Nchimbi Ruksa Yanga | .

#VPLUpdates | Nchimbi Ruksa Yanga | .
:
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Ditram Nchimbi ambaye leseni yake kuichezea Yanga ilizuiwa tayari amepata leseni hiyo saa chache zilizopita na atakuwa miongoni mwa wachezaji wa Yanga kwenye mchezo wa Jumamosi dhidi ya Simba.
:
Ikumbukwe kuwa Klabu ya Polisi Tanzania kupitia kwa kaimu katibu mkuu wao walisema kuwa, wameweka pingamizi TFF kuhusu mshambuliaji huyo kusajiliwa na Yanga msimu huu wa dirisha dogo kwa kuwa walimpa fedha anazotakiwa kuzirejesha ili zitumike kusajili mchezaji mwingine. Hivyo kwa sasa Mambo yote yamekwisha na NCHIMBI Ruksa Yanga.
:
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limeshindwa kutoa leseni ya mshambuliaji mpya wa Klabu ya Yanga Ditram Nchimbi

Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limeshindwa kutoa leseni ya
mshambuliaji mpya wa Klabu ya Yanga Ditram Nchimbi
kutokana na klabu ya Polisi Tanzania kumuwekea pingamizi
kwa madai ya kuwa na makubaliano naye. TFF tayari imetoa
leseni za wachezaji wawili tu wa Klabu ya Yanga (Adeyum
Ahmed na Tariq Seif Kiakala). Pia TFF imesema itatoa leseni
ya Ditram Nchimbi mpaka pale makubaliano yatakapofikia kati
ya Klabu ya Polisi Tanzania, Klabu ya Azam FC na Nchimbi
mwenyewe.

Simba Sc Vs Ndanda FC | 🏟️ Uwanja wa Taifa | ⏰ 10:00 Jioni | 🏆 ligi kuu Tanzania bara

#VPLUpdates | Simba Sc Vs Ndanda FC | 🏟️ Uwanja wa Taifa | ⏰ 10:00 Jioni | 🏆 ligi kuu Tanzania bara | .
:
Nondo Ni 1 🔨 Tu.
Tangu 2014, Simba Na Ndanda zimekutana x10 na mara zote hizo Ndanda ameambulia vipigo vya aina tofauti tofauti, isipokuwa Septemba 15, 2018 mchezo ulimalizika kwa sare ya 0-0.
:
#NjooKwetu #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Kiungo wa Barcelona, Arturo Vidal, Ameishtaki klabu ya Barcelona

#Arturoupdates | Kiungo wa Barcelona, Arturo Vidal, Ameishtaki klabu ya Barcelona kwa kuwa anaidai kiasi cha pauni milioni 2 (Sh bilioni 6) za bonasi mbalimbali.
:
Wanasheria wake wanadai kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 32, alitakiwa kupewa bonasi mbalimbali baada tu ya msimu wake wa kwanza kusajiliwa Barcelona akitokea Bayern Munich.
:
Vidal aliichezea Barcelona mechi 53 msimu uliopita waliposhinda ubingwa wa La Liga na kuifikisha nusu fainali ya ligi ya mabingwa ulaya. Wanasheria wa Vidal wanasema anatakiwa alipwe bonasi ya pauni milioni 2 kwa kucheza asilimia 60 ya mechi hizo za Barca.
:
Barcelona wao wanapingwa vikali madai hayo kwa hoja ya kwamba Arturo hakufikisha angalau dakika 45 kwa mechi. Huku wakisema wanasheria wake wametafsiri vibaya vipengele katika mkataba wake. Vidal anaamini alikuwa anadai pauni 3,500,637 lakini alipewa pauni 1,446,388 tu.
:
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Takwimu za ADEYUM Vs Biashara

Takwimu za ADEYUM Vs Biashara

KIPINDI CHA KWANZA

Pasi alizopiga kwenda mbele : 8
Pasi alizopiga kurudi nyuma (Backpass) : 3
Pasi alizopoteza : 3
Pasi aliyopita akiwa kwenye nusu ya Biashara (zilizofika) : 1
Pasi aliyopiga akiwa kwenye nusu ya Yanga (Zilizofika) : 11
Krosi: 0
Block : 1
Faulo alizocheza : 1
Faulo alizochezewa : 1
Mipira ya Juu aliyocheza : 4
Shot on Target : 0
Shot off Target : 1

KIPINDI CHA PILI

Pasi alizopiga kwenda mbele : 5
Pasi alizopiga kurudi nyuma (Backpass) : 3
Pasi zilizopotea: 4
Pasi aliyopiga kwenye nusu ya Biashara : 0
Pasi alizopiga kwenye nusu ya eneo la Yanga (Zilizofika) : 5
Krosi : 0
Block: 1
Faulo alizocheza : 0
Faulo alizochezewa : 0
Mipira ya juu aliyocheza : 3
Shot on Target : 0
Shot of Target : 0

Hii ina maana gani kwa Adeyum?
Kwa jicho la kawaida, kwa kutazama ‘style of play’ ya mahitaji ya mfumo wa 4-3-3 aliotumia Mkwasa, hapa unaweza kuona Adeyum alifeli. Alikua chini mno, hakuonekana kabisa akipanisha timu mbele, kuattack space za pembeni na kupiga krosi.

Lakini kwa kutazama jinsi Yanga walivyokua wanacheza, ni ngumu sana kumlaumu Adeyum. Kwanini?

Ili beki wa pembeni upande na uweze kushambulia ni lazima uwe na uhakika na vitu vitatu
.
.
Kwanza timu yako iwe inamiliki mpira sana kwenye nusu ya wapinzani, uwe na winga atakakutengeneza nafasi/ njia za kupita na tatu, uwe na uhakika ni nani anabaki kuziba nafasi yako.

Kwa Yanga leo, asilimia 65 ya umiliki wa mpira waliufanya wakiwa kwenye zone yao. Makame na Fei walikua eneo moja, walipiga pasi nyingi fupi na back pass.. Hali hii ilimfanya Adeyum na Mustafa kugusa mpira mara nyingi wakiwa nyuma
.
.
Pili, Sibomana aliathirika na mfumo wa leo. Alicheza kwenye mstari wa kati, Ngassa hakua na speed yake tuliyoizoea. Hakutengeneza njia nyingi upande wa kushoto, ilikua ngumu sana kwa Adeyum kusogea juu.

Tatu, ni nani wakumzibia nafasi. Makame ndie holding pekee aliyekua eneo la nyuma. Kasi yake sio nzuri, mtu mwingine wa kumtegemea alikua Sonso, kasi yake haikua nzuri pia. Ni ngumu kwa Adeyum kutake risk kupanda mbele
.
.
Kitakwimu alikua hovyo, lakini kimchezo, alibaki kufanya jukumu lake la msingi, KUKABA TU
.
.
© Imeandaliwa na Allykamwe

TFF yawaita Azam na Yanga …kuhusu sakata la ditrum nchimbi

#VPLUpdates | SHIRIKISHO la mpira wa miguu nchini ‘TFF’, limewaita mezani viongozi wa Polisi Tanzania na Azam FC kujadili sakata la uhamisho wa straika Ditram Nchimbi, aliyejiunga na Klabu ya Yanga

Inaelezwa Polisi walimchukua Nchimbi kwa mkopo wa mwaka mmoja kutoka Azam.

Lakini kwenye makubaliano ya mkopo huo ni kumpa mchezaji signing fee kwa mkataba wa kubaki kwao mpaka msimu utakapomalizika, huku wakimlipa mshahara kwa kipindi chote hiko.

Mkataba huo kati yao na Nchimbi, Polisi wanadai unatambulika na viongozi wa Azam na waliuwasilisha TFF, mwanzoni mwa msimu ukapokelewa

Hoja ya Polisi ni kutaka kulipwa gharama zao (Ambazo wamegoma kuiweka hadharani) ili waweze kuondoka pingamizi lao.

Taarifa zaidi zinadai kua Uongozi wa Yanga ulikua tayari kulimaliza sakata hilo kwa kuwapa Polisi kwa mkopo kiungo Raphael Daud

Lakini Polisi walikataa ombi hilo kwa madai kua wana wachezaji wengi eneo la kiungo hivyo hawana shida na Loth, wanachotaka wao ni Azam na Nchimbi wakae mezani ili walipe gharama zao

| IMEFAHAMIKA kua straika mpya wa Yanga, Tariq Seif alipewa kiasi cha Tsh 65,000 na mashabiki

#VPLUpdates | IMEFAHAMIKA kua straika mpya wa Yanga, Tariq Seif alipewa kiasi cha Tsh 65,000 na mashabiki wa timu hiyo, kama pongezi ya kufunga bao pekee lililowapa ushindi dhidi ya Biashara

Hata hivyo, Tariq alichukua kiasi hiko na kumpa nahodha wa Yanga, Papy Tshishimbi ili aigawe kwa wachezaji wote

Kitendo hiko kilimshtua nahodha msaidizi wa Yanga, Juma Abdul na kumpongeza kijana huyo kwa maana ya kuthamini mchango wa wenzake katika mafanikio yake

Simba Vs Ndanda

#VplPreview | Simba Vs Ndanda

Kwenye mechi 13 walizocheza msimu huu, Ndanda ameshinda mechi 1, sare 5 na vichapo 7.
Ni siku 58 zimepita tangu walipopata ushindi wao pekee mpaka sasa, mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting

Mechi zao 5 za mwisho, wamefungwa 4, wamepata sare 1 (Ugenini Vs Kagera Sugar 0-0)

Ndanda ni timu iliyosheheni wachezaji wazoefu wa Ligi, lakini hawana muunganiko mzuri kama timu. Kukosa kocha wa uhakika imeendelea kua changamoto kubwa kwao.

Leo wanacheza na @simbasctanzania .. Kocha wa Lipuli aliwaita ‘Mnyama’.. Pamoja na heshima hiyo, mwisho wa dakika 90, akachezea 4-0🙌😀
.
.
Simba ndio vinara wa Ligi, mechi zao 5 za mwisho, wamepata sare 1 tu, wameua 4
.
.
Katika ushindi huo wa mechi 4, wamefunga mabao 13. Idadi ya mabao ambayo Ndanda amefungwa mpaka sasa msimu huu, kwenye mechi zake 13🤔

Simba ni imara sana katikati ya kiwanja. Wana utajiri wa viungo wanaompa jeuri kocha kufanya rotation
.
.
Simba imekua ikipata mabao yake katika maeneo matatu, mastraika, viungo na mawinga.. Inahitaji timu imara sana kuwalinda kwa dakika 90

Utabiri …….❓

Design a site like this with WordPress.com
Get started