Kocha mkuu wa Ruvu Shooting Salum Mayanga amesema atawasajili wachezaji wawili wa Milambo

Tetesi Bongo: Kocha mkuu wa Ruvu Shooting Salum Mayanga amesema atawasajili wachezaji wawili wa Milambo ambao ni beki wa kati Pascal Paul na mshambuliaji, Evarist Tembo, Mayanga amesema ameridhishwa na viwango vyao katika mechi dhidi yao Kombe la Shirikisho ambapo Ruvu Shooting walishinda goli 1-0.
:
Alisema wachezaji hao walimkuna katika mchezo huo kwani walipiga mpira mwingi na atapeleka majina yao kwa uongozi.
:
🗣️“Ni wachezaji wazuri hawa watanisaidia sana lakini niwapongeze Milambo wana vijana wenye vipaji sana kama wakiwaendeleza watakuwa nyota wazuri sana,” alisema Mayanga.
:
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Yikpe Ghislain amefuzu vipimo vya afya

Mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Yikpe Ghislain amefuzu vipimo vya afya na yupo njiani kuelekea Mbeya kujiunga na kikosi cha Yanga japo hakuna taarifa kama amesaini mkataba na klabu hiyo. .

Wachezaji wengine ambao wapo njiani pia kuelekea Mbeya ni Ditram Nchimbi,
Ali Ali,
Abdulaziz Makame,
Mohamed Issa,
Feisal Salum,
.

#wapendasokaupdates

GSM imeweka mezani kitita cha Tsh Milioni 10 kwa wachezaji wa Yanga wakipata ushindi dhidi ya Mbeya City leo

Uongozi wa klabu ya Yanga umesema kampuni ya GSM imeweka mezani kitita cha Tsh Milioni 10 kwa wachezaji wa Yanga wakipata ushindi dhidi ya Mbeya City leo “Mdhamini wetu ambaye ni Msambazaji wa jezi zetu kupitia Brand Chapa GSM leo jumanne kuelekea mchezo wetu dhidi ya Mbeya City utakaopigwa saa kumi jioni ndani ya Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya ameweka mezani tena ahadi ya pesa taslimu shilingi milioni kumi {10,000,000} kwa ajili ya hamasa ya kupata pointi tatu muhimu”

#SokaplaceUPDATES

Design a site like this with WordPress.com
Get started