

–
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ leo kimeondoka nchini kuelekea nchini Misri kwa ajili ya kuweka kambi maalum ya maandalizi ya michuano ya AFCON itakayofanyika nchini huo kuanzia Juni 21
–
Kocha wa Stars, raia wa Nigeria Emanuel Amunike amesema kuwa amechagua timu yenye vipaji ambayo ana imani italeta matokeo kwa ajili ya Taifa la Tanzania
–
Amesema “Vijana wengi wa Tanzania wana vipaji na ndio ambao nimewajumuisha kwenye kikosi changu, wapo ambao nimewaacha na sababu kubwa ni kushindwa kuwa na nidhamu, pia wapo wale ambao walishindwa kutimiza mazoezi na wengine hawapo fiti.”
–
Ameongeza kuwa “Najua kwamba kila mmoja anachaguo lake ila hamna namna ni lazima niwe na kikosi makini kitakachopambana, kwa vijana wadogo nimewajumuisha ili wapate uzoefu.”





























