Fraga awa gumzo

ABDULAH MKEYENGE

NAPENDA kumtazama kiungo Mbrazil wa Simba Gelson Fraga. Ni kiungo anayejua kutimiza vyema majukumu yake. Mpira ukiwa mguuni mwake hakai nao hata kwa sekunde kumi anautoa kuupeleka kwingine. Viungo wa kileo ndiyo wanacheza hivi.

Kuna sehemu tunajidhulumu tunapomtazama Fraga, kibaya zaidi tumeamua kumdhulumu na Fraga mwenyewe. Tunamtaka afanye zaidi ya anachotuonyesha. Kiungo wa chini hapaswi kuwa na mambo mengi mguuni. Kwake mpira unatakiwa kuwa njia kuelekea kwa mtu mwingine.

Ubrazil wa Fraga unamuhukumu mbele ya mboni zetu. Tunapoambiwa mchezaji anatokea Brazil, picha ya kwanza inayotujia ni Ronaldinho Gaucho.

Tunamtaka Fraga awe kama Gaucho. Amekuja na aina nyingine ya mchezo tunamuona mchezaji wa hovyo asiyestahili kuvaa jezi ya Simba. Watanzania tumechelewa kujua mpira, mbaya zaidi hatutaki kujifunza mpira wenyewe ulivyo. Tukiwa na msimamo wetu ni ngumu kutubadili.

Fraga anacheza basic football. Haupandi mpira, hampigi mtu tobo, kanzu. Mchezaji aliyepitia academy katika eneo lake anatakiwa acheze vile anavyocheza. Namba sita si sehemu ya kuuchezea sana mpira. Si sehemu salama mpira ukipotea.

Ubrazil wa Fraga umefanya tutake kumsuta. Tuna lundo la maswali kila tunapomtazama. Swali letu kuu inakuwaje Fraga hana udambwi kama Ajib ambaye ni Mtanzania mwenzetu? Hili ni swali tunalolijiuliza kila leo. Tumekwamia hapa.

Hatumtazami kiufundi. Tumebaki kumuhukumu na uraia wake. Usipomtazama Fraga kiufundi unaweza usilione jukumu lake kiwanjani kutokana na kukosa mboga mboga mguuni mwake.

Fraga anawafanya walinzi wa Simba wawe salama. Hatembei eneo kubwa. Anachokifanya ni kusimama mbele ya mabeki wanne na kuwalinda.

Unamuona Mbwana Samatta dhidi ya Wazungu? Anawatesa Wazungu kadri anavyojisikia. Lakini Wazungu wanamfurahia na kuushangaa Utanzania wake. Wengi walidhani anatokea Afrika Magharibi au Kaskazini. Hawaamini kama katoka Tanzania.

Garry Lineker jana katikati ya wachambuzi wake studio (Peter Crouch, Rio Ferdinand, Robin Van Parsie) alimshangaa Mbwana kama sisi tunavyomshanga Fraga. Hajamshangaa kwa ubaya.

Tofauti ya Lineker na sisi ni kwamba, Lineker ameshangazwa na kiwango cha Mbwana. Sisi hatuishii kumshangaa Fraga, pia tunamuona hana analolijua kabisa. Tumechelewa kujua mpira.

Katika nchi ambayo haijawahi kushinda Kombe la Mataifa Afrika, haijawahi kufuzu Kombe la Dunia wala kukaribia kufuzu, mashabiki wa nchi yake wanatoa wapi ujasiri wa kutambua mchezaji bora?

Muda huu tunaomshangaa Mbrazil Fraga kwa kumuona hajui, wacha Wazungu waendelee kuufurahia ubora wa Mtanzania Samatta.

Unai Emery asema ameifanya Arsenal iwe bora.

Leo Arsenal wanacheza Europa League Live on @StartimesTZ dhidi ya Victoria FC. Kwenye mkutano na waandishi wa habari kocha wa Arsenal anasema kwamba ameifanya Arsenal imekua bora kwa sasa.
.
Unai alisema,”Wakati nafika hapa timu ilikua na historia ya kushinda 1-0 na kuonekana kama inashindana, lakini hiyo ilikua haitoshi. Kitu nilichofanya ni kuongeza uwezo wa timu kushindana na kuonyesha ubunifu uwanjani.” .

Akaendelea kusema,”Mashabiki ni wengi na wanataka vitu kwa mawazo tofauti tofauti.Wengine wanataka kuona ubunifu uwanjani, wengine wanataka kuona nguvu nyingi uwanjani. Mimi nataka vyote kwa pamoja. Lakini wakati mwingine wachezaji wanapungukiwa kimoja wapo”. .
Oky, Leo usiku kwenye mechi yao dhidi ya Victoria sijui tutaona nguvu nyingi au ubunifu uwanjani. Muda ni Saa 4 usiku kupitia channel ya World Footaball ya @StartimesTz

Siku kama ya leo Manchester United walimaliza “49 Unbeaten” ndani ya Old Trafford.

Siku kama ya leo Manchester United walimaliza “49 Unbeaten” ndani ya Old Trafford. Arsenal ilikua ya moto na Manchester United ilikua ya moto. Ngoja nikukumbushe vikosi.

Manchester United: Carroll; G. Neville, Ferdinand, Silvestre, Heinze; Ronaldo (Smith-85), P. Neville, Scholes, Giggs; Rooney, Van Nistelrooy (Saha-90)
.
Arsenal: Lehmann; Lauren, Campbell, Toure, Cole; Ljungberg, Vieira, Edu, Reyes (Pires-70); Bergkamp, Henry
.
Mechi iliisha Manchester United 2-0 Arsenal, magoli yalifungwa na Van Nisterlrooy kwa penati na Rooney dakika ya 90.
.
Imebaki historia may be itajirudia kuona competitive Arsenal na Manchester United kama zile.

Mashabiki wa Liverpool wapotea, wameenda Gent badala ya Genk

.
Mashaiki wawili wamesafiri kutoka nchini kwao hadi Belgium kwa ajili ya mechi ya Liverpool. Lakini wakaenda Gent badala ya Genk.
.
Nusu saa kabla ya mechi wakaanza kutafuta uwanja ulipo. Wakaenda kwenye uwanja wa Gent na kuona hali sio kama ya Champions League. .
Baada ya kuuliza wakaambiwa huo ni uwanja wa Gent sio Genk. Wakiwa na ticket zao mkononi ikawa too late kuwai uwanjani Genk.
.
Wakajisogeza kwenye pub ya karibu na kuangalia mechi kwenye Tv.

Manchester united kibaruani Leo europeleague

Huu ni mchezo mwingine mgumu kwa Manchester United baada ya kumalizana na Liverpool katika ligi kwa sare ya 1-1.
Harry Maguire ana matumaini kwamba matukio ya ubaguzi wa rangi hayatojirudia kama ilivyokuwa katika mchezo wa England vs Bulgaria.
.
.
TeamNews: David De Gea na Paul Pogba hawajasafiri na timu kwenda Belgrade wakiuguza majeraha, wanaungana na Diogo Dalot, Luke Shaw, Nemanja Matic, Timothy Fosu-Mensah, Axel Tuanzebe na Eric Bailly.
Lakini Jesse Lingard amerudi kikosini na amesafiri na timu, Ethan Laird ameongezwa kwenye kikosi na golikipa wa timu ya U23 Matej Kovar nae ameenda Serbia.
Kwa upande wa Partizan, winga wa zamani wa Liverpool Lazar Markovic hatocheza kutokana na majeruhi, wakati kiungo Seydouba Soumah pia ana hatihati kutokana na utimamu wa afya..
.
.
Takwimu: •Wakati pekee ambao FK Partizan na Manchester United zilikutana ilikuwa msimu wa 1965-66 katika nusu fainali ya European Cup. Partizan walishinda 2-0 nyumbani kisha wakafungwa 0-1 na kusonga mbele kwenda fainali.
.
.
• Huu ni mchezo wa kwanza wa Man Utd dhidi ya timu kutoka Serbia tangu mwaka 1991 katika mashindano ya European Super Cup, ambapo waliwafunga Red Star Belgrade 1-0.
.
.
• Manchester United hawajafungwa katika mechi 13 za Europa League tangu walipofungwa na Fenerbahce mnamo November 2016 (W9 D4) – wamepata clean sheet 9 katika mechi hizo – hawajawahi kufungwa zaidi ya goli moja katika mechi hata moja.

RATIBA YA SOKA LEO.

#TanzaniaVodacomPrimierLeague
16:00 Mbeya City Vs Kagera Sugar :
#UefaEuropaLeague
19:55 Qarabag FK vs APOEL Nicosia
22:00 Sevilla vs F91 Dudelange
22:00 Dynamo Kyiv vs FC Koebenhavn
22:00 Malmoe FF vs Lugano
22:00 Getafe vs Basel
22:00 Trabzonspor vs FC Krasnodar
22:00 PSV Eindhoven vs LASK
22:00 Sporting CP vs Rosenborg
22:00 Celtic vs Lazio
22:00 Rennes vs CFR Cluj
22:00 Arsenal vs Vitoria de Guimaraes
22:00 Eintracht Frankfurt vs Standard Liege
19:55 FC Porto vs Rangers
19:55 Young Boys vs Feyenood
19:55 CSKA Moscow vs Ferencvaros
19:55 Ludogorets Razgrad vs RCD Espanyol
19:55 Gent vs Wolfsburg
19:55 Saint-Etienne vs Oleksandriya
19:55 Istanbul Basaksehir vs Wolfsberger AC
19:55 Roma vs Borussia Mönchengladb..
19:55 Besiktas vs SC Braga
19:55 Slovan Bratislava vs Wolverhampton
19:55 AZ Alkmaar vs FC Astana
21:55 Partizan Beograd vs Manchester United
:
#AfricaChampionsLeague
21:00 El Zamalek vs Génération Foot
:
#MoroccoBotolaPro
19:00 Raja Casablanca vs Raja Beni Mellal
:
#TunisiaLigue I
16:30 Esperance vs Ben Guerdane
16:30 Etoile Metlaoui vs Club Africain
16:30 US Tataouine vs Etoile du Sahel

Imeandaliwa na @officialchristz Wa @sokaplace_

MATOKEO YA SOKA JANA

#TanzaniaVodacomPrimierLeague
FT Ndanda SC 1-1 Lipuli FC (Kigi Makasi 74’ : Paul Nonga 42’)
FT Polisi Tanzania 1-0 Mwadui FC (Baraka Majogoro 76’)
FT Namungo FC 1-0 Mtibwa Sugar (Bigirimana Blaise 39’)
FT Alliance FC 1-0 Ruvu Shooting (Israel Patrick 19’)
FT Tanzania Prisons 0-0 Biashara United
FT Coastal Union 0-0 Singida United.
FT Simba Sc 1-0Azam Fc
:
#UefaChampionsLeague
FT Genk 1 – 4 Liverpool
FT Salzburg 2 – 3 Napoli
FT Inter 2 – 0 Borussia Dortmund
FT Slavia Prague 1 – 2 Barcelona
FT RasenBallsport Leipzig 2 – 1 Zenit St. Petersburg
FT Benfica 2 – 1 Lyon
FT Ajax 0 – 1 Chelsea
FT Lille 1 – 1 Valencia
:
#EnglandChampionship
FT Bristol City 2 – 1 Charlton Athletic
FT Derby County 1 – 0 Wigan Athletic
FT Fulham 3 – 2 Luton Town
FT Huddersfield Town 0 – 0 Middlesbrough
FT Nottingham Forest 1 – 2 Hull City
:
#AlgeriaLigue1
FT AS Ain Mlila 3 – 0 US Biskra
FT MC Alger 3 – 0 NA Hussein Dey
FT USM Alger 3 – 0 CA Bordj Bou Arreridj
FT ES Setif 0 – 1 ASO Chlef
FT MC Oran 0 – 1 Paradou AC
FT USM Bel Abbes 0 – 1 CR Belouizdad
FT CS Constantine 3 – 1 JS Kabylie
FT JS Saoura 3 – 0 NC Magra
:
#MoroccoBotolaPro
FT MCO Oujda 1 – 1 Wydad Casablanca
:
#SouthAfricaPremierLeague
FT Mamelodi Sundowns FC 1 – 0 Highlands Park FC
:
#TunisiaLigueI
FT AS Slimane 1 – 2 CS Hammam-Lif
FT CA Bizertin 1 – 2 CS Sfaxien
FT JS Kairouanaise 0 – 1 Stade Tunisien
FT US Monastir 2 – 0 Sportif de Chebba
:
Imeandaliwa na @officialchristz
Wa @sokaplace_
Powered by @bikotanzania

Klabu ya Flamengo 🇧🇷 itacheza fainali ya Michuano ya Copa Libertadores kwa mara yao ya Pili

1981 – Klabu ya Flamengo 🇧🇷 itacheza fainali ya Michuano ya Copa Libertadores kwa mara yao ya Pili katika historia, Walicheza mara ya mwisho mwaka 1981 na kuibuka kuwa Mabingwa katika Ushiriki wao wa kwanza Pia.

– Alfajiri wakiwa nyumbani, wametoa dozi nzito ya Magoli 5-0 kwenda kwa ndugu zao Grêmio 🇧🇷; kwa Ushindi huo wanafuzu fainali kwa Ushindi wa Jumla 6-1 baada ya Sare ya 1-1 katika mechi ya kwanza.

– Tangu wameanza Kushiriki Michuano hii ya Copa Libertadores, Grêmio hawajawahi kufungwa kwa idadi ya Magoli 5+; kipigo hiki ndio mara ya kwanza katika historia yao..
#CopaLibertadores #OlaFla #Gremio
@Harunlugoyah

Simba kucheza mechi.tano siku 15

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam Fc jana, kikosi chake kitakuwa na kazi ya kuhakikisha kinabaki kileleni mwa msimamo wa ligi ambapo wanakabiliwa na ratiba ngumu ya kucheza mechi tano katika kipindi cha siku 16

Aussems amesema haitakuwa jambo jepesi hasa ikizingatiwa mechi za mikoani zitapigwa katika viwanja vizivyo rafiki

“Wengi walikuwa wakiutazamana mchezo huu dhidi ya Azam kuwa ndio mgumu zaidi kwetu lakini si kweli. Tumecheza katika uwanja mzuri hivyo tuliweza kutimiza mpango wetu wa mchezo lakini hali ni tofauti tunapoenda kucheza viwanja visivyo rafiki”

“Nimewaambia wachezaji wangu tunakabiliwa na ratiba ngumu ya kucheza mechi tano ndani ya siku 16 lengo letu ni kuhakikisha tunaendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya michezo hiyo,” amesema

Simba inatarajiwa kuelekea mkoani Arusha kuifuata Singida United ambayo imehamia huko kwa muda baada ya uwanja wa Namfua kuzuiwa na TFF

Jumapili Oktoba 27 timu hizo zitachuana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid

Baadae Simba itaelekea mkoani Shinyanga ambako Oktoba 30 itachuana na Mwadui Fc

Design a site like this with WordPress.com
Get started