Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu Simba Mo Dewji atengua.kauli

Muwekezaji na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu Simba Mo Dewji, amesema kuwa kilichotokea kwenye akaunti zake jana usiku baada ya mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi kati ya Simba na Mtibwa Sugar ni bahati mbaya.

Mo amesema hayo leo kupitia ukurasa wake wa Twitter ikiwa ni saa 13 tangu alipotangaza kujuzulu nafasi ya uenyekiti na kwamba angebaki kama muwekezaji na kuangazia zaidi katika maendeleo ya miundombinu na soka la vijana.

Usiku wa kuamkia Januari 14 Mo Dewji alitangaza kujiuzulu kutokana na Simba kushindwa kutwaa kombe la Mapinduzi baada ya kufungwa goli moja na Mtwibwa katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar.

Baaada ya kutoa kauli hiyo mashabiki wa Simba walimtaka muwekezaji huo kutafakari upya uamuzi wake kwa madai kuwa tatizo huwa halikimbiwi bali linakabiliwa.

#tbconline

KLABU ya Ligi Kuu ya Kenya (KPL) Bandari imemtimua rasmi Bernard

KLABU ya Ligi Kuu ya Kenya (KPL) Bandari imemtimua rasmi Bernard Mwalala na nafasi yake kuchuliwa na Twahir Muhiddin.


Mwenyekiti wa Klabu Musa Hassan amethibitisha kupitia taarifa iliyotolewa na klabu hiyo ya Mombasa.

… “Bodi ya wadhamini ya Bandari FC imemtaka kocha mkuu Bernard Mwalala kuhama kando kutokana na utendaji duni wa kilabu hivi karibuni,” alisema Hassan katika taarifa hiyo.
..
..
Mwalala amekuwa na Bandari tangu mwaka 2018 wakati alijiunganayo akitokea Nzoia Sugar na kuisaidia klabu hiyo kushinda Kombe la Shirikisho la Soka Kenya na kukata tiketi ya moja kwa moja kwenye Kombe la Shirikisho la CAF.

Tariq Seif Kihakala tayari ameanza mazoezi na wenzake

Imeripotiwa kuwa Mchezaji mpya wa Yamba sc Tariq Seif Kihakala tayari ameanza mazoezi na wenzake baada ya kukaa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa kutokana na majeraha aliyo yapata kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Biashara Utd.

Kihakala amejiunga na Yanga sc katika dirisha dogo la usajili la msimu huu.

#fullsokatzupdates

Antonio Conte ameshinda kesi dhidi ya klabu hiyo, ingawa amelipwa zaidi ya pauni 85,000 kama fidia.(Mirror) :

#TetesiZaSokaBaraniUlaya
:
✍️ Kocha wa zamani wa Chelsea Antonio Conte ameshinda kesi dhidi ya klabu hiyo, ingawa amelipwa zaidi ya pauni 85,000 kama fidia.(Mirror)
:
✍️ Kocha wa Tottenham Jose Mourinho anahofu kuwa mshambuliaji wa kikosi hicho Harry Kane, 26 atakuwa nje ya uwanja mpaka msimu ujao na atakosa michuano ya Euro 2020 kutokana na jeraha. (Sun)
:

✍️ Mourinho anahitaji washambuliaji wawili Januari hii kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Kane. Mshambuliaji wa AC Milan Krzysztof Piatek, 24, ni mmoja kati ya wachezaji wanaotupiwa macho sambamba na mshambuliaji wa Napoli Fernando Llorente 34 na mshambuliaji wa Crystal Palace Christian Benteke, 29. (Independent)
:
✍️ Mshambuliaji Thomas Mular ataondoka Bayern Munich baada ya miaka 20 kuwa na klabu hiyo. (Sport 1, via Sun)

:
✍️ Atletico Madrid imeamua mshambuliaji wa Arsenal na Ufaransa Alexandre Lacazette, 28 kuwa kipaumbele chao ikiwa watashindwa kumsajili Edinson Cavani, 32, mshambuliaji wa Paris St-Germain na timu ya taifa ya Uruguay.(Express)
:
✍️ Mshambuliaji wa Southampton Danny Ings,27, anastahili nafasi kwenye kikosi cha Gareth Southgate, amesema kocha wa Leicester Brendan Rodgers, ambaye alimsajili kujiunga na Liverpool.(Sky Sports)

:
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Design a site like this with WordPress.com
Get started