DUNIA YAADHIMISHA MIAKA75 YA D-DAY

UINGEREZA: DUNIA YAADHIMISHA MIAKA 75 YA D-DAY

Rais Donald Trump ameungana leo na viongozi wa nchi 16 katika kuadhimisha miaka 75 tangu kuanza kwa operesheni ya kijeshi iliyoikomboa Ulaya kutoka mikononi mwa Wanazi wa Ujerumani, maarufu kama D-Day

Trump atakuwa pamoja na wenyeji wake, Malkia Elizabeth II, Waziri Mkuu Theresa May, na pia Kansela wa Ujerumani Angela Merkel katika maadhimisho hayo yanafanyika katika mji wa Portsmouth

Tarehe kama ya leo mwaka 1944, wanajeshi 170,000 wa nchi washirika walivuka bahari na kutua kwenye fukwe za Normandy nchini Ufaransa, ikawa mwanzo wa mwisho wa utawala wa Wanazi wa Ujerumani waliokuwa wameyakalia maeneo makubwa ya Ulaya katika vita vikuu vya pili

FAINALI YA CAF. KURUDIWA

#BREAKING
– Fainali ya Michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika “CAF Champions League” Mkondo wa Pili Kati ya Waliopewa Ubingwa, Klabu ya Esperance de Tunis πŸ‡ΉπŸ‡³ dhidi ya Wydad Casablanca πŸ‡²πŸ‡¦, itarudiwa upya nchini Afrika Kusini πŸ‡ΏπŸ‡¦; Ikumbukwe game hii ilivunjika Dakika ya 62 kufuatia sintofahamu ya mwamuzi kukataa goli La WAC na wao Kuamua kugomea kucheza Dakika zilizosalia na kumchukua mwamuzi kuwapa Ubingwa wa Mezani Esperance.
.
– Esperance wametakiwa kurejesha Kombe na Medali za Ubingwa ambazo walipewa wikendi siku ya fainali, Matokeo ya Mchezo huo yamefutwa Miamba hao wa Tunisia walikuwa wakiongoza 1-0 na 2-1 kwa Aggregate. Hivyo Sasa game itachezwa upya Mwezi Julai Baada ya Michuano ya AFCON kutamatika.
#CAFCL #CAFCLFinal
@Sokawaytz

Samatta. Kuwindwa na vilabu vinne kutota uingereza

– Klabu ya Brighton inaongoza mbio za vilabu vya Uingereza kumuwania Mshambuliaji hatari wa Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta.. Kwa mujibu wa @thesunfootball.
.
– Aston Villa, Leicester, Watford na Burnley vilabu vyote vinatajwa hivi karibuni kutoa dau la Β£12m kumsajili nahodha huyo wa timu ya taifa ya Tanzania; Na Samatta, mwenye umri wa miaka 26, inaeleweka kuwa ana nia ya kuhamia England baada ya msimu bora katika Ligi Kuu ya Ubelgiji.
.
– Samatta 26; Alifunga mabao 23 na kuisaidia Genk kutwaa Ubingwa wa Ligi, huku yeye akishinda tuzo ya Shoe Ebony – tuzo itolewayo kwa mchezaji bora wa Ubelgiji anaetokea Bara la Afrika.. hapo awali imewahi kuchukuliwa na Mastaa kama Romelu Lukaku, Vincent Kompany na Michy Batshuayi.
.
– Samatta ataongoza mashambulizi akiwa Kama nahodha katika timu yake ya taifa ya Tanzania kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika baadaye mwezi huu – ni kwa mara ya kwanza Tanzania inafuzu Michuano hiyo tangu 1980; lakini baada ya mashindano hayo kumalizika, anatarajia kuondoka Genk, ambayo alijiunga nayo Januari 2016 kutoka klabu ya TP Mazembe ya DR Congo, na nia yake ni kucheza Ligi Kuu ya Uingereza.
.
– Brighton imekuwa ikimfuatilia Samatta kwa muda na aliyekuwa kocha wao, Chris Hughton alikuwa shabiki mkubwa, wakati kocha mpya, Graham Potter pia anamkubali Mchezaji Hugo bora Mara Moja wa Afrika.
.
– Lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa wapinzani wenzao katika Ligi, Watford na Aston Villa na klabu za AS Roma na Lyon ya Ufaransa…
#Updates #transfers
@Sokawaytz

Gianni Infantino…. Kuendelea. Kuwa raisi wa FIFA

– Gianni Infantino amechaguliwa tena kuongoza Shirikisho La Soka Duniani “FIFA” kama raisi kwa Mara ya Pili bila ya kuwa na mpinzani yoyote.
.
– Muitaliano huyo Raia wa Uswisi mwenye umri wa miaka 49, amechaguliwa tena kuongoza hadi mwaka 2023 bila kuwa na mpinzani; Kachaguliwa katika mkutano wa kila mwaka wa FIFA huko jijini Paris, Infantino alichukua kijiti hicho kutoka kwa aliyekuwa Raisi wa Shirikisho hilo Sepp Blatter Mara ya kwanza Mwaka 2016.
.
– Rais wa zamani wa FIFA, Blatter alikuwa Katika kiti hicho kwa miaka 17 mpaka alipokutana na kifungo katika Soka kufuatia kashfa ya rushwa mwaka 2015; Katibu mkuu wa zamani wa Uefa ambaye ndiye Raisi wa FIFA Kwasasa, Infantino alikuja na pendekezo la upanuzi wa mataifa Shiriki katika Kombe la Dunia kutoka timu 32 hadi 48 kwa mashindano ya mwaka 2026 ambayo yatafanyika Marekani, Canada na Mexico.
.
– Mpango huo wa kuleta upanuzi katika Kombe la Dunia ulitakiwa kuanza mwaka 2022 lakini ulikataliwa mwezi uliopita… Mwezi Machi, FIFA iliidhinisha mpango ya Raisi Infantino kuwa Kombe la Dunia kwa Vilabu (FIFA Club World Cup) kuwa na timu 24 kuanzia mwaka 2021, licha ya klabu za Ulaya kutaka kupinga ongezeko la mashindano hayo..
#Updates
@Sokawaytz

Odoi– asain. Mkataba. Mpya chelsea

– Callum Hudson-Odoi atasaini mkataba mpya wa miaka mitano kuendelea kuitumikia klabu yake ya Chelsea. Kinda huyo wa Kiingereza anatarajia kupokea mshahara wa Β£100k kwa wiki kuendelea kuhudumu Stamford bridge.
.
– Chelsea ilikuwa karibu kumpoteza Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 baada ya kuwasilisha ombi la kutaka kuondoka klabuni hapo mwezi Januari alipokuwa na miezi 18 tu katika mkataba wake; Bayern Munich iliwasilisha dau la Β£35m ($44m) kwa ajili ya kumsajili Hudson-Odoi dau ambalo lilikataliwa na Chelsea..
#Updates #transfers
@Sokawaytz

JAY. Z. ATANGAZWA KUWA RAPA BILIONEA WA KWANZA DUNIANI


Jay-Z ametangazwa rasmi na Jarida la Forbes kuwa ndiye bilionea wa kwanza wa Muziki wa HipHop baada ya kujijengea utariji wake kutokana na muziki, mali, fasheni na uwekezaji huku akikadiriwa kuwa na utajiri wa jumla ya dola bilioni 1

Jarida la Forbes limesema lilikuwa limekadiria utajiri wa Jay-Z kwa kuongeza mali zake mbalimbali na kutoa kiasi cha utajiri kinachomuwezesha kuishi maisha ya umaarufu

Jarida limetaja vyanzo vya mapato vya rapa huyo mkongwe kuwa ni pamoja na kuwa na hisa ya dola milioni 70 kwenye kampuni ya usafiri ya Uber, dola milioni 70 kwenye masuala ya sanaa, dola milioni 50 kwenye umiliki wa majumba ya kupangisha na muziki, umiliki wa β€˜Tidal’ inayouza nyimbo mtandaoni pamoja na umiliki wa Kampuni ya Roc Nation

Umaarufu wa Jay-Z ulianza kushamiri mnamo mwaka 1996 kwa kazi yake iliyomuwezesha kutoa albamu ya Reasonable Doubt

Aidha, Mke wa Jay-Z, Beyonce Knowles anaripotiwa kuwa na utajiri wa takribani dola milioni 335, alizotengeneza zaidi kutokana na muziki na kuidhinisha nembo

BENI:KUNDI LA WAASI LA. ADF LAUA WATU 12


Kundi linaloaminiwa ni la waasi wa The Allied Democratic Forces(ADF) limewaua watu hao katika mji wa Beni uliopo Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Meya ya mji huo, Modeste Bakwanamaha amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo, ambayo amesema yamekuwa yakishuhudiwa tangu siku ya Jumatatu Juni 03, 2019

Ripoti zinasema kuwa waasi hao walitekeleza mashambulizi hayo pia katika kambi ya Jeshi ya Rwangoma na kuua Wanajeshi wawili lakini baada ya muda walielemewa na kukimbia

Tangu mwaka 2014, makundi ya Waasi wamekuwa wakishambuliwa katika makazi hayo, suala lililowakasirisha wakazi wa mji huo wakitaka Serikali kufanya juhudi za kuimarisha usalama

Design a site like this with WordPress.com
Get started