja wa taifa jijini dar es salaam…ikumbukwe tu…mchezo wa kwanza uliopigwa nchini rwanda kati ya KMC na As kigali ulimalizika kwa timu hizo kutoka suluhu ya bila.kufungana….

Baada ya mchezo wa Leo. Timu.itakayoondoka na ushindi itafuzu kucheza hatua ya pili.ya mtoano katika michuano ya shirikisho barani afrika

Kila raheli KMC mnapo peperusha bendela ya tanzania hii Leo

@habarizamichezo

RATIBA YA SOKA LEO IJUMAA + MATOKEO YA SOKA JANA.

#CafConfederationCup
16:00 KMC vs As Kigali
AGG 0-0
19:00 Santoba vs Tornadoes
AGG 2-1
20:30 Ahly Shendi vs Bandari Fc
AGG 0-0
20:30 Alkhartoum vs ART
AGG 1-1
17:00Ascot vs Belouizdad
AGG 0-2
16:00Esae vs SNIM
AGG 5-0
19:00Etoile Congo vs Pyramids
AGG 1-4
19:00Maniema vs Pelican
AGG 1-1
#EnglandPremierLeague
22:00 Aston Villa vs Everton

#SpainLaLigaSantander
21:00 Granada vs Sevilla
23:00 Levante vs Villarreal

#GermanyBundesliga
21:30 1. FC Köln vs Borussia Dortmund

#NetherlandsEersteDivisie
21:00 De Graafschap vs FC Volendam
21:00 FC Den Bosch vs FC Eindhoven
21:00 FC Dordrecht vs Jong Ajax
21:00 Go Ahead Eagles vs Jong FC Utrecht
21:00 Helmond Sport vs Almere City FC
21:00 NAC Breda vs Cambuur
21:00 Roda JC Kerkrade vs NEC Nijmegen
21:00 Telstar vs Excelsior
21:00 TOP Oss vs Jong AZ Alkmaar

#BelgiumFirstDivisionA
21:30 Genk vs Anderlecht

#CafChampionsLeague
16:00 KCCA vs African Star
21:00 Alhly vs Atlabara
22:00 Cote D’Or vs Fomboni
KAMTA MATOKEO YA SOKA JANA.
@sokaplace_

#EuropaLeagueQualification
FT FC Astana 3 – 0 BATE Borisov
FT Ararat Armenia 2 – 1 F91 Dudelange
FT Malmoe FF 3 – 0 Bnei Yehuda Tel Aviv
FT Suduva 0 – 0 Ferencvaros
FT Feyenoord 3 – 0 Hapoel Beer Sheva
FT Ludogorets Razgrad 0 – 0 Maribor
FT FC Koebenhavn 3 – 1 Riga FC
FT AEK Athens 1 – 3 Trabzonspor
FT Legia Warszawa 0 – 0 Rangers
FT AZ Alkmaar 1 – 1 Royal Antwerp
FT FC FCSB 0 – 0 Vitoria de Guimaraes
FT Gent 2 – 1 Rijeka
FT PSV Eindhoven 3 – 0 Apollon Limassol
FT Strasbourg 1 – 0 Eintracht Frankfurt
FT SC Braga 1 – 0 Spartak Moscow
FT Celtic 2 – 0 AIK
FT Linfield 3 – 2 Qarabag FK
FT RCD Espanyol 3 – 1 Zorya Luhansk
FT Partizan Beograd 2 – 1 Molde
FT Slovan Bratislava 1 – 0 PAOK Thessaloniki FC
FT Torino 2 – 3 Wolverhampton Wande.

#SokaPlaceUpdates

Design a site like this with WordPress.com
Get started