DIDA AANGUKIA LIPULI FC YA IRINGA

:
Golikipa wa zamani wa vilabu vya Simba na Yanga Deogratius Munish ‘Dida’ ni miongoni mwa wachezaji wapya tisa waliojiunga na Lipuli FC katika kipindi kifupi cha usajili (dirisha dogo) kilichofungwa Januari 15, 2020.
:
Dida ambaye msimu uliopita alikuwa akiwatumikia mabingwa Tanzania Bara Simba SC kabla ya kutemwa mwanzoni mwa msimu huu, alikuwa hana timu yoyote, hivyo Lipuli imemsajili kama mchezaji huru lengo likiwa kuimarisha eneo hilo la ulinzi wa lango lao.
:
Wengine waliosajili Lipuli ni pamoja na:
:
Isihaka Luhago – Azam FC.
David Mwantika – Azam FC.
Ally Myovela – Tanzania Prisons.
Peter Mwangosi – Alliance FC (mkopo).
Paul Ngalema – Namungo FC (Mkopo).
Said Musa – Yanga SC (Mkopo).
Joseph Mtamaki – Mchezaji huru.
Shaaban Adda – Mchezaji huru.
:
Lipuli FC pia imetema wanne katika kipindi hicho ambao ni Rajabu Mpululo, Dereck Karulika, Waziri Tajir na Shaban Kimaro.

Via @azamsports2

MJUE HASSAN SALEHE DILUNGA mpaka “HD”

.
Inaandikwa na @danirito_thomson
.
Kwanza kabisa HAPPY BIRTHDAY midfielder kisheti, ishi tu, endelea kuwafurahisha WAKALI WA TERMINAL jukwaani
.
Hasan Dilunga akili na mwili na style kama mJapan Shinji Kagawa, anafit kama namba nane wa kulia au kushoto kwenye 4-3-3 anafit kama 10, 7,11 kwenye 4-2-3-1
.
Kiungo mshambuliaji anaeweza pia kucheza winga ya kisasa sahau wale mawinga mbio mwisho mita 100 kwenye kibendera, NO thank you
.
Alianza kuonekana kwa waTanzania akiwa kijana mdogo miaka ya 2013, alikua na mwili usiotisha ila football brain na miguu yenye kipaji
.
Alikuwa pale kwa Masau Bwire msemaji mwenye simu zake, Mpapaso-CEO, kipindi kile wakiitwa Ruvu Shooting
.
Yanga ya kocha Ernest Brandts walimsajili Dilunga kutoka Ruvu Shooting, wengi waliangalia ule mwili wake wakasahau football is upstairs kwenye ubongo
.
Alianza slow kidogo ila mwendo ukachanganya
.
Akaja Hans Van Pluijm na ile Yanga yenye Nizar Khalfan, Niyonzima msimu wa 2015, kuna kipindi alipokezana na Niyonzima ila bado pale jangwani hawakupiga stori zake wakikutana vijiweni
.
Mnaikumbuka ile Stand United chini ya matajiri wa migodi ACCACIA? ile iliyobadili jezi ya orange ya chama la wana mpaka Blue na kuwachefua wapiga debe wa stand mitaa ya Ngokolo na Ndala pale ardhi yenye madini yake Shinyanga, basi ile Stand ilimchukua Dilunga kwa mkopo kutoka Yanga 2015
.
Stand iliyokuwa na Kiemba ya kocha mfaransa Patrick Liewig, pale Dilunga gari lilipungua kasi injini ilichoka kidogo kiwango kilikula pause
.
Akasajiliwa tena kule JKT Ruvu, kisha Ajax ya Bongo Mtibwa chini ya mwalimu Katwila gari likawaka kiwango kikarejea, Simba akamuona na kumsajili kile kipindi wakitafuta nani mbadala wa Niyonzima ambae alisajiriwa ila alionekana majeruhi spana mkononi
.
Dilunga wa Simba hapo sasa ndipo akawa HD tunaemjua, makocha wote pale msimbazi wamemtumia huyu Kagawa
.
Ila naona Sven Van de Broeck anamuhusudu sana bwana HD, ile kasi yake na akili kumkichwa kwenye ule mfumo wa 4-2-3-1
.
HD anampa Sven faida katika mafungu matatu, winga na ile kasi, kiungo na ule ubongo na mshambuliaji na lile jicho
.
Nimeona niandike hii kabla TCRA kwa ushirikiano na NIDA hawafunga line yangu
.
💪

Kamata Ratiba Ya Soka Leo

:
👉England – Premier League
22:30 Aston Villa vs Watford
22:30 AFC Bournemouth vs Brighton & Hove Albion
22:30 Everton vs Newcastle United
22:30 Sheffield United vs Manchester City
22:30 Crystal Palace vs Southampton
23:15 Chelsea vs Arsenal
:
👉England – Championship
22:45 Barnsley vs Preston North End
22:45 Middlesbrough vs Birmingham City
:
👉Italy – Coppa Italia
22:45 SSC Napoli vs Lazio
:
👉Netherlands – KNVB Cup
20:30 TOP Oss vs AZ Alkmaar
22:45 FC Eindhoven vs FC Utrecht
22:45 Fortuna Sittard vs Feyenoord
:
👉Spain – Copa del Rey
23:00 Real Zaragoza vs Mallorca
23:00 Recreativo Huelva vs Osasuna
:
👉International – Club Friendlies
15:00 AGF vs AaB
17:00 Al-Uwaynah vs Zenit St. Petersburg
17:00 Basel vs Grasshopper
18:00 Lyngby vs Hvidovre
19:00 AC Horsens vs Aarhus Fremad
:
👉Egypt – Premier League
17:30 Tanta vs El Gounah
17:30 Pyramids FC vs Misr El-Maqasa
:
👉France – League Cup
23:10 Lyon vs Lille
:
👉Morocco – Botola Pro
21:00 Hassania Agadir vs Difaa El Jadida
:
Prepared by @officialchristz
#SokaplaceUPDATES
@danirito_thomson

Kamata Matokeo Ya Soka Jana

:

👉England – Championship
FT West Bromwich Albion 0 – 1 Stoke City
:
👉Italy – Serie A
FT Atalanta 1 – 2 SPAL
:
👉France – Cup
FT St-Pryve St-Hilaire 1 – 3 Monaco
:
👉International – Friendlies
FT Seychelles 2 – 2 Mauritius
:
👉International – Club Friendlies
FT Sevilla 1 – 3 SV Sandhausen
FT Dinamo Moscow 5 – 1 Zaglebie Lubin
FT FK Akhmat 1 – 3 Botosani
FT FC FCSB 3 – 3 Lokomotiv Moscow
:
👉Algeria – Ligue 1
FT JS Kabylie 1 – 0 MC Oran
FT ASO Chlef 0 – 0 USM Alger
:
👉Egypt – Premier League
FT Aswan FC 1 – 3 Wadi Degla FC
FT El Geish 0 – 3 Al-Ittihad Al-Sakandary
:
👉Morocco – Botola Pro
FT Olympic Club de Safi 1 – 2 Wydad Casablanca
:
👉Ghana – Premier League
FT Bechem United 1 – 0 Eleven Wonders FC
:
Prepared by @officialchristz
#SokaplaceUPDATES
@danirito_thomson

Inter Milan pia ina hamu ya kumsaini kiungo wa kati wa Croatia Luca Modric

Inter Milan pia ina hamu ya kumsaini kiungo wa kati wa Croatia Luca Modric , 34, kutoka Real Madrid(Sport – in Spanish) Atletico Madrid imeipatia Paris St-Germain Yuro milioni 10 (£8.5m) ili kumnunua mshambuliaji wa Uruguay Edinson Cavani, 32. (L’Equipe – in French)

Design a site like this with WordPress.com
Get started