
Mlinzi wa kati wa timu ya Taifa ya Tanzania bara ‘Kilimanjaro Stars’ Bakari Mwanyeto amesema mchezo wa kesho wa nusu fainali ya michuano ya Cecafa dhidi ya Uganda watajitahidi wapate ushindi ili kuweka historia.
Mwanyeto ambaye yupo kwenye ubora mkubwa kwa sasa ametengeneza maelewano mazuri na mkongwe Kelvin Yondani kwenye kikosi hicho baada ya kuumia kwa Erasto Nyoni.
Nahodha huyo wa Coastal Union amesema wanafahamu mchezo utakuwa mgumu kutokana na ubora wa Uganda lakini hawatishiki kwa hilo watajipanga kuhakikisha wanashinda na kuingia fainali. “Ukiangalia kikosi chetu wengi ni vijana na tunahitaji kupata ubingwa ili kuweka historia. Uganda wana timu nzuri na ni wenyeji kwahiyo tumejipa kuhakikisha hatuwapi nafasi ya kutuadhibu na kutumia nafasi tutakazopata kuwaadhibu,” alisema Mwamnyeto.
Mara ya mwisho Kili Stars kuchukua ubingwa wa michuano hiyo ilikuwa mwaka 2010 ambayo ilifanyika hapa jijini Dar es Salaam.
#wapendasokaupdated
#CecafaSeniorChallengeCup
Arsenal 0-3 Man City
.












:
:
.

