
Uongozi wa klabu ya Azam umethibitisha kuwa umemalizana na Yanga juu ya usajili wa mshambuliaji Ditram Nchimbi aliyekuwa anacheza Polisi Tanzania kwa mkopo.
Nchimbi yupo nchini Uganda na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania bara ‘Kili Stars’ kinacho shiriki michuano ya Cecafa Senior Challange.
Msemaji wa klabu hiyo, Jaffer Iddi amesema Yanga iliwaandikia barua juu kutaka huduma ya mshambuliaji huyo aliye kwenye kiwango bora kwa sasa na baada ya kumuuliza Nchimbi mwenyewe amewajibu yupo tayari kujiunga na mabingwa hao zamani wa Tanzania.
Jaffer ameongeza kuwa Nchimbi alikuwa amebakisha mkataba wa miezi sita na walikuwa na nia ya kumuongeza lakini baada ya mwenyewe kukubali kujiunga na Yanga na wamelipa kiasi walicho kubaliana wameamua kumuachia mchezaji huyo. “Sasa ni rasmi Ditram Nchimbi ni mchezaji halali wa Yanga, wametulipa pesa tuliyo kuwa tunaihitaji na mchezaji mwenyewe amekubali kujiunga na Yanga kwahiyo ni sasa ni mchezaji wao,” alisema Jaffer.
#wapendasokaupdates

👉SpainLaLigaSantander







