
Mambo kadhaa niliyogundua kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara kati ya Kagera Sugar dhidi ya Simba. .
.
Kagere, wakiwa washambuliaji wao walikuwa wakicheza 4-4-2 na washambuliaji wawili mbele pale mpira wanapopoteza au kushambuliwa wao walikuwa wakitumia mfumo wa 4-5-1 kwa kujilinda zaidi.
.
.
Awesu, kijana mdogo mwenye vitu kibao mguu naweza kusema kwenye mchezo wa leo kwa upande wa Kagera Sugar, ameonyesha uhai mtulivu anapiga pasi fupi ndefu lakini kulikuwa na utofauti na viungo wa Simba, walikuwa wakicheza kitimu. .
.
Kagera walijiamini sana katika uwanja wa nyumbani kwa sababu historia ilikuwa inawabeba wakasahau ubora wa Simba ,kwenye uwezo wa mchezaji moja moja.
.
.
Ile pitch ya Kaitaba, nimeielewa sana mpira unatulia chini mpira ukipiga inafika sehemu husika ila ni mdogo sanaπ€.
.
.
Santos, what man π akupi nafasi ya kugeuka ana hakikisha mpira yote ya hewani ni yake huyu sio Mbrazil, ni Mjerumani mwenye roho kama ya Adolf Hitler πͺ.
.
.
Simba, waliamua kumaliza mechi ndani ya dakika 45 za kipindi cha kwanza walifahamu ugumu wa uwanja huo wa Kaitaba.
.
.
Rudi kwenye ile mechi ukipata mda rudia ile pasi ya Shiboub, kutika ya uwanja, mpaka kumfikia Mohamed Hussein, na kufunga zile huwa tunasema tigo pesa,amenikumbusha ubora wa Lampard, Scholes, Gerrard na Schweinsteiger π.
.
.
Deo Kanda, badae anaweza akawa CD, ana maamuzi ya haraka kwenye, nimeona utofauti leo wa Miraji na Kanda, akae chini na kujitafsiri. .
.
NB, mwenye namba ya Mecky Mexime, anipe kuna swali nataka nimuulize kwa nini alimuacha nje Juma Nyoni, na kumuingiza kipindi cha pili.
.
.
@azizi_mtambo_15 wa @sokaplace__

















KAMATA RATIBA YA SOKA LEO.

