
Achana na alivyoagwa mwaka 2016 wakati akitangaza kustaafu kucheza ligi ya mpira wa kikapu Marekani (NBA) baada ya kucheza misimu 20 mfululizo.
Wakati ule alipoagwa kucheza ligi hiyo alipata nafasi ya kusema neno lililopata umaarufu, *”what can I say?..Mamba Out”* akimaanisha kuwaaga kwenye mchezo huo baada ya kumaliza muda wake wa miaka 20 akicheza ligi hiyo kubwa Duniani.
Asubuhi ya Jumapili kwa muda wa Marekani na usiku kwa Afrika Mashariki,haikuwa kama ilivyokuwa mwaka 2016 kwa Kobe Bryant (Mamba) kuaga kawaida badala yake alifikia mwisho wake wa kuishi Duniani (miaka 41) akiacha majonzi makubwa kwa wapenzi wa mchezo huo na ulimwengu kwa ujumla kufuatia kifo chake kilichotokana na ajali ya ndege yake binafsi.
Taarifa zimeeleza kuwa Kobe alikuwa njiani kuelekea kilipo kituo chake cha kuendeleza michezo kinachoitwa Mamba Sports Academy ambacho hutoa mafunzo na kuandaa wanamichezo shindani.
Ukiachana na salamu mbalimbali za maombolezo kutoka kote ulimwenguni,Kamishna mkuu wa NBA,Adam Silver amemuelezea Kobe kupitia misimu yake 20 aliyocheza ligi hiyo kama kielelezo tosha cha ushindi na hekima kama mfano bora kwa kizazi kijacho cha wachezaji wa mpira huo.
Tofauti na wachezaji wengi,Kobe aliitumikia Los Angeles Lakers tu katika maisha yake yote ya kucheza kikapu akiitumikia miaka 20 mfululizo akishinda mataji matano,akishinda tuzo ya MVP mara moja pamoja na Kuwa MVP bora wa fainali mara mbili.
Kobe ambaye namba za jezi zake zote mbili (8 na 24) zilistaafishwa kuvaliwa na timu hiyo baada ya kustaafu kwake,anashika nafasi ya nne kwa ufungaji wa muda wote kwenye ligi hiyo,alicheza NBA all-star mara 18,kikosi bora cha NBA mara 15,mlinzi wa muda wote mara 12 mbali na mengineyo.
SEKUNDE 24 ZA MAJONZI MECHI ZOTE*
Haikuwa rahisi kwa wachezaji katika mechi za leo kujizuia kuomboleza kifo cha Kobe Bryant ambapo mechi zote za alfajiri ya leo zililazimika kuchelewa kuanza kwa sekunde 24 kupisha ombolezo la kifo hicho.
.
.
@materekajr
#dailysporttz



:

















: