
Uongozi wa klabu ya Yanga umeilalamikia Bodi ya ligi (TPLB) kwa kubadilisha tena sehemu ya mchezo wao dhidi ya Singida United kutoka Arusha kurudi Singida muda mfupi huku wao wakiwa wameshafanya maandalizi ya awali.
Siku chache zilizopita Bodi hiyo ilitangaza kuwa mchezo huo utaenda kupigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kwakua uwanja wa Liti (zamani Namfua) unahitaji marekebisho lakini leo kumetoka taarifa nyingine kuwa mchezo huo utapigwa mkoani Singida.
Katibu Mkuu wa Yanga, Dk. David Luhago amesema tayari wameshafanya maandalizi ya usafiri kwa kuweka booking kwenye ndege na kulipa sehemu ya pesa (advance) kwenye hoteli watakayo fikia hivyo hawaelewi jinsi ya kurudisha gharama zao baada ya mabadiliko hayo.
Dk. Luhago amesema kwa kawaida kama kuna mabadiliko ya ratiba ya mchezo taarifa inapaswa kutolewa saa 48 kabla lakini Bodi haikufanya hivyo na kuwashtukiza kuwaambia mchezo huo utapigwa mkoani Singida nasi Arusha tena. “Bodi ya ligi ilituandikia barua kuwa mchezo wetu wa Jumanne dhidi ya Singida utapigwa uwanja Sheikh Amri Abeid Arusha lakini wamebadili tena kuwa tutaenda Singida wakati sisi tushalipa gharama za awali. Taarifa ilipaswa kutolewa mapema, sisi tumejiandaa kuwa tunasafiri kwenda Arusha,” alisema Dk. Luhago.
#wapendasokaupdates