
Baada ya Simba kuondolewa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, straika wao Meddie Kagere amesema akili zao sasa wamezihamishia kwenye ligi kuu kuhakikisha wanatetea ubingwa wao
Simba imeanza ligi vizuri kwa kuifunga JKT Tanzania mabao 3-1 huku Kagere akifunga mabao mawili
Kagere aliyeibuka mfungaji bora msimu uliopita kwa kufunga mabao 23 amesema wachezaji wote wanatakiwa kuweka akili na mawazo yao kwenye ligi ili kuhakikisha wanabaki na ubingwa wao.
“Ukiangalia kwenye ligi kila timu ipo imara hivyo lazima tuwe na malengo na kupambana ili kuhakikisha malengo yetu yanatimia
“Tumeanza vizuri ligi kwa ushindi hivyo tutajitahidi kuhakikisha tunafanya vizuri kwenye michezo mingine itakayofuata ili tutetee ubingwa”alisema Kagere
Kagere alisema ni mapema mno kuanza kufikiri kutetea kiatu cha dhahabu alichokipata msimu uliopita kwani ligi ni ndefu na ina mambo mengi na hakuna kitu kizuri kama kuwaza kuisaidia kwanza timu yake itetee ubingwa ndipo mambo mengine yafuate
Kagere alifunga mabao 23 msimu uliopita akiwazidi Salim Aiyee ambaye msimu uliopita aliichezea Mwadui Fc akifunga mabao 18 wakati mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Heritier Makambo akitikisa nyavu mara 17
Waliofuatia walikuwa ni John Bocco wa Simba aliyefunga mabao 16 na Emmanuel Okwi aliyefunga 15
Makambo hivi sasa ametimkia timu ya Horoya AC ya Guinea wakati Okwi amejiunga na klabu ya Ittihad ya Misri huku Aiyee amejiunga na KMC
Mwanaspoti
Baada ya Simba kuondolewa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, straika wao Meddie Kagere amesema akili zao sasa wamezihamishia kwenye ligi kuu kuhakikisha wanatetea ubingwa wao
Simba imeanza ligi vizuri kwa kuifunga JKT Tanzania mabao 3-1 huku Kagere akifunga mabao mawili
Kagere aliyeibuka mfungaji bora msimu uliopita kwa kufunga mabao 23 amesema wachezaji wote wanatakiwa kuweka akili na mawazo yao kwenye ligi ili kuhakikisha wanabaki na ubingwa wao.
“Ukiangalia kwenye ligi kila timu ipo imara hivyo lazima tuwe na malengo na kupambana ili kuhakikisha malengo yetu yanatimia
“Tumeanza vizuri ligi kwa ushindi hivyo tutajitahidi kuhakikisha tunafanya vizuri kwenye michezo mingine itakayofuata ili tutetee ubingwa”alisema Kagere
Kagere alisema ni mapema mno kuanza kufikiri kutetea kiatu cha dhahabu alichokipata msimu uliopita kwani ligi ni ndefu na ina mambo mengi na hakuna kitu kizuri kama kuwaza kuisaidia kwanza timu yake itetee ubingwa ndipo mambo mengine yafuate
Kagere alifunga mabao 23 msimu uliopita akiwazidi Salim Aiyee ambaye msimu uliopita aliichezea Mwadui Fc akifunga mabao 18 wakati mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Heritier Makambo akitikisa nyavu mara 17
Waliofuatia walikuwa ni John Bocco wa Simba aliyefunga mabao 16 na Emmanuel Okwi aliyefunga 15
Makambo hivi sasa ametimkia timu ya Horoya AC ya Guinea wakati Okwi amejiunga na klabu ya Ittihad ya Misri huku Aiyee amejiunga na KMC
Mwanaspoti