#REPOST
.

.
Moja kati ya nafasi muhimu katika football ni ile ya kiungo, muhimu zaidi ni kiungo namba 6 maarufu kama kiungo mkabaji, tuanzie hapo
.
Kiungo mkabaji kama wengi wanavyomuita, inamaminika ni nafasi ya kufanya kazi chafu, wengine umuita “msafishaji” na kuamini sifa mama kwake ni kuwa na uwezo mkubwa wa kukaba na kulinda safu ya ulinzi katika mashambulizi ya kushtukiza
.
Nafasi hii kwa wafaransa waliipa jina “Water Carrier ” ikiaminika wako kila mahali. Klabu ya Nantes pale France ilisifika kuwazalisha viungo aina hii, France pale walitoka kina Christian Karambeu, Claude Makelele, Marcel Deschamps
.
Waswahili tunawaita “wakata umeme” labda chanzo ni mahusiano yetu na Tanesco 😂. Zidane aliwaita “Engine” kule Argentina nafasi hii wanaiita namba 5, Ureno ni “Trico”
.
Kutokana na maendeleo ya soka, Italia wanawaita “Regista”. Wakiamini kiungo kama huyo hapewi majukumu ya kukaba sana ama kuzuia, wanaamini nafasi yake ni kuchezesha timu(deep lying playermaker) mfano Jorginho Frello, Sandro Tonali, na Adre Pirlo
.
Italy wanaendelea kuamini kiungo mkabaji anabidi awe pembeni mwa kiungo huyo kama Matuidi anayekaa eneo la pembeni kwa Pjanic na Allan anachokifanya kwa Napoli, ama alichokifanya Mauricio Sarri pale Chelsea, alimchezesha Kante pembeni mwa Jorginho
.
Pale Barcelona na timu zenye ufanano wa falsafa ambayo ilitengenezwa na Johan Cruyff hususani timu ya taifa ya Uhispania kiungo ni kiunganishi wa eneo la walinzi na wachezaji wengine akitakiwa kuwa na uwezo mkubwa wa kupiga pasi zenye kuvuka mistari(pasing lanes) ama kuelekea pembeni (sideways) pia aweze kuzuia vertical passes zinazokuja eneo lake, hapa sasa Sergio Bousquet anahusika
.
Kuanzia miaka ya 2018 kumekuwa na namna nyingine ya kiungo huyu wa kati akiaminika kuwa (CDM), anakuwa anajumuika na mabeki wa kati wawili na kutengeneza jumla ya wachezaji watatu, kitaalam “third man concept”
.
Klopp tangu 2019 amekuwa muumini wa “third man concept” akimtumia Fabinho na Henderson kurudi kati ya Gomez na Van Djik ama pair yoyote ya Centre Back za Liverpool, yote hii ni kuwapa uhuru mabeki wake wa pembeni kuanzisha mashambulizi
.
RIPOTI YA SKAUTI NA @prosperbarthalomew