
– Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania, Emmanuel Amuneke amesema kuwa upande wao utajitahidi kufuzu hatua ya Mtoano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka hui 2019.. Taifa Stars imefanikiwa kufuzu kucheza mashindano haya baada ya miaka 39 na wamepangwa pamoja na Miamba wa Afrika Magharibi timu ya taifa ya Senegal, Algeria kutoka Afrika ya Kaskazini na wapinzani wenzao kutoka Afrika Mashariki, timu ya taifa ya Kenya “Harambee Stars” katika Kundi la C.
.
– Katika maandalizi ya Kuelekea Michuano hii, Tanzania Imecheza mechi mbili za Kirafiki, Mechi ya kwanza ni dhidi ya Misri wakipoteza kwa Kufungwa 1-0 na mechi ya pili ni dhidi ya Zimbabwe ikimalizika kwa Sare ya goli 1-1..
.
🗣 Amunike 🗣.. “Lengo letu kucheza mechi za kirafiki ni kujiweka fiti kiasi ambacho tunaweza Kwa bora katika Mashindano..
🗣 “Bila shaka tunacheza katika kundi gumu, lakini tutajitahidi kucheza vizuri kwa ubora wetu kufuzu raundi ya Pili..
.
– Kuhusu Kukosekana kwa Sadio Mane katika Mchezo wa kwanza wa kundi, Kocha amefunguka..
🗣 “Sidhani kwamba Senegal itakuwa dhaifu bila Mane, yeye ni mchezaji mkubwa lakini wana wachezaji wengine wengi wakubwa na wenye majina makubwa wa kuweza kushindania Mashindano”.
.
– Tanzania itaanza kampeni yao katika mashindano dhidi ya Senegal siku ya Juni 23, kisha kucheza dhidi ya Harambee Stars siku nne baadaye kabla ya mchezo wao wa mwisho wa Kindi Julai 01 dhidi ya Algeria..
#TotalAFCON2019 #AFCON2019 #zamuyetu2019🇹🇿⚽ @Sokawaytz













