JKT TANZANIA .MECHI YETU NA SIMBA NI NGUMU SANA

ABDALLAH Mohamed ‘Bares’, Kocha mkuu wa JKT Tanzania amesema kuwa mchezo wa kesho mbele ya Simba ni mgumu ila kikosi kipo tayari kupata ushindi.

JKT Tanzania itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kufungwa mabao 3-1 na Simba kwenye mechi ya kwanza iliyochezwa Uwanja wa Uhuru.

Akizungumza na Saleh Jembe, Bares amesema kuwa wachezaji wapo tayari kupata matokeo mazuri mbele ya Simba.

“Ni mchezo mgumu kwetu hilo lipo wazi ila halitukatishi tamaa kwamba hatuwezi hapana, tupo tayari na tumejipanga kuona namna gani tushinda mbele ya Simba na kuzipata pointi tatu.

“Morali ya wachezaji ni kubwa na kila kitu kipo sawa tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kushuhudia burudani,” amesema.

AZAM KUHAMISHI HASIRA ZA PRISONS KWA KMC

UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa utapambana kupata pointi tatu muhimu mbele ya KMC watakapokutana kesho, Februari,8, Uwanja wa Uhuru.

Azam FC itashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kubanwa mbavu na Tanzania Prisons kwa kufungana bao 1-1 mchezo wao uliochezwa Uwanja wa Uhuru huku KMC ikiitandika bao 1-0 Mbeya City, Samora.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Azam FC Jaffary Maganga amesema kuwa wanaitambua vema KMC ni timu imara wataingia kwa tahadhari kubwa.

“Ni timu nzuri KMC ila tutawafuata kwa tahadhari kubwa ili kuona namna gani tutashinda mchezo wetu na kuchukua pointi tatu muhimu,” amesema.

Mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Uhuru wakati huo KMC ikiwa chini ya Jackson Mayanja na Azam chini ya Ettiene Ndayiragije, Azam ilisepa na pointi tatu muhimu.

RUVU SHOOTING YAIPIGA MKWARA MWINGINE YANGA, YATAKA MABAO MENGI KINOMA

MASAU Bwire, Ofisa Habari wa Ruvu Shooting amesema kuwa wanahitaji kushinda mbele ya Yanga kwa mabao zaidi ya mawili kwa kuwa wanajiamini.

Kesho, Uwanja wa Taifa, saa 1:00 usiku, Ruvu itamenyana na Yanga ikiwa na kumbukumbu ya kuwatungua kwa bao 1-0 mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, bao pekee la ushindi lilifungwa na Sadat Mohamed.

Bwire amesema kuwa:-“Tupo imara na tunatambua kwamba tutakutana na Yanga ambao nao wapo vizuri hilo halitupi shida, tunaendelea na kampeni yetu ya kupapasa kama ilivyo ada.

“Tumeshinda mchezo wetu kwa bao 1-0 mbele ya Mtibwa Sugar, hatujafurahi kwani ni ushindi mdogo tunapenda kushinda mabao zaidi ya mawili kwani uongozi upo pamoja nasi na wachezaji wanapambana,”.

Vandenbroeck mtegoni dhidi ya JKT Tanzania

Kocha Mkuu wa Simba Sven Vandenbroeck leo atakiongoza kikosi chake kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ruvu Shooting

Mchezo huo utapigwa saa kumi jioni kwenye uwanja wa Uhuru

Vandenbroeck yuko kwenye presha kubwa kutokana na mwenendo ambao timu imekuwa ikionyesha chini yake licha ya kupata matokeo

Inaelezwa mabosi wa Simba tayari wako mguu sawa kusaka mbadala wake kama mambo hayatabadilika

Mchezo wa leo dhidi ya JKT Tanzania unaweza kuwa mtihani wake wa kwanza, wanahitaji kuona Simba ikicheza vizuri na kupata ushindi

Matokeo tofauti na ushindi huenda yakapunguza siku zake za kuendelea kubaki kunako mabingwa hao wa nchi

Mbelgiji huyo leo anaweza kukirejesha dimbani kikosi kilichopata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union

Katika mchezo huo Simba ilitumia mfumo wa 4-4-2 ambao ulijumuisha washambuliaji wawili

Simba kuanza mzunguko wa pili kwa kuwavaa JKT Tanzana

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba ambao ndio vinara wa ligi kuu, leo wanaanza mzunguko wa pili wa Ligi hiyo kwa kuwakaribisha ‘Maafande’ wa JKT Tanzania katika mechi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini, Dar es Salaam.

Simba itashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu ya kupata ushindi mfululizo wa mechi tano wakati JKT Tanzania wao wametoka kubanwa nyumbani kwa kulazimishwa sare dhidi ya Coastal Union kutoka jijini Tanga.

Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, amesema kikosi kiko tayari na kamili kwa mchezo huo na kuitaja JKT Tanzania ni moja ya timu zenye wachezaji walioimarika na wenye kutoa ushindani kwa klabu pinzani.

Matola alisema wamewaandaa wachezaji wao kupambana katika mechi zote kwa sababu hatua ya lala salama ndio wakati wa kukamilisha ‘hesabu’ za ubingwa.

Alisema hakuna mechi rahisi na hakuna timu ndogo katika Ligi Kuu Tanzania Bara, hivyo watakuwa makini katika kila mpira watakaokuwa nao wachezaji wake.

“Ni mechi ngumu, hatutarajii kitu kingine, msimu huu na hasa mzunguko huu mambo yatazidi kuwa magumu, kila timu inahitaji kukamilisha malengo yake, bado hakuna ambaye yuko salama, walioko chini wanataka kukimbia na walioko chini yetu wanatukimbiza,” Matola alisema.

Nahodha na kiungo huyo wa zamani wa Supersport ya Afrika Kusini alisema wanahitaji kuendeleza matokeo mazuri katika kila mechi ili watangaze ubingwa mapema.

“Hatutaki presha huko mbele, ukifanikiwa kushinda mechi nyingine tano za mzunguko wa kwanza, unakuwa nafasi salama, dua na mipango yetu ni kutoangusha pointi katika mechi hizi za nyumbani, tumejiandaa kukabiliana na kila ushindani,” alisema Matola.

Naye Meneja wa timu hiyo, Patrick Rweyemamu, alisema wachezaji wote wapo salama na wanaendelea kujipanga kwa ajili ya mechi hiyo ya leo.

“Tuliendelea na mazoezi kama kawaida, kama unavyojua kwa sasa huwezi kufanya mazoezi magumu, mwalimu huangalia na kuwapa mbinu zake za kiufundi baada ya kurekebisha makosa ya mchezo uliopita, tuko vizuri, tunaamini tuna nafasi ya kupata pointi tatu nyingine,” alisema Rweyemamu.

Aliongeza kuwa nyota wao wawili, Shiza Kichuya pamoja na Luis Miquissone, tayari wamepata ITC na uwezekano wa kuonekana uwanjani leo utatokana na uamuzi wa Kocha Mkuu Mbelgiji Sven Vandenbroeck.

Baada ya mechi ya leo, Simba itasafiri kwenda Morogoro kuwafuata Mtibwa Sugar katika mechi nyingine ya ligi hiyo itakayochezwa Jumanne na Februari 15, mwaka huu watakuwa ugenini Iringa kuwakabili Lipuli FC kwenye Uwanja wa CCM Samora mkoani humo.

SAMATTA AENDA KUJIFUA KIVYAKE DUBAI BAADA YA KUPEWA MAPUMZIKO MAFUPI ASTON VILLA

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta akinywa maji baada ya mazoezi makali gym jana Dubai. Samatta yupo Dubai akitumia kipindi cha mapumziko mafupi ya klabu yake katika Ligi Kuu ya England kujifua binafsi kujiweka fiti zaidi ili aweze kumudu mikiki ya ligi hiyo.

Baada ya kufunga kwenye mechi yake ya kwanza EPL mwishoni kwa wiki iliyopta, Aston Villa ikichapwa 2-1 na wenyeji, AFC Bournemouth Uwanja wa Vitality akina Samatta hawatakuwa na mchezo mwingine hadi Jumapili ijayo, watakapoikaribisha Tottenham Hotspur.

Kazi na dawa; Hapa Mbwana Samatta akicheza kwenye ngamia baada ya mazoezi

Visit website

MBELGIJI SIMBA ATOA SABABU ZA TIMU YAKE KUBORONGA KIWANGO

MASHABIKI wa Simba wameonyesha hasira huku wakidai hawaelewi kinachoendelea kwenye timu yao haswa kwenye kiwango na aina ya matokeo.
Lakini kocha mkuu wa timu hiyo, Mbelgiji, Sven Vanderboeck amesema hata kubana kwa ratiba kunachangia.
Kocha huyo amesema hayo kutokana na ushindi wa mabao ya dakika za mwisho ambayo walioupata kwenye mechi dhidi ya Mwadui, Namungo na juzi Jumanne dhidi ya Polisi Tanzania.
“Unapocheza kila baada ya siku mbili kama ambavyo ilivyo kwetu, inapofika kipindi cha pili pale ndiyo mnakuwa na nguvu kubwa sana ya kupata ushindi ndiyo maana unaona inakuwa hivyo kwetu.
“Tuna ratiba ambayo haitupi muda wa kutosha kupumzika kwa hiyo ni lazima tuwe tunapambana kupata ushindi dakika za mwisho, lakini kitu kingine kinachochangia kushinda dakika za mwisho ni kwa sababu ya kufungwa mapema.
“Tunapofungwa mapema tunazidisha juhudi ya kufunga na nina safu nzuri ya washambuliaji ambao wanafanya kile ninachokitaka. Japo hali hii siifurahii sana kwa sababu ninataka tumalize mechi kabla ya kufika muda huo,” alisema.
Katika hatua nyingine, habari za ndani kutoka Simba zinasema kuwa, kocha huyo amewapiga pini wasaidizi wake wote akiwemo kocha mzalendo, Seleman Matola, kuzungumza jambo lolote bila ya ruhusa maalum tofauti na ilivyokuwa awali.
AJIBU ATAJWA
Sven ametamka kuwa sasa ameanza kumuelewa kiungo wake mshambuliaji Ibrahim Ajibu ambaye juzi alitokea benchi na kuisaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi Tanzania.
“Alipoingia Ajibu timu ilionekana kubadilika kwa timu kushambulia goli la wapinzani baada ya kufanyia maelekezo yangu vizuri na yeye nilimtaka kuwalazimisha mabeki kuingia ndani ya 18 ndiyo kitu ambacho alichokifanya kabla ya kufunga bao.
“Ninataka wachezaji wa aina hii ya Ajibu anayecheza kwa kufuata maelekezo yangu kama ilivyokuwa yeye, kuingia kwake kulibadilisha timu nzima kutokana na uwezo wake wa kumiliki mpira huku akilazimisha mashambulizi.
“Nilimuingiza Ajibu baada ya kumuona (Francis) Kahata, (Clatous) Chama wote wamechoka ambao nilikuwa nawategemea katika mchezo huu, hivyo nimpongeze kwa kuiwezesha timu kupata matokeo mazuri.”

Visit website

KUMEKUCHA, MFAUME ATAKA AZICHAPE NA MWAKINYO

Bondia Mfaume Mfaume amesema anataka kupambana na Bondia kutoka mjini Tanga, Hassan Mwakinyo muda wowote akitaka na kwa gharama yoyote anayotaka wakikubaliana.
Mfaume amedai pambano lake na Mwakinyo litakuwa safi sana, amesema anaamini Tanzania itasimama siku hiyo ya pambano. “Mimi binafsi natamani sana kucheza na Mwakinyo, lakini yeye ukimgusia anataja hela kubwa sababu ya hofu”, amesema Mfaume.
“Mimi niko tayari muda wowote, saa yoyote kupigana naye, aseme tu anataka lini mimi nitampiga tu Mwakinyo, nina 100% mbele ya Kocha wangu nitampiga tu, yeye ni mzuri kupigana na mimi mzuri kupigana wote tupo katika Taifa moja”, ameeleza Mfaume.
Mfaume amesema ili mchezo wa ngumi usonge mbele lazima Mabondia wa Taifa moja wacheze wenyewe kwa wenyewe ili mpimane uwezo na ubora katika Ngumi. Amesema ni mwaka wa pili yeye na Mwakinyo wanakimbiana amesisitiza lazima ifike hatua Watanzania wapate radha ya mchezo wa ngumu kwa wao kukutana ulingoni.
“Siku nyingi sana namtafuta Hassan Mwakinyo, saa yoyote, muda wowote mimi niko tayari kupigana naye, aje tu yeye Bondia mzuri lakini mimi mzuri ziadi yake”, amedai Mfaume.
Kwa upande wake, Kocha wa Mfaume Mfaume, Ramadhan amesema kama Hassan Mwakinyo atakubali ilo pambano, lazima atapigwa na Bondia Mfaume Mfaume, “Naamini Mfaume ni Bondia bora sana katika Taifa hili, Mwakinyo lazima atapigwe”, ameeleza Ramadhan.

Visit website

MTAALAMU WA SOKA LA KISASA YANGA ASEPA ZAKE KWAO, KILICHOFANYIKA CHATAJWA

NGULI na mtaalam wa mfumo wa soka la kisasa, Carraca Antonio Domingoz Pinto (pichani), amefikia muafaka na Yanga na amerejea kwao kuweka mambo sawa huku mtaalam mwingine Msauzi, mambo yakinoga.
Mreno huyo, alitua nchini kufanya mazungumzo na GSM ambao ni wadhamini wa Yanga, na kufikia pazuri kabla ya kurejea tena kwa mara pili kuanza kazi Jangwani.
Sasa Yanga inayoelekea kwenye mabadiliko ya kimfumo wa uendeshaji, itakuwa na Wazungu wanne. Wengine ni kocha Mbelgiji Luc Eymael, kocha wa viungo Riedoh Berdien na daktari wa misuli, Faried Cassiem wote kutoka nchini Afrika Kusini ambao wana asili ya Ulaya.
Ujio wa Faried umekuwa raha kwa wachezaji wa Yanga kutokana na umahiri wake kwenye ishu za afya ambako sasa wana uhakika wa kutatua matatizo yao kwa wakati.
Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM, Mhandisi, Hersi Said, alisema; “Alikuja kwa ajili ya makubaliano na majadiliano ambayo tayari tumefikia muafaka mzuri na ndani ya siku hizi mbili haraka atarejea nchini kwa ajili ya kuanza kazi Yanga.
“Amekuja katika projekti tunayoifanya kwenye klabu yetu, hivyo kwa kuliona hilo ndio maana tukamleta mtaalam huyu mwenye uzoefu mkubwa kutoka klabu kubwa ya Benfica.
“Tunaendelea na tutaendelea kufanya vitu vingine ambavyo vipo nje ya mkataba , lengo ni kuendelea kuisaidia timu yetu ya Yanga ili kufikia levo za kimataifa kama zilivyokuwa klabu nyingine kubwa nje na ndani ya Afrika.”

Visit website

MAAMUZI MAGUMU KUFANYIKA NDANI YA SIMBA, MBADALA WA SVEN ATAJWA

Baada ya kikiso cha Simba kuonesha kiwango kilicho butu katika mechi za hivi karivuni, inaelezwa kuwa mabosi wa Simba wapo kwenye mchakato wa kusaka Kocha mwingine.
Timu hiyo inayonolewa na Sven Vandenbroeck ambaye ni raia wa Ubelgiji, imekuwa ikipata matokeo ya kusuasua tangu aanze kuinoa jambo ambalo limeanza kuleta wasiwasi katika mechi za ligi na mashindano ya kimataifa hapo baadaye.
Tetesi zilizopo hivi sasa ni kuwa mabosi Simba wanatajwa kutaka kumleta Kocha wa As Vita, Jean Florent Ibenge ili kuchukua majukumu ya Sven.
Taarifa za ndani zinasema uwezekano mkubwa wa Sven kufutwa kazi upo kutokana na uongozi wa juu, mashabiki na hata wanachama kutofurahishwa na namna mwenendo wa timu hiyo unavyoenda hivi sasa.
Sven alichukua nafasi ya kuinoa Simba baada ya kufutwa kazi kwa Patrick Aussema aliyekuwa akiinoa timu hiyo.

Visit website

Design a site like this with WordPress.com
Get started