RASMI ZAHERA ATUPIWA VIRAGO YANGA ARITHI MKWASA

Uongozi wa klabu ya Yanga umethibitisha kuachana na kocha wao mkuu Mwinyi Zahera pamoja na benchi zima la ufundi baada ya kushindwa kufanya vizuri.

Uamuzi huo umetangazwa mbele ya Waandishi wa Habari makao makuu ya klabu hiyo na Mwenyekiti, Dk. Mshindo Msola ambapo kwa sasa timu hiyo itakuwa chini ya kocha wa muda Charles Mkwasa.

Taarifa za awali zilikuwa zinasema kocha wa Bandari FC ya Kenya, Ben Mwalala ndiye atakaye chukua nafasi ya Mkongomani huyo lakini Dk. Msola amemtangaza Mkwasa mchana huu.

Kibarua cha kwanza cha Mkwasa kitakuwa siku ya Ijumaa kitaposhuka dimbani kuikabili Ndanda katika uwanja wa Nangwanda.
#wapendasokaupdates

RATIBA YA 16 BORA KOMBE LA DUNIA LA FIFA U17: 🇧🇷 2019 •

■Hatua ya makundi imemalizika kwa Afrika kuingiza timu 3 katika hatua ya mtoano:
Nigeria 🇳🇬 ✅
Senegal 🇸🇳 ✅
Angola 🇦🇴 ✅
Cameroon ❎

■Hatua ya mtoano inaanza leo:
5 Nov: Angola vs South Korea, Nigeria vs Netherland

6 Nov: Japan vs Mexico, Spain vs Senegal, Brazil vs Chile, France vs Australia

7 Nov: Ecuador vs Italy, Paraguay vs Argentina

#U17WC🏆?

Lampard, sasa N’Golo Kante yupo fiti kwa UEFA

OFFICIAL: Kocha Mkuu wa Klabu ya Chelsea, Frank Lampard, Amethibitisha kuwa kiungo wake wa Kimataifa wa Ufaransa, N’Golo Kante yupo fiti na atakuwa katika Kikosi cha klabu hiyo ambacho kesho kitacheza mechi ya Marudiano ya hatua ya Makundi ya Michuano ya UEFA Champions League dhidi ya AFC Ajax..
#chelsea #ajax #championsleague

Arsenal europe jumatano badala ya alhamis

✍ Arsenal itacheza mechi yake ya hatua ya Makundi ya Europa League dhidi ya Vitoria SC siku ya Jumatano na Sio Alhamisi ili kuepusha msongamano wa magari nchini Ureno… Game hii itapigwa Saa 18:50 siku ya kesho Novemba 06, siku moja kabla ya mechi zingine 23.
..
✍ Wapinzani wa Vitoria huko Ureno, Braga itawakaribisha Besiktas kwenye Uwanja wa Manispaa siku ya Alhamisi, takribani maili 15 kutoka ulipo uwanja wa Vitoria… Kwa kusogeza mbele mchezo wa Arsenal, UEFA inatarajia kuipunguzia kazi mamlaka ya Ureno na kuepuka foleni za Mashabiki watakaotaka kuingia katika Viwanja hivyo viwili tofauti.
..
✍ Mbali na kusogeza mbele mchezo huo pia Utaanza mapema ili kuepuka muingiliano kati ya watangazaji na Ligi ya Mabingwa ambapo mechi kadhaa zitapigwa siku hiyo ya kesho… Mechi za Europa League kawaida huchezwa Alhamisi saa 20:55 au 23:00..
#Arsenal #EuropaLeague
@Harunlugoyah

RATIBA YA SOKA LEO +MATOKEO YA SOKA JANA

:
#UefaChampionsLeague
23:00 Liverpool vs Genk
23:00 Napoli vs Slazbarg
20:55 Barcelona vs Slavia Prague 23:00 Borussia Dortmund vs Inter
20:55 Zenit St. Petersburg vs RasenBallsport Leipzig
23:00 Lyon vs Benfica
23:00 Chelsea vs Ajax
23:00 Valencia vs Lille
:
#AfricaConfederationsCup
18:00 Esae vs Generation Foot
:
#MoroccoBotolaPro
17:00 Renaissance Club Zemamra vs Raja Casablanca
:
#SouthAfricaPremierLeague
20:30 Bloemfontein Celtic vs Highlands
:
#World Cup U-17 – Play-off
22:30 Angola vs Korea Republic
:
Kamata Matokeo ya Soka Jana :
#VodacomPrimierLeague
FT Azam Fc 0-0 Kagera Sugar
FT KMC 2-1 Biashara Mara :
#Tanzania FDL
FT Boma Fc 0-1Ihefu Fc
:
#EnglandChampionship
FT Stoke City 0 – 2 West Bromwich
:
#ItalySirie A
FT SPAL 0 – 1 Sampdoria
:
#World Cup U-17
FT Italy 1 – 2 Paraguay
FT Mexico 8 – 0 Solomon Islands
:
Prepared by @officialchristz
Powered by @bikotanzania

Design a site like this with WordPress.com
Get started