Inter Milan wamefungua mazungomzo ya kumsaini mshambuliaji wa Manchester United

Inter Milan wamefungua mazungomzo ya kumsaini mshambuliaji wa Manchester United Tahith Chong, (Sky Italia)


Inter ulikutana na wakala wa mchezaji huyo wa umri wa miaka 20 Jumanne ili kufungua mpango wa usajiri wa nyota huyo wa taifa la Uholanzi.


Mkataba wa Chong na United unamalizika mwishoni mwa msimu huu na Inter ina matumaini kuwa inaweza kumsaini mchezaji huyo kwa uhamisho wa bure.

Makundi kufuzu World 2022, Qatar, TANZANIA tumepangwa KUNDI J

Makundi kufuzu World 2022, Qatar, TANZANIA tumepangwa KUNDI J
.

Kila kundi inafuzu timu 1. Kimahesabu zitabaki timu 10. Wanakwenda kwenye raundi nyingine ya mtoano.. Mechi 2 tu (Nyumbani na Ugenini) kisha unakata tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia Qatar
.
.

Tukikaza, si tunatoboa hapa ndugu zangu!

Liverpool kutwaa ligi kuu Uingereza msimu

#Sababu 1 Liverpool kutwaa ligi kuu Uingereza msimu huu.
.
โœ๏ธ Kinachoendelea kunako ligi kuu Uingereza kwasasa kila mtu aanakiona, Mabingwa wa Uefa Champions league na klabu Bingwa Dunia Liverpool wapo on๐Ÿ”ฅ kweli kweli, hadi hivi sasa klabu ya Liverpool Tayari inaongoza kwa alama 64 ikiwa imeiacha Man City kwa alama 16 huku Liverpool wakiwa na mchezo mmoja mkononi yaani wamecheza michezo 22, na Man City wao wamecheza michezo 23, Je..!! Unaweza kusema kuwa Liverpool msimu huu Ubingwa upo mikononi mwao, Bado mapema kutabiri hivyo lakini kwa mwenendo wao unaweza kusema hivyo.
:
โœ๏ธ Basi hii ndio sababu ambayo inanifanya niamini kwa % 79 kuwa Liverpool msimu huu Anaweza kutwaa UBingwa, sababu ni moja lakini inavipengele ndani yake.
.
1: Timu ya Klopp imeimarika sana. Jurgen Klopp alitua Liverpool 2015 akitoea Borussia Dortmund. Klopp ameifanya Liverpool kuwa imara kila idara pamoja na kuwa hawana Kikosi kipana kivile.
.
โœ“ Utayari Wa Wachezaji.
Unawapo watazama wachezaji wa Liverpool wanacheza kwa spirit ya hali ya juu sana, kuanzia mabeki , viungo hadi Forward zao ni wamoja, Organization imekuwa kubwa sana pindi wanapo kuwa uwanjani.
.
โœ“ Kuchechema kwa CITY.
Vijana wa Pep msimu huu wanachechemea sana, licha ya kuwa sio wakubeza kwani ukiingia kichwa kichwa utapigwa za kutosha pia, hadi hivyi Sasa wameshaachwa alama 16 nyuma na kiporo Cha mechi 1 kwa Liverpool, hii nayo yaweza kuwa sababu mojawapo ya kuifanya Liverpool kutwaa taji hili msimu huu.
.
โœ“ Fitness. Wachezaji wa Liverpool wanaonekana wana energy ya kutosha bado pamoja na kucheza mechi nyingi za klabu Bingwa Dunia, bado wana Energy ya kupambania Ubingwa msimu huu.
.
โœ“ Uchu wa kuukosa Ubingwa kwa kipindi kirefu tangu msimu wa 1989/90 chini ya Kenny Dalgish kunawafanya Liverpool wapambane kulisaka taji hili msimu huu.
.
โœ“ Ubora wa Klopp.
Ki mbinu, amekuwa Bora pia katika kumtengeneza mchezaji na kuwa wakiwango Cha juu, Kloop amekuwa Bora Sana na ndio silaha kubwa Sana ya Liverpool msimu huu.
.
#bakinasisi__
#NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Lipuli FC..yamshitaki kocha wa KMC TFF

#LipuliNews | Uongozi wa Klabu ya Lipuli FC ya Mkoani Iringa imemuandikia barua na kumshtaki katika shirikisho la mpira wa miguu TFF aliyekuwa kocha wake Haruna Harerimana Raia wa Burundi baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu (miezi 18) na KMC na kuacha kuifundisha timu hiyo kinyume na mkataba waliojiwekea. .
.
Kupitia kwa kaimu mwenyeki wa timu ya Lipuli, Ayubu Kihwelo amesema
.
๐Ÿ—ฃ๏ธโ€œTumemuandikia barua yeye lakini pia na TFF kwa ajili ya kumfungulia mashtaka kwa sababu ameenda kusaini sehemu nyingine akiwa na mkataba halali na Lipuli na mkataba huu ulikuwa unaisha mwezi wa saba ambao ulikuwa wa mwaka mmojaโ€ alisema Kihwelo. .
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Unamkumbuka Chicharito, yule wadakika za mwisho chini ya Sir Alex Ferguson, ndio yeye bwana. .

#LaGalaxyTransferNews | Unamkumbuka Chicharito, yule wadakika za mwisho chini ya Sir Alex Ferguson, ndio yeye bwana.
.
#DealDone | amejiunga na klabu ya La Galaxy ya marekani kwa kandarasi ya miaka 3 akitokew Sevilla kwa kitita cha Dola Million 10 ($10M).
.

#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Kelvin John โ€˜Mbappeโ€™, anajiunga rasmi na klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji

MSHAMBULIAJI chipukizi wa Tanzania, Kelvin John โ€˜Mbappeโ€™, anajiunga rasmi na klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji ambayo nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mbwana Ally Samatta, alikuwa akiichezea kabla ya kujiunga na Aston Villa inayoshiriki Ligi Kuu ya Uingereza.
Kelvin ambaye pia anaichezea timu ya vijana chini ya miaka 20 ya Ngorongoro Heroes ya Tanzania, amekamilisha dili hilo la kujiunga na Genk.

Meneja wa mchezaji huyo Mbaki Mutahaba amesema, uongozi wa Genk umevutiwa na uwezo wa kijana huyo na kila kitu kimekamilika na kinachosubiriwa sasa ni umri tu.
Mchezaji huyo atafikisha miaka 18 baadaye mwaka huu na kwa sasa anaendelea na masomo katika chuo cha Brooke House nchini Uingereza.

Guardiola atoa pole. “Pole kwa Kane Na Rashford” .

Pole kwa Kane Na Rashford” .
:
Kocha mkuu wa klabu ya Man City Pep Guardiola amefunguka na kusema kuwa ligi kuu Uingereza itegemee ongezeko la kubwa la idadi ya majeruhi kipindi hiki, msikie yeye Pep anasemaje..๐Ÿ‘‡
:
๐Ÿ—ฃ๏ธโ€œPole kwa Kane na Rashford. Ni pigo kubwa na hii inatokana na mfumo wa ligi ulivyo, lakini tumekuwa tukilalamika bila mafanikio, tutegemee idadi kubwa ya wachezaji kupata maumivu,โ€ alisema Guardiola.
:
Kocha huyo alisema wachezaji England wanacheza mechi nyingi kulinganisha na Ujerumani au Hispania. Guardiola alisema idadi kubwa ya mechi zinachezwa katika kipindi cha majira ya baridi.
:
Pep amesema haya mara baada ya kushuhudia washambuliaji tegemeo Kane wa Tottenham Hotspurs ambaye atakuwa nje ya uwanja wiki 12 , Rashford wa Man UTD atakosa mechi za Manchester United miezi mitatu.
.
#bakinasisi__
#NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Design a site like this with WordPress.com
Get started