CHINA YAIONYA MAREKANI KUHUSU KUTUMA WANAJESHI MASHARIKI YA KATI

CHINA YAIONYA MAREKANI KUHUSU KUTUMA WANAJESHI MASHARIKI YA KATI

China imeionya Marekani baada ya Marekani kutangaza kutuma Wanajeshi 1,000 wa ziada katika eneo la Mashariki ya Kati huku mvutano kati ya nchi hiyo na Iran ukiongezeka

Pia, imeisihi Iran kutojitenga na makubaliano ya nyuklia baada ya nchi hiyo kusema itarutubisha Uranium kwa kiwango kikubwa iwapo nchi zenye nguvu zitashindwa kutimiza ahadi zake chini ya makubaliano ndani ya siku 10

Marekani iliongeza shinikizo lake dhidi ya Iran hapo jana, kwa kutangaza kutuma Wanajeshi zaidi wa majini, ardhini na anga ili kuongeza nguvu zaidi kwa vikosi vilivyopo Mashariki ya Kati

Aidha, imetoa picha kadhaa ambazo inasema ni ushahidi mwingine kuwa Iran inahusika na mashambulizi dhidi ya meli za kubebea mafuta yaliyotokea katika Ghuba ya Oman wiki iliyopita lakini Iran inakanusha madai hayo

ETHIOPIA: INTERNET YAREJEA BAADA YA KUKATWA KWA WIKI MOJA

ETHIOPIA: INTERNET YAREJEA

BAADA YA KUKATWA KWA WIKI MOJA

Huduma hiyo imerejeshwa leo baada ya mtandao kuzimwa kwa muda wa wiki moja. Shirika la Mawasiliano la Ethio Telecom limeahidi kuwafidia wateja wake

Kwa muda wote Wananchi hawakuwa na uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii huku Serikali ikishindwa kutoa sababu za hatua hiyo ya kuzima mtandao

Taarifa zisizo rasmi zinaeleza kuwa Serikali ilizima mtandao ili kuepusha udanganyifu kwenye mitihani ya Taifa ya elimu ya Sekondari

NAIBU SPIKA AWATOA BUNGENI WABUNGE WATATU WA CHADEMA –

NAIBU SPIKA AWATOA BUNGENI WABUNGE WATATU WA CHADEMA

Dkt. Tulia Ackson amewatoa Bungeni Wabunge hao walioibua zogo kuhusu uamuzi wa Mbunge wa Kasulu Vijijini(CCM), Augustine Vuma kuchana kitabu cha hotuba mbadala ya bajeti ya Kambi Rasmi ya Upinzani mwaka 2019/20

Wabunge hao Esther Matiko(Tarime Mjini), John Heche(Tarime Vijijini) na Dkt. Emmaculate Sware(Viti maalum), walipinga uamuzi wa Dkt. Tulia kumtaka Vuma kuomba radhi kwa alichokuwa akizungumza wakati akichana kitabu hicho na si kitendo chake cha kuchana kitabu

Dkt. Tulia alichukua uamuzi huo kwa maelezo kuwa taarifa iliyoombwa na Mbunge wa Tunduma (CHADEMA), Frank Mwakajoka baada ya Vuma kuchana kitabu hicho, inazungumzia Mbunge kutamka maneno yasiyoruhusiwa Bungeni

Vuma wakati akizungumza utekelezaji mzuri wa miradi ya Serikali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), alishika kitabu hicho cha upinzani na kusema kina maneno yasiyofaa na kinafaa kuchanwa kisha akakichana

Mwakajoka akitumia Kanuni ya 64 alitoa taarifa kuwa “Mchangiaji wakati akizungumza amechana hotuba ya upinzani ndani ya Bunge nafikiri jambo hili ni dharau kubwa. Ni kutojielewa kwa Mbunge na hajui kwa nini vitabu hivi amepewa. Achukuliwe hatua maana tumemuona kama kichaa fulani hivi ndani ya Bunge.”

HISTORIA YA MICHUANO YA AFCON

👉🏻 Ijumaa ya Wiki hii Rasmi Michuano ya Kombe La Mataifa ya Afrika “AFCON 2019” itaanza kutimua vumbi kwa jumla ya Mataifa 24 kuwania kuwa Bingwa mmoja mpya wa Afrika..
:
– KUNDI A… Kuna Wenyeji ambao ni Misri..
✍🏻 Misri hujiita “Pharaoh” 🇪🇬 wanafuzu AFCON Kwa Mara ya 24… Ni Mabingwa wa Kihistoria wakitwaa Ubingwa huu Mara Saba, licha ya kutwaa Ubingwa Pia wamepigwa fainali Mara Mbili, Wamemaliza mshindi wa tatu Mara tatu na Mshindi wa Nne Mara tatu… Tayari wametangaza Kikosi Chao cha Wachezaji 23 (Pichani)… (Kufuzu mtoano 9.5/10).
:
✍🏻 DR Congo 🇨🇩, Hawa ni Mabingwa wa Afrika Mara mbili, na Pia wameweza kushika nafasi ya tatu Mara mbili… DR Congo wamekuwa washindi wa Nne mara moja…Tayari wametangaza Kikosi Chao cha Wachezaji 23 (Pichani)… (Kufuzu Mtoano 8/10).
:
✍🏻Uganda 🇺🇬, Wanajiita The Cranes wanacheza AFCON kwa Mara ya Saba.. Historia yao hawajawahi kuwa Mabingwa zaidi ya kupoteza Fainali Mara moja, Waganda hawa Pia wamemaliza nafasi ya Nne Mara Moja… (Kufuzu Mtoano 6.5/10).
:
✍🏻 Zimbabwe 🇿🇼, Kama kocha wao Alivyosema wanaingia kwenye kundi Kama Underdog, kwani hawana historia yoyote Kama wapinzani wao walivyo licha ya kuwa na Timu Bora na Wachezaji wazoezu zaidi… Wanaingia katika AFCON yao ya Nne mwaka huu, Mara yao ya mwisho kushiriki ni 2017, 2006 na 2004; Mara zotee hizo wameishia tu hatua ya makundi.. (Kufuzu Mtoano 6/10).
:
👉🏻 Mechi ya kwanza itapigwa Juni 21,2019 kwa mujibu wa Ratiba ya CAF… Ratiba kamili mpaka mwisho wa kundi hilo La A… Games zote zitapigwa Dimba La Cairo International Stadium isipokuwa mechi ya mwisho ya Kundi hili itapigwa 30 June Stadium..
📅 Juni 21,2019; Misri v Zimbabwe
📅 Juni 22,2019; DR Congo v Uganda.
📅 Juni 26,2019.
Misri v DR Congo
Uganda v Zimbabwe
📅 Juni 30,2019.
Uganda v Misri
Zimbabwe v DR Congo
#TotalAFCON2019 #AFCON2019
@sokawaytz

Eduardo Vargas Sasa kafunga Magoli 38 kwa timu yake ya taifa ya Chile 🇨🇱,

GOAL MACHINE 🙌🏻🇨🇱 @eduardovargasrj1
:
✍🏻 Eduardo Vargas Sasa kafunga Magoli 38 kwa timu yake ya taifa ya Chile 🇨🇱, hivyo amekuwa mfungaji bora wa muda wote namba mbili Akimpita Marcelo Salas (37) katika Orodha hiyo ya wafumania nyavu wa La Roja 🇨🇱… Kinara wao Ni Alexis Sanchez akiwa na Magoli 42..
:
✍🏻 Eduardo Vargas 🇨🇱, Baada ya kufunga Magoli Mawili dhidi ya Japan 🇯🇵, amekuwa Mchezaji anaecheza Soka mpaka Sasa (Ambaye hajastaafu) kuwa na Magoli mengi zaidi katika Mashindano ya Copa America akifikisha Magoli 12, Akimpita Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Peru 🇵🇪, Paolo Guerrero mwenye Magoli yake 11..
:
✍🏻 Eduardo Vargas Sasa amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Timu ya taifa ya Chile katika Historia ya Michuano ya Copa America.. Magoli yake mawili dhidi ya Japan 🇯🇵 yamemfanya kufikisha Magoli 12 akimpita Marehemu ambaye ni Legend wa Chile, Enrique Hormazábal (R.I.P) mwenye Magoli 10..
#Updates #copaamerica #CopaAmerica
@Sokawaytz

Design a site like this with WordPress.com
Get started