UsikuWaMabingwa | USIKU MWINGINE WA NDONDI | Tarehe 28/3/2020 Uwanja wa Uhuru. :

#

✍️ 1-Hassan Mwakinyo vs Rodolfo Ezequiel.Kg 69 superwelter. Raundi 10 ubingwa wa mabara WBF na UBO.
: .
✍️ 2-Twaha Kiduku VS Tinampay au Narong Bunchan. kg 72 Raundi kumi. Ubingwa wa UBO.
:
✍️ 3-Dula Mbabe vs Bordin Peepueh. kg76 Raundi kumi. Ubingwa WBF.
:
✍️ 4-Salimu Mtango vs Francis miyeyusho.kg 59 Raundi kumi. Ubingwa WBF.
.
NB: Kwa mujibu wa Promoter Ally Mwazoa
.

Pambano lipi tubebe machela 🤔

:
#bakinasisi__ #NjooKwetu #TupoNawePaleUlipo

BRUNO MASHAKANI KUTUA UNITED

Wakala wa Bruno fernandes Jorge Mendes amesema kwamba hakuna uhakika kwamba Bruno Fernandes atajiunga na Manchester United kutoka Sporting Lisbon mwezi huu Januari na kuonya kwamba klabu ya Sporting imefanya mawasiliano na klabu zingine kuhusu uhamisho wa Bruno ndani ya Januari hii au majira ya kiangazi .
…..
. “ Sijui , kama hatoondoka sasa hivi nina uhakika ataondoka Majira ya kiangazi kwasababu Sporting tayari wameshaongea na klabu zingine . Kuna kitu kitatokea lakini sina uhakika kama sasa hivi au mwishoni mwa msimu “
.

‘Haaland anaweza kuhamia Ligi Kuu ya Uingereza siku moja’ … …

Uamuzi wa Erling Haaland kujiunga na Borussia Dortmund haimaanishi kuwa hataenda kucheza Ligi Kuu, ya Uingereza kulingana na wakala wake Mino Raiola.
..
..
Nyota huyo wa Norway alijiunga na Dortmund akitokea RB Salzburg mwezi huu, lakini Raiola anasema kwamba Haaland inajiandaa na kutua sehemu nyingine hapo badae

Tottenham kuleta mbrazili EPL

Tottenham wanamlenga mshambuliaji wa Real Sociedad, Mbrazil Willian Jose na kiungo huyo wa miaka 28-anatarajiwa kusafiri kwenda London kwa ajiri mazungumzo. (AS)
..
..
Klabu sita za ligi ya Uingereza zinataka kumsaini beki wa Tottenham Muingereza Danny Rose, 29, mwezi huu. (Sky Sports)

..
Tottenham wanapanga kutoa ofa ya pili ya kumnunua mshambuliaji wa Fenerbahce na Kosovo Vedat Muriqi. (Aksam, via Sport Witness)

Arsenal wanaripotiwa kuwa wapo tayari kuboresha mshahara kinda Gabriel Martinelli na kumlipa mara tatu zaidi

Arsenal wanaripotiwa kuwa wapo tayari kuboresha mshahara kinda Gabriel Martinelli na kumlipa mara tatu zaidi ya alicholipwa awali kwa nia ya kukwamisha riba kutoka Real Madrid kwa kijana huyo wabrazil.


Martinelli amefunga mabao 10 katika michezo 21 ndani ya Arsenal msimu huu tangu kutua kwake kwa pauni milioni 7 akitokea Ituano nchini Brazil majira ya joto.

..

Kasi nzuri inayoendana na umri wake wa miaka 18, umeonyesha kuwavutia Real Madrid na kutoa ofa ya pauni milioni 50 kwa Martinelli, kwa mujibu wa Daily. Lakini Arsenal hawataki kumuuza Martinelli huku wakiboresha malipo yake ya wiki kutoka pauni 10,000 kwa pauni 30,000.

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Wasichana U17 kimeondola leo kueleka Burundi

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Wasichana U17 kimeondola leo kueleka Burundi kwenye mchezo wa marudiano kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Burundi mchezo utakaochezwa Januari 25,2020 Bujumbura.
@samia_suluhu_hassan @wallacekaria @wilfredkidao @regofficeaa @taifastars_ @twigastarstz @azamtvtz @fifawomensworldcup#wapendasokaupdates

Mambo 10 nilioyaona Singida Vs Yanga

1: Benard Morrison.. What a player🙌 Akiwa hajazoeana vizuri na wenzake, akiwa kwenye kiwanja kibovu na bado aliamua kufanya mapenzi na mpira👏 Ni mtu tishio aliyekosekana kwenye kikosi cha Yanga tangu Simon Msuva.

2: Luc Eymael. Angalau leo presha yake ilikua chini, Yanga ikaonekana inacheza kwa utulivu zaidi. Licha ya changamoto ya kiwanja, bado Yanga ilikua ikifanya build up kutokea chini
.
.
3: Tshishimbi🙌 Siku akiwa kwenye kiwango bora, Yanga inakua bora. Alikua kiongozi kwa mabeki wake na akawa backup kwa viungo wake wa juu.

4: Napenda sana mikimbio ya Balama Mapinduzi kwenye eneo la mwisho. Kasi yake, pasi zake zinawapa kitu cha ziada mastraika wa Yanga.

5: Molinga.. Yes. Ameanza kuimarika. Ari yake kiuchezaji iko juu sana. Ni straika pekee wa Yanga mpaka sasa mwenye uwezo mkubwa wa kunusa hatari kwenye eneo la mwisho

6: Chuji👏 Dakika zake chache uwanjani zilitosha kabisa kutukumbusha Taifa kitu gani tumekimisi kwa viungo wetu wa ‘kisasa’

7: Sumbi🙌 yule namba 27 wa Singida anajua sana. Ni mtulivu mno na pasi zake ni za uhakika. Bahati mbaya kwake, yuko katika kiwango bora akiwa na jezi ya Singida.

8: Navutiwa sana na nidhamu ya Jafar Mohamed kwenye kukaba. Akijiongezea bidii mazoezini, akaboresha kasi yake, anaweza kua mtu sahihi sana kwenye eneo lile

9: Singida imepigwa Mabao 3, lakini ni ngumu sana kuacha kuizungumzia mikono ya Owen Chaima🙌 Alikua kwenye kiwango bora sana aisee.

10: Kama Yikpe huwa anajifanyia tathimini ya uchezaji wake basi bao la leo linaweza kumpa mwanga mzuri. Kwa mwili wake, kimo chake, nguvu anatakiwa awe anazurura sana ndani ya boksi na sio nje.

Nb: Kamati mpya oyee😀

Design a site like this with WordPress.com
Get started