

–
Klabu ya Simba SC imepanga kujitoa kwenye michuano ya Kagame Cup yanayotarajia kufanyika Julai 07 hadi 21 nchini Rwanda
–
Mkurugenzi wa klabu hiyo, Crescentus Magori amesema watapeleka barua rasmi kwenye Shirikisho la soka Tanzania kuwajulisha kutoshiriki mashindano hayo kwasababu za kiufundi
–
Magori amesema iwapo watashiriki mashindano hayo hawatapata muda wa kuweka kambi nje ya nchi kwa ajili ya mashindano ya Afrika Caf Champions League raundi ya awali yatakayoanza Agosti 9 mpaka na ligi kuu Tanzania Bara itakayoanza mwishoni mwa mwezi wa nane
–
Amedai kutokana na sababu za kubadilika kwa ratiba ya CAF, michuano ya Afcon itakayofanyika Misri itakuwa ngumu kwa klabu ya Simba kushiriki mashindano ya Kagame Cup
–
Simba inatarajia kwenda kuweka kambi ya mwezi mmoja nje ya nchi kujiandaa na msimu wa 2019/20


























