
ROSTAM APINGA UFADHILI NDANI YA YANGA
Mfanyabiashara maarufu, Rostam Aziz, amesema kwa maoni yake Yanga inastahili kuendelea kuendeshwa kwa michango ya wanachama wake pamoja na vyanzo vingine vya mapato badala ya kumilikiwa na mtu binafsi au kuwa na mfadhili.
Ametaja vyanzo vingine vya mapato mbali na michango ya wanachama kuwa ni pamoja na wadhamini, makampuni kutangaza bidhaa zao, viingilio vya milangoni, biashara ya bidhaa mbalimbali kwa chapa ya Yanga kama vile jezi pamoja na haki za matangazo ya televisheni.
Mfanyabiashara huyo ambaye alikuwa akitajwa kuwa na mpango wa kuwekeza katika klabu hiyo amesema kwa mtazamo wake timu kubwa kama Yanga kuwa na mfadhili ni kuziba nafasi kwa wadhamini wengine ambao wangependa kutangaza bidhaa na huduma zao kupitia klabu hiyo, jambo ambalo litaipunguzia mapato.
.
.
βUfadhili ni mlango wa nyuma wa kumiliki,β amesisitiza.