Kipa wa kimataifa wa Kenya Ian Otieno yupo mbioni kujiunga na Zanaco ya Zambia akitokea Red Arrows.

Kipa wa kimataifa wa Kenya Ian Otieno yupo mbioni kujiunga na Zanaco ya Zambia akitokea Red Arrows.


Otieno, ambaye alijiunga na Red Arrows mnamo februari 2018 kutoka AFC Leopards, amejipatia jina katika Ligi Kuu ya Zambia (ZSL) katika misimu miwili iliyopita.


Umahili wake umekuwa akimpa imani Kocha Mkuu wa Harambee Stars, Francis Kimanzi ambaye amemfanya kuwa na namba ya kudumu mbele ya Patrick Matasi na Timothy Odhiambo.

..
“Tumekubaliana kwa mahitaji binafsi na sasa ni kwa vilabu hivyo viwili kukubaliana juu ya ada ya uhamisho,” Otieno aliiambia Nation Sport kwa simu kutoka Zambia .

Hatimae siku husika imefika

Hatimae siku husika imefika.

Mashindano ya Mapinduzi Cup yatamalizika Leo kwa mwaka huu 2020 kwa fainali Kali ya Simba Sc vs Mtibwa Sugar.

Toka kuanzishwa ma mashindano haya, Simba na Mtibwa katika hatua ya Fainali wamekutana mara mbili lakini kwa bahati mbaya Mtibwa hakubahatika kubeba kombe mbele ya wekundu hao.

2008 Simba sc 1-0 Mtibwa Sugar

2015 Mtibwa Sugar 0-0 Simba Sc ( Simba Sc 4-3 Mtibwa Sugar.

2020 Mtibwa Sugar vs Simba Sc je’ ninani atatwaa taji hilo??. #fullsokatzupdates

Siku ya Tarehe 11/1/2020 klabu ya Mbeya City ilicheza mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Ndanda Fc.

Siku ya Tarehe 11/1/2020 klabu ya Mbeya City ilicheza mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Ndanda Fc.

Mchezo huo ulimalizika kwa Mbeya City kushinda bao 1-0, bao hilo likifungwa na Kelvin John.

Jina la mchezaji huyo lilileta sitofaham na watu wengi wakajua ni kinda @kelvin.p.john .

Pichani 📸 ni picha ya mchezaji Huyo, kwamana hiyo ambao mlikuwa na maswali mpaka sasa ni majina tuu yamefanana lakini Kelvin John wa Mbeya city ni huyu hapa 📸. #fullsokatzupdates

Muargentina kuchukua nafasi ya Valverde huko Camp Nou …


Barcelona inaonekana imedhamiria kutafuta kocha atakayechukua mikoba ya Ernsto Valverde kupitia kituo cha redio cha Uhispania RAC1 sasa wanasema watamwangalia Mauricio Pochettino kuchukua jukumu hilo.


Chaguo la kwanza klabu la Barca lilikuwa kwa mchezaji wao wa zamani Xavi, lakini aliwakatalia jana Jumapili na akachagua kubaki Qatar na Al Sadd.


Pochettino ambaye hana kazi baada ya kuachana na Tottenham amekuwa akihusishwa na vilabu mbalimbali ulaya
Je anaweza kuwa chaguo sahihi kwa Barca

Design a site like this with WordPress.com
Get started