
– Mshambuliaji wa Inter Milan, Romelu Lukaku alitolewa matamshi ya ubaguzi wa rangi na mashabiki wa Klabu ya Cagliari kabla ya kufunga bao la ushindi katika mchezo wa Serie A Jana na kutoka na ushindi wa Magoli 2-1.
.
– Lukaku alivumilia milio ya tumbili alipokuwa anajiandaa kuchukua jukumu la kupiga mkwaju huo uliosababishwa na Stefano Sensi katika kipindi cha pili Cha Mchezo… Lukaku alifunga Goli na kufanya kufunga Katika mechi yake ya Pili mfululizo akiwa Kama Mchezaji wa Inter Tangu ajiunge nao!.
:
– Hili ni tukio lingine linalowahusisha mashabiki wa Cagliari, ambao wameshutumiwa na kuwabagua wachezaji weusi wengi katika miaka ya hivi karibuni, Ikumbukwe Hawa Hawa Msimu uliopita walifanya kwa bwana mdogo, Moise Kean, Pia Walifanya kwa Blaise Matuidi..
:
– Lakini Ulaya haya matukio Sasa Hivi yamechukua Nafasi kubwa, pia tuliona yalimkuta Paul Pogba na Marcus Rashford wote wa Manchester United Baada ya kukosa Penati wakiitumikia timu yao Mechi tofauti tofauti msimu huu, wikendi hii tumetoka kuona yamemkuta Beki wa Klabu ya Chelsea, Kurt Zouma Baada ya kujifunga Goli Dakika za lala Salama na kufanya timu Yake itoke Sare ya 2-2 vs Sheffield United Katika Premier League, yalimkuta pia Tammy Abraham Baada ya kukosa Penati Katika mechi ya Fainali ya UEFA Super Cup, The Blues ikipoteza vs Liverpool!.. Enough #NoToRacism 👊🏿👊🏾👊🏽👊🏼👊🏻.
#updates
@Sokawaytz_