VAR yakataa bao la.samatta

Usiku wa jana Mtanzania Mbwana Samatta aliiongoza klabu ya KEC Genk kuikabili Liverpool kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya

Haukuwa usiku mzuri sana kwa Genk iliyokubali kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa mabingwa hao wa Ulaya

Watanzania wengi waliushuhudia mchezo huo kupitia runinga zao

Samatta alifanikiwa kufunga bao lakini waamuzi wa VAR walilikataa katika mazingira ya kutatanisha

Kumekuwa na mjadala ambapo baadhi ya wachambuzi nguli duniani wameshangazwa na kukataliwa kwa bao hilo

Nyota wa zamani wa timu ya Taifa ya Uingereza Gary Leneker ambaye sasa anafanya kazi kituo cha televisheni cha BT Sports ni miongoni mwa walioshangazwa na kukataliwa kwa bao hilo

“RASHFORD RONALDO MPYA”

Mfululizo wa kupachika Magoli muhimu kwa Timu ya Taifa ya England na Klabu yake ya Man United hivi karibuni kwa msimu huu wa 2019/2020 imemtambulisha upya kinda Marcus Rashford Kama mmoja ya Nyota vijana wakutazamwa Sana katika Soka Ulimwenguni kwa Sasa. .

ALHAMISI hii Mashetani wekundu watatua Nchini Ubelgiji kukipiga na Partizan Belgrade katika Europa League mapema saa 1:55 usiku.Mechi hii itaoneshwa LIVE kupitia STARTIMES pekee kwenye chaneli ya World Football. Je, Rashford ataiongoza Vema Man United katika Mchezo huu?

@startimestz @startimestz @europaleague

#wapendasokaupdates

SIMBA YAICHAPA AZAM, YAZIDI KUJIKITA KILELENI VPL

Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara timu ya Simba imeibuka na ushindi wa bao moja dhidi ya Azam FC katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom, Tanzania bara uliofanyika uwanja wa Taifa.

Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha pointi 15 ikishinda mechi zake zote tano za awali wakiwa kileleni mwa msimamo wa VPL.

Mchezo haukuanza kwa kasi sana kama ilivyo kawaida kwa mechi kubwa ingawa Simba ilifika mara nyingi zaidi kwenye lango la Azam kipindi cha kwanza.

Wachezaji wa Azam walionekana kupaniki hali iliyomfanya mwamuzi Hance Mabena kutoka Tanga kuwaonya kwa kadi ya njano Frank Domayo, Bruce Kangwa, Daniel Amoah na Obrey Chirwa katika kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili Simba ilirudi kwa kasi na iliwachukua dakika nne kupata bao hilo la ushindi lililofungwa na Meddie Kagere kwa kichwa baada ya kupokea pasi ya Francis Kahata.

Baada ya bao hilo kasi ya mchezo iliongezeka na timu zote zikishambuliana kwa zamu lakini hukuna timu iliyopata bao.

Kocha wa Azam, Idd Cheche aliwatoa Richard Djodi, Joseph Mahundi na Frank Domayo na kuwaingiza Shaban Chilunda, Idd Seleman na Donald Ngoma wakati Simba iliwapumzisha Hassan Dilunga, Sharaf Shiboub na Kahata nafasi zao zikachukuliwa na Clatous Chama, Miraji Athumani na Ibrahim Ajibu.

#wapendasokaupdates

Mambo kadhaa yaliyojitikeza.katika.mchezo wa simba vs Azam

Mambo kadhaa niliyoyaona kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara kati ya Simba dhidi ya Azam.
.
.
Kipindi cha kwanza Azam, walifanikiwa kuwazuia Simba, eneo la kiungo kwa asilimia 70 walikuwa matumizi ya nguvu wanashambulia kutumia mpira mirefu huu ndo ulikuwa mpango sahihi kwa aina ya viungo wa Simba. .
.
Yule Yakubu Mohamed, moja ya mabeki bora wa kati wenye uwezo mkubwa wa kukaba kushambulia mpira wowote duniani anaweza kucheza leo ndo nimemtizama kwa umakini wa hali ya juu.safu yake ya ulinzi ilikuwa chini yake. .
.
Obrey Chirwa, sio mshambuliaji wa kati lakini leo amecheza eneo la ushambuliaji la kati kipindi cha kwanza Mwalimu Cheche, aligundua mabeki wa kati hawana spidi, bahati nzuri amekutana na Nyoni, mwenye uzoefu wa mechi kubwa🙌.
.
.
Richard Djodi, kipindi cha kwanza kama angekuwa makini zile nafasi, walizotengeneza Azam, huenda angeamua mechi mpira mingi iliyokufa alishindwa kuitumia ukirudia mechi huenda akajilaumu sana.
.
.
Iddi Cheche, sijajua kwa nini leo ameanzisha nje Iddi Nado, na Donaldo Ngoma, mabadiliko yao yaliwapa faida sana Azam eneo la ushambuliaji mda haukuwa rafiki kwao.
.
.
Fraga, ni Mbrazil ambaye wakati anakuja wengi walimuona ni mchezo wa kawaida sana anajua kukaba anacheza eneo lake la chini akai na mpira sana huyu Brazil, anaendelea kuonyesha ubora wake.
.
.
Mzamiru Yassin, dar 🙌 kiungo anayetumika juu ya Fraga, anapiga pasi za macho anashambulia ana spidi ila wachache sana ndo wanamuongelea.
.
.
Gadiel Michael, some how leo amekuwa bora kokote kwenye kufanya majukumu ya ulinzi na kushambulia, aendelea kujifunza hila eneo la battle bado kuna kazi kubwa baina yake na Mohamed Hussein. .
.
Kahata, ni mchezaji mzuri sana amekosa spidi tu anajua kuficha mpira mguuni na kuwafungua mabeki wa timu pinzani.
.
.
NB:huyu mwamuzi wa leo me nadhani tuwaachie TFF, amechezesha kimazoea na sio kiweledi. .
.
✍🏻 @azizi_mtambo_15 Wa @sokaplace_

Jose Mourinho kutangazwa kocha mkuu. .Borussia Dortmund

🇵🇹 Benfica
🇵🇹 União de Leiria
🇵🇹 FC Porto
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Chelsea
🇮🇹 Inter Milan
🇪🇸 Real Madrid
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Chelsea
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Manchester United
🔄 Borussia Dortmund

✍🏻 Borussia Dortmund wanamtazama, Jose Mourinho kuja kuwa kocha wao Mkuu kama kocha wa Sasa, Lucien Favre atashindwa kuirudisha timu kupata Matokeo ya Ushindi… Dortmund katika msimamo wa Bundesliga mpaka sasa wanakaa katika nafasi ya nne, mechi Sita zilizopita za Mashindano yote, wameshinda tatu (1 ya Champions league) na sare Tatu (1 ya Champions league).

– Ripoti iliyotolewa na SportBild ni kuwa Mourinho yupo katika Mazungumzo ya awali na Mabosi wa BvB kuja kuifundisha klabu hiyo ya Ujerumani..
#transfersUpdates #bvb
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started