Brazil, Neymar….kuondoka PSG…rasmi

– Paris St-German wako tayari kumuuza mshambuliaji nyota wa Brazil, Neymar mwenye umri wa miaka 27 msimu huu Baada ya kuonesha nia ya kutaka kutimka klabuni hapo… Raisi na Mmiliki wa PSG, Bilionea Nasser Al Khelaïf Amethibitisha kuwa Mchezaji anaetaka kuondoka ni ruksa na ikiwa atataka kusalia ndani ya Klabu ni lazima afuate kanuni, taratibu na misingi yote inayotolewa na Uongozi wa timu.
.
– Real Madrid huenda wakamjumuisha kiungo wa kati Mbrazil Casemiro 27, kwa ofa yoyote ya kumsajili Neymar kutoka PSG… Wakati huo huo FC Barcelona inapambana kutaka kumrejesha Camp Nou kwani wao ndio walimuuza kwenda Paris… Kwa mujibu wa Taarifa, Nahodha wa @fcbarcelona, Lionel Messi ametoa pendekezo lake La kusajiliwa kwa Neymar kuliko Antoine Griezmann ambaye nae yupo mbioni kutua kwa Miamba hao wa Laliga..
#transfers #Updates

AC Milan imemtangaza Marco Giampaolo kuwa kocha wao mpya Mkuu

OFFICIAL! Klabu ya AC Milan imemtangaza Marco Giampaolo kuwa kocha wao mpya Mkuu kwa Mkataba mpaka mwaka 2021.. Mswisi huyo anakuja Milan kuchukua Mikoba iliyoachwa wazi na Mtukutu, Gennaro Gattuso “Rino” ambaye alitangwa kuwa ataachana na Klabu kwa makubaliano binafsi na Uongozi.. Hiyo ilikuja Baada ya kushindwa kuiwezesha timu hiyo Kufuzu kucheza Champions league.
.
– Giampaolo 51,alianza kujulikana katika ukocha June 2015 Baada ya kupewa kubarua cha kuinoa Klabu ya Empoli… Siku ya Julai 2016, Giampaolo alitangazwa kuwa kocha Mkuu wa Klabu ya Sampdoria kwa Kipindi cha Miaka miwili akichukua mikoba ya Vincenzo Montella… Baada ya msimu wa 2018-2019 kumalizika, Giampaolo alivunja Mkataba wake na Klabu ya Sampdoria, kisha June 2019, Giampaolo akatangazwa kuwa kocha mkuu wa Klabu ya Kihistoria, AC Milan kwa Mkataba mpaka 2021 na Kipengele cha kupanua Mkataba mpaka kufikia 2022..
#transfersUpdates
@Sokawaytz

JESHI LA POLISI: TAARIFA ZA TISHIO LA SHAMBULIO DAR, TUNAZIFANYIA KAZI

JESHI LA POLISI: TAARIFA ZA TISHIO LA SHAMBULIO DAR, TUNAZIFANYIA KAZI

Jeshi la Polisi limesema kuwa taarifa hizo hawakutaka kuzisambaza na wanaendelea kuzifanyia kazi

Mussa Taibu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni amewataka Wananchi kutoa taarifa za viashiria vyovyote vya hatari watakavyosikia au kukutana navyo

Amesema kuwa simu za Jeshi la Polisi zinapatikana wakati wote hivyo Wananchi wasisite kutoa taarifa muda wowote ule

Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi huu baada ya kusambaa kwa taarifa za kuwepo kwa viashiria vya shambulio katika eneo la Msasani hususani katika migahawa na Slipway Shopping Center Msasani

Taarifa hizo za tahadhali zimetolewa na Ubalozi wa Marekani nchni Tanzania

RAIS MAGUFULI KUONGOZA KONGAMANO LA KOROSHO, MTWARA

RAIS MAGUFULI KUONGOZA KONGAMANO LA KOROSHO, MTWARA

Rais Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la korosho litakalofanyikia mkoani Mtwara Julai 12 na 13 mwaka huu

Tangazo hilo lililotolewa leo na Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC), limesema lengo la kongamano ni kuwavutia Wawekezaji wa nje na wa ndani waanzishe miradi na viwanda vya kusindika hasa katika mikoa ya Lindi na Mtwara

Tangazo hilo limesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa korosho ghafi duniani, kwa msimu wa 2017/18 ilizalisha tani za ujazo 313,826, lakini 90% za korosho hizo huuzwa nje ya nchi zikiwa ghafi kutokana na uwezo mdogo wa ubanguaji

Mkutano huo unakuja wakati tayari Rais Magufuli ameshaengua mawaziri watatu tangu Novemba 2018 wote wakitajwa kushindwa kusimamia biashara ya korosho mbali na sababu nyingine

WADAIWA SUGU WA MADENI YA CIS NA FACF WATAKIWA KULIPA MADENI –

WADAIWA SUGU WA MADENI YA CIS NA FACF WATAKIWA KULIPA MADENI

Wizara ya Fedha na Mipango inawataka wadaiwa sugu wa madeni ya mikopo ya Commodity Import Suport(CIS) na Food Aid Counterpart Fund(FACF), walipe madeni yao mara moja

Ni mikopo yenye masharti nafuu yaliyotolewa kwa Taasisi, Kampuni, Viwanda na Wafanyabiashara na wakopaji walitakiwa kulipa deni bila kutozwa riba katika kipindi cha Miezi 18 tangu kukopeshwa

Mkopaji akichelewa kulipa katika kipindi cha miezi 18 tangu kupatiwa mkopo, atapaswa kulipa riba ya asimilia sawa na kiwango kinachotozwa na Benki Kuu ya Tanzania inapoikopesha Serikali katika kipindi husika

Zaidi ya Kampuni 980 zilikopeshwa chini ya utaratibu huu na Serikali inatangaza kwa mara ya Mwisho kufuatia baadhi ya wadaiwa kushindwa kuitikia wito wa matangazo ya awali ya tarehe 30/12/2015 na 05/04/2018

Baadhi ya wadaiwa ni wadaiwa ni Yusuph Manji(Farm Equipment Tanzania Ltd, Quality Group Ltd, Funhill Motors Ltd, Quality Seed Ltd, Quality Garage Ltd), Mohamed Dewji( 21st Century Textiles Ltd, Afritex Ltd)

Wengine baadhi ni S. S Rashid(Pwani Tours and Safari Ltd, Pwani Investment Ltd), Issack Bugali(Dar es Salaam International School Trust Fund, Upoloto Farm Ltd), Stephen Wassira(Siza Cold Storage Co.Ltd), na Hashim Rungwe(Bahari Motor Co Ltd)

Borussia Dortmund Imethibitisha kumsajili beki wao Mats Hummels

– Hii leo Klabu ya Borussia Dortmund Imethibitisha kumsajili wakimrejesha nyumbani beki wao Mats Hummels ambaye walimuuza kwenda Bayern Munich na Sasa wamemrudisha kwa dau La £33.8m… Baada ya Usajili huo Borussia Dortmund imetumia £100m kwa Wachezaji wanne tu..
🇩🇪 Mats Hummels (£33.8m)
🇧🇪 Thorgan Hazard (£22.5m)
🇩🇪 Julian Brandt (£22.1m)
🇩🇪 Nico Schulz (£22m)
#transfersUpdates #bundesliga

Simba yaleta kitu kipya toka afrika kusini

Ryan Moon… Ndiye Mshambuliaji wa Kimataifa wa Afrika Kusini ambaye yupo katika Mazunguko na Klabu ya Simba SC ya Tanzania… Winga huyu alijiunga na Klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini Mwaka 2016 akitokea Maritzburg United akasaini Mkataba ambao unafikia Tamati Juni 30,2019.
.
– Kwa Taarifa nilizonazo ni kwamba Kaizer Chiefs imeachana nae Baada ya Mkataba wake kumalizika Mwishoni mwa mwezi huu… Simba SC na Klabu yake ya zamani Maritzburg Ndio zinamtaka… Tangu atue Chiefs kacheza games 46 kafunga Magoli Sita na Assist Moja… Katika timu ya taifa Alianza kucheza mwaka 2017 kacheza mechi Nane na kufunga Goli Moja… Msimu huu kucheza games 15 Hana Goli kadi, mbili za njano… Ana miaka 22…
#Updates #transfers
@Sokawaytz

BRAISON, HAULE WAONGEZA MKATABA AZAM FC

BRAISON, HAULE WAONGEZA MKATABA AZAM FC

Nyota wawili wa Azam FC, kipa Benedict Haule na kiungo Braison Raphael, wameongeza mkataba wa miaka miwili kila mmoja wa kuendelea kuitumikia timu hiyo.

Wawili hao ambao kila mmoja alikuwa akimaliza mkataba, wanatarajia kudumu kunako viunga vya Azam Complex hadi 2021.

Huo ni muendelezo wa uongozi wa timu chini ya Afisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin ‘Popat’, kwa kushirikiana na benchi la ufundi, linaloongozwa na kocha mpya, Etienne Ndayiragije, kuwabakiza nyota wenye umuhimu kikosini.

#Usajili #AzamFC #Michezo #Sports #TransferNews #AzamTVUpdates #BraisonRaphael #BenedictHaule #AzamComplex @azamfcofficial

Design a site like this with WordPress.com
Get started