INDIA: JOTO LAZIDI KUONGEZEKA, WATU 92 WAFARIKI

INDIA: JOTO LAZIDI KUONGEZEKA, WATU 92 WAFARIKI

Joto limezidi kuwa kali katika Jimbo la Bahir katika kipindi hiki ambapo India inakumbana na kipindi kidogo cha mvua katika kipindi cha takribani miongo 10 iliyopita

Vifo vingi huko Bahir vimerekodiwa katika maeneo ya Aurangabad, Gaya, na Nawada, ambapo joto limefikia jotoridi 45, huku watu 562 wakiwa wamelazwa na kuongeza hofu ya vifo kuongezeka

Mamlaka zinasema kuwa idadi kamili ya vifo haitakuja kujulikana kwa hakika kwa sababu vifo vingine vinavyotokea na kuhusishwa na joto, ndugu huzika miili kabla haijathibitishwa rasmi

Mamlaka zimewataka watu kukaa ndani, shule na vyuo vimefungwa, masoko yametakiwa kufunguliwa kuanzia saa kumi na moja alifajiri hadi saa kumi na moja jioni

Joto hilo ilimeathiri takribani mbili ya tatu ya nchi ya India, huku Jimbo la Magharibi la Rajasthan lilirekodi jotoridi 50 na Jimbo la Maharashtra lilikumbwa na ukame mkubwa kwa kipindi cha miaka 47

TAHADHARI: UBALOZI WA MAREKANI UGANDA WATOA ONYO LA SHAMBULIO

TAHADHARI: UBALOZI WA MAREKANI UGANDA WATOA ONYO LA SHAMBULIO

Tahadhari iliochapishwa katika ukurasa rasmi wa mtandao wa kijamii wa balozi hiyo umesema kuna uvumi wa mashambulizi katika maeneo yanayopendwa na raia wa kigeni Afrika Mashariki ikiwemo Uganda

Ubalozi huo umesema kuwa ijapokuwa hauna ushahidi wa kutosha kuhusu tishio hilo ama habari kuhusu wakati ambapo mashambulizi hayo yatafanyika umewaonya Wakazi kuchukua tahadhari

Ubalozi umewataka raia kuwa macho wakati wowote katika maeneo wanayotembelea, kuwaangalifu dhidi ya makundi ya watu wengi na kufuatilia habari zinazotolewa mara kwa mara

Tahadhari hiyo inatoka siku moja tu baada ya ubalozi huo kutoa tahadhari nchini Tanzania ambayo imewatakaa Wakazi kuchukua tahadhari hususani wale waliopo katika maeneo ya Masasani na Masaki

Tahadhari hiyo ilibainisha kuwa, maeneo yanayolengwa ni mahoteli na migahawa ambayo hutembelewa na watalii ikiwemo eneo maarufu la maduka ya Slipway

KENYA: ALIYEKUWA MGOMBEA URAIS KENYA AKAMATWA AKISAFIRISHA BANGI

KENYA: ALIYEKUWA MGOMBEA URAIS KENYA AKAMATWA AKISAFIRISHA BANGI

Aliyekuwa mgombea Urais nchi Kenya mwaka 2017, Jaffer Isaak Sora amekamatwa huko Marsabit baada ya Polisi kukamata Kilo 445 za bangi kwenye gari lake

Kamanda wa Polisi Kanda ya Mashariki, Esther Kihiko amesema Mwanasiasa huyo mwenye miaka 45 alikuwa alisafirisha bangi hizo zinazodhaniwa zimetoka nchini Ethiopia

Sora alisimamishwa na Maafisa Polisi katika kizuizi cha Polisi siku ya Jumatano usiku lakini alikataa ombi la Polisi kutaka kupekuwa gari lake

Baada ya hapo, Polisi walimkamata na kumpeleka kituo cha Polisi cha Marsabit ambapo alifanikiwa kupata bangi hizo zikiwa katika tela(Trailer)

Real Madrid imethibitisha..kumsajili kiungo kutoka atletico madrid

OFFICIAL: Real Madrid imethibitisha kwamba wamefikia makubaliano na Klabu ya Atletico Madrid kwa mauzo ya kiungo wa Kimataifa wa Hispania, Marcos Llorente… Kiungo huyo Atasaini Mkataba wa miaka Mitano kuwatumikia wababe hao wa Wanda Metropolitano..
.
– Ujio huu wa Nyota huyo unaashilia kwa 100% kwamba Rodri yupo hatua za mwisho kutua ndani ya Mabingwa wa Uingereza Klabu ya Manchester City..
#transfersUpdates

Shirikisho La Soka Rwanda lathibitisha vilabu vinavyo kushiriki Michuano ya #CECAFAKagameCup kwa 2019;

OFFICIAL!! Shirikisho La Soka nchini Rwanda limethibitisha vilabu vilivyo toa Uthibitisho wa mwisho kushiriki Michuano ya #CECAFAKagameCup kwa Mwaka huu 2019; Michuano hiyo itafanyika Kigali Rwanda kuanzia mwezi Ujao.
.
– Kwa Mujibu wa FERWAFA Ratiba na Makundi ya Michuano hii ipo tayari na Inatangazwa mapema hapo Kesho Ijumaa kuanzia majira ya Saa Sita za Mchana Makao Makuu ya Shirikisho hilo ambapo ndipo utafanyika Mkutano na Waandishi wa Habari.
:
– Timu kutoka Tanzania Zilizothibitisha kushiriki ni Mabingwa watetezi, Azam FC na KMC FC zote zikitokea Dar ES Salaam, huku Wawakilishi kutoka Visiswani Zanzibar ni Mabingwa, KMKM.
– Wawakilishi kutoka Rwanda ni APR FC na Mabingwa wa Nchi Klabu ya Rayon Sports FC.
– Wawakilishi kutoka Nchini Kenya ni Bandari FC na Mabingwa wa Ligi ya Kenya, Klabu ya GOR Mahia FC (Walifungiwa na Kifungo Chao Kimetenguliwa).
– Wawakilishi kutoka Uganda ni Proline FC na Mabingwa wa Ligi ya Uganda, KCCA FC.
– Wawakilishi kutoka Djibouti ni Klabu ya AS Ports, Wawakilishi kutoka Somalia ni Klabu ya Heegan, Wawakilishi kutoka DR Congo ni Mabingwa TP Mazembe, Wawakilishi kutoka Zambia ni klabu ya Green Buffaloes.
.
– FERWAFA Pia Imethibitisha kabla ya Ijumaa inasubiri majibu kamili katoka katika Uongozi wa vilabu vya DC Motema Pembe ya DR Congo na Miamba wa Soka nchini Malawi Klabu ya Big Bullets. #CECAFAKagameCup
@Sokawaytz

Historia ya Vigogo wa kundi E katika Afcon 2019

👉🏻 Ijumaa ya Wiki hii Rasmi Michuano ya Kombe La Mataifa ya Afrika “AFCON 2019” itaanza kutimua vumbi kwa jumla ya Mataifa 24 kuwania kuwa Bingwa mmoja mpya wa Afrika..
:
KUNDI E.
✍🏻 Tunisia 🇹🇳, Mabingwa mara Moja wa Afrika, wanaingia Kushiriki Michuano hii kwa Mara ya 19.. Licha Ubingwa Pia Tunisia imepigwa fainali Mara mbili na kumaliza mshindi wa tatu Mara Moja… (Kufuzu Mtoano 9/10).
:
✍🏻 Mali 🇲🇱, Mwaka huu wao wanacheza AFCON yao ya 11.. Hawana Historia ya kuwa Mabingwa katika Michuano hii zaidi ya kufika fainali Mara Moja na kupoteza mwaka 1972 mbele ya Congo 🇨🇬.. (Kufuzu Mtoano 8.5/10).
:
✍🏻 Angola 🇦🇴, Baada ya kukosekana hatimae wamerejea tangu 2013.. Hawajawahi Kutwaa Ubingwa huu wa Afrika zaidi ya kufika Nusu fainali Mara Mbili.. Kwao hii ni AFCON yao ya Nane kushiriki… (Kufuzu Mtoano 7/10).
:
✍🏻 Mauritania 🇲🇷, Novemba 2018 ndio siku ya Historia ndani ya taifa La Mauritania, kwani waliweza Kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa Mara ya kwanza kabisa.. Wao katika Kundi hili ndio Wageni wakijaribu kuweka rekodi mpya na ya kwanza katika Ushiriki wao wa kwanza… (Kufuzu Mtoano 4/10).
:.
– Kwa mujibu wa Ratiba ya Shirikisho La Soka Barani Afrika, Mechi ya kwanza ya Kundi hili itapigwa Juni 24.. Uwanja wa Suez Stadium jijini Suez utakuwa mwenyeji wa mechi za Kundi hili.. Isipokuwa mechi ya mwisho ya Kundi hili itapigwa ndani ya jiji La Ismailia katika Dimba La Ismailia Stadium..
:
📅 Juni 24,2019.
Tunisia v Angola
Mali v Mauritania
📅 Juni 28,2019.
Tunisia v Mali
📅 Juni 29,2019.
Angola v Mauritania
📅 Julai 02,2019.
Mauritania v Tunisia
Angola v Mali.
#TotalAFCON2019
© @Sokawaytz

MICHEZO: MSHAMBULIAJI WA KLABU YA MBEYA CITY ASAJILIWA NA TP MAZEMBE

MICHEZO: MSHAMBULIAJI WA KLABU YA MBEYA CITY ASAJILIWA NA TP MAZEMBE

Eliud Ambokile mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji amesajiliwa na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Taarifa zinaeleza kuwa Ambokile amesajiliwa kwa ada ya Shilingi za Kitanzania milioni 50

Hivi karibuni Klabu ya TP Mazembe ilituma ofa ya kumsajili mchezaji wa Klabu ya Yanga, Ibrahim Ajibu ambaye hata hivyo alikataa kujiunga na timu hiyo

KENYA: MTANZANIA AKUTWA NA HATIA KATIKA MAKOSA YA

KENYA: MTANZANIA AKUTWA NA HATIA KATIKA MAKOSA YA UGAIDI

Rashid Mberesero ambaye ni Mwenyeji wa mkoa wa Kilimanjaro amekutwa na hatia kutekeleza shambulio la kigaidi nchini Kenya mwaka 2015 katika Chuo Kikuu cha Garissa na kusababisha mauaji ya wanafunzi 148

Rashid pamoja na Wakenya wawili wamekutwa na hatia ya kufanya njama za kutekeleza ugaidi na kuwa Wanachama wa kundi la kigaidi la Al Shabaab lenye makao yake makuu nchini Somalia

Wakenya hao wawili wanajulikana kwa majina ya Hassan Edin na Mohammed Abdi maarufu ‘Mohamned Ali Abikar’, lakini pia Mahakama hiyo ilimuondoa katika mashtaka mtu wa nne, Sahal Diriye Hussein

Design a site like this with WordPress.com
Get started