YANGA YAVUNJA MWIKO NAMFUA

Yanga imepata ushindi wa kwanza katika uwanja wa Liti (zamani Namfua) baada ya kuifunga Singida United mabao 3-1 katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom uliomalizika muda mfupi uliopita.

Tangu Singida ilipopanda daraja misimu mitatu iliyopita Yanga haikuwa imepata ushindi katika uwanja huo ikiambulia sare au kipigo.

Katika mchezo huo ambao Yanga ilitawala sehemu kubwa bao la kwanza lilifungwa dakika ya 12 na mshambuliaji David Molinga baada ya kuwazidi ujanja walinzi wa Singida.

Kipindi cha pili Yanga iliongeza mengine mawili dakika ya 59 na 74 yaliyofungwa na Haruna Niyonzima na Yikpe Gislain wakati Six Mwakasega akiifungia Singida bao la kufutia machozi dakika ya 84.

Winga mpya Bernado Morrison ambaye alicheza kwa mara ya kwanza ameonyesha uwezo mkubwa huku ikionekana kama unaweza ukawa usajili mzuri kwa Yanga.

#wapendasokaupdates

Maneno ya niyonzima baada ya mchezo wa jana

Watu wakumbuke kuwa pamoja na kwamba mimi nilicheza Yanga, lakini hii ni Yanga mpya, ni timu ambayo inajengwa.

Sisi kama timu tuna malengo yetu na kama tutaendelea kuwa pamoja kama wachezaji, viongozi, mashabiki na wadhamini wetu basi tutakua na timu nzuri sana kwa siku zijazo.

HARUNA NIYONZIMA

#wapendasokaupdates

Kamata Ratiba Ya Soka Leo

:
👉England – Premier League
23:00 Wolverhampton Wanderers vs Liverpool
:
👉England – FA Cup
22:45 Tranmere Rovers vs Watford
:
👉Spain – Copa del Rey
21:00 Ebro vs Leganes
21:00 Mirandes vs Celta Vigo
23:00 CD Badajoz vs Eibar
23:00 Leonesa vs Atletico Madrid
23:00 Rayo Vallecano vs Real Betis
:
👉Belgium – Beker Van Belgie
22:45 Royal Antwerp vs Kortrijk
:
👉Algeria – Ligue 1
19:00 Paradou AC vs CS Constantine
:
👉Morocco – Botola Pro
21:00 Ittihad Tanger vs Olympic Club de Safi
:
Prepared by @officialchristz
#SokaplaceUPDATES
@danirito_thomson

Wachezaji yanga wafunguwa michezo mi tatu(3)

Mechi namba 17

Mbeya City vs Yanga

Wachezaji wa Mbeya City
Kelvin na Majaliwa Shaban,wachezaji wa Yanga Ngassa,Kabwili na Cleophas Sospeter kila mmoja amefungiwa michezo mi 3 na faini ya sh laki 5 kila mmoja kwa kosa la kugoma kuingia vyumbani Suala la waamuzi limepelekwa kwenye kamati maalum kwa uchunguzi

Mechi namba 22
Yanga vs Prison

Timu zote zimepigwa faini laki 5 kwa kutowasilisha kikosi kwenye pre match meeting

Kanuni namba 14-3 Taratibu za mchezo

Mechi namba 89

Azam vs Yanga

Kocha wa Yanga amepewa onyo kali kwa kosa la kutoa matamshi yasiyofaa
Yanga wametakiwa kutoa tamko kwa sababu ni kitu ambacho hakipo katika taifa letu ubaguzi

Mechi namba 130

Simba vs Yanga

Klabu ya Yanga imetozwa faini ya sh laki 5 kwa kosa la washabiki kurusha chupa za maji uwanjani na kuwarushia chupa waamuzi wakati wakielekea vyumbani

Klabu ya Yanga imepigwa faini laki 2 kwa kutotumia chumba rasmi uwanjani.

Matukio mengine yaliyotokea kwenye mechi hiyo yamepelekwa kwenye kamati maalum kwa uchunguzi

Mechi namba 163

Coastal Union vs Biashara

Mjumbe wa kamati ya utendaji wa Coastal union Salum amepelekwa kwenye kamati ya nidhamu kwa kosa la kutaka kuingia uwanjani kwa lengo la kumdhuru mwamuzi huku akitoa maneno makali.

Klabu ya Tanzania Prisons na Yanga Sc zimepigwa Faini ya Tsh.500,000/

Klabu ya Tanzania Prisons na Yanga Sc zimepigwa Faini ya Tsh.500,000/=(Laki Tano) kila mmoja kwa kosa la kutokuwakilisha vikosi vya timu zao kwenye kikao cha maandalizi ya mchezo katika mechi hiyo iliyochezwa Disemba 29,2019 katika Uwanja wa Samora mjini Iringa.

Adhabu dhidi ya Timu hizo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

#wapendasokaupdates

#TetesiZaSokaBaraniUlaya

:

✍️ Liverpool wako tayari kumuuza Xherdan Shaqiri kwa £25m msimu wa joto lakini haitaki kumuachilia winga huyo wa Uswizi wa miaka 28, aondoke kwa mkopo mwezi huu. (Liverpool Echo)
:
✍️ Inter Miami imewasiliana na wawakilishi wa mshambuliaji wa Manchester City na Argentina Sergio Aguero, 31, na David Silva, 34, ambao wataondoka klabu hiyo msimu wa joto. (Sun)
:
✍️ Manchester United huenda ikamsajili kiungo wa kati wa Ureno Bruno Fernandes, 25, kwa mkataba wa £55m mwisho wa wiki hii baada ya kuafikiana na Sporting Lisbon. (Mirror). Fernandes aliwapuuza mashabiki wa Sporting na kusukuma kamera za televisheni baada ya kupoteza mechi dhidi ya Braga siku ya Jumanne katika kile kilionekana kuwa mechi yake ya mwisho katika klabu hiyo. (Star)
:
✍️ Manchester United imetoa ofa ya zaidi ya £30m kumnunua kiungo wa kati wa Birmingham City wa miaka 16 Jude Bellingham. (Sun)
:
✍️ Mkufunzi wa Barcelona Quique Setien anasema kuwa klabu hiyo inamtafuta mchezaji atakayeziba pengo lililoachwa na mshambuliaji wa Uruguay aliyeumia Luis Suarez, 32 mwezi huu. (Sport)
:
✍️ Barca inapania kumsajili mshambuliaji wa Uhispania Rodrigo Moreno lakini Valencia inataka kumnunua kiungo huyo kwa euro milioni 60. (Marca)
:
✍️ Beki wa Real Madrid, Mhispania Alvaro Odriozola, 24, ametua Ujerumani kukamilisha uhamisho wake kwenda Bayern Munich hadi msimu utakapokamilika. (AS – in Spanish)
:
✍️ Barcelona inamtaka Pierre-Emerick Aubameyang lakini kuondoka kwake Arsenal kabla ya mkataba wake kuisha mwaka 2021 huenda kukamgharimu mshambuliaji huyo wa Gabon, 30, £15.15m. (Star)
:
✍️ Bournemouth wanamtaka kumnunua mshambuliaji wa Lyon -anayekadiriwa kuwa na thamani ya £35 Bertrand Traore. (Mail)
:
✍️ Leicester na West Ham pia wanamfuatilia Traore, 24, . (Foot Mercato – in French)
:
✍️ Burnley, Leicester na Sheffield United wanamtaka kiungo wa kati wa Bristol City Josh Brownhill, 24. (Bristol Post)
;
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

#Maoni Ya Wachambuzi Wa Soka kuhusu Arsenal hii Ya Mikel Arteta. :

Rio Ferdinand, Martin Keown na Joe Cole 🗣️ “Arsenal haina beki imara” .
:
Keown 🗣️ “Tunapomzungumzia beki kama Mustafi kabla ya mechi, nilikuwa nina hofu kwa mchezaji huyu kama anaweza kucheza kwa kiwango kinachostahili,”alisema Keown.
:
Keown aliyecheza kwa mafanikio nafasi ya beki wa kati Arsenal, alisema timu hiyo inahitaji beki imara wa kati tofauti na Luiz au Mustafi.
:
Cole 🗣️ “Ukiwa na mabeki kama Luiz au Mustafi huwezi kuwa na uhakika wa kushinda mechi, itachukua muda mrefu kupata matokeo,”alisema Cole.
:
Ferdinand 🗣️”Arteta anafanya makosa kumpa jukumu Mustafi kucheza beki wa kati kwa kuwa hana uwezo.”
.
Nini Maoni Yako______?
:
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

Design a site like this with WordPress.com
Get started