– Shabiki wa #TaifaStars Pierre Liquid na Wabunge waliokuwa nchini Misri , muda mfupi uliopita wamewasili Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam

Shabiki wa #TaifaStars Pierre Liquid na Wabunge waliokuwa nchini Misri kuipa nguvu #TaifaStars kwenye fainali za #AFCON2019 , muda mfupi uliopita wamewasili Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam, baada ya kushuhudia mchezo wa kwanza wa timu hiyo dhidi ya Senegal uliochezwa jana usiku.

JKT YAIVAMIA TZ PRISONS, YANASA MMOJA MWINGINE ANAFUATA. . .

JKT YAIVAMIA TZ PRISONS, YANASA MMOJA MWINGINE ANAFUATA. .
.
Katika kuhakikisha inarejesha makali yake kuelekea kwenye Ligi Kuu Tanzania msimu ujao, klabu ya JK Tanzania imefanikiwa kuinasa saini ya mshambuliaji Adam Adam kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Tanzania Prisons ya Mbeya. .
.
Adam Adam ni moja ya washambuliaji bora kabisa katika msimu uliomalizika akisaidiana na Ismail Aziz ambaye naye yupo kwenye mazungumzo ya mwisho ya kujiunga na klabu hiyo ya JKT Tanzania. .
.
Unafikiri muunganiko mzuri wa Ismail Aziz na Adam Adam walioufanya Prisons unaweza kuendelea kutamba pale JKT Tanzania?

Klabu ya Simba SC Imethibitisha kumuongeza Mkataba mpya beki wao na Nahodha Msaidizi, Mohammed Hussein “Tshabalala

OFFICIAL | ✍🏻 Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Klabu ya Simba SC Imethibitisha kumuongeza Mkataba mpya beki wao na Nahodha Msaidizi, Mohammed Hussein “Tshabalala”… Beki huyo wa Timu ya taifa ya Tanzania, Amesaini Mkataba huo mpya wa Miaka Miwili kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi..
#TPLTransferUpdates

Aaron Wan-Bissaka atafanyiwa vipimo vya afya wiki hii ndani ya viunga vya Klabu ya Manchester United

– Aaron Wan-Bissaka atafanyiwa vipimo vya afya wiki hii ndani ya viunga vya Klabu ya Manchester United ikiwa ni hatua za mwisho kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Klabu hiyo kwa dau La £55m ($70m) kutoka Crystal Palace.
.
– Beki huyo wa kushoto mwenye ufundi wa haina yake anakuwa ni usajili wa pili wa kocha wa United Ole Gunnar Solskjaer kuelekea msimu ujao; United tayari imemsajili winga wa Kimataifa wa Wales, Daniel James kutoka Swansea City… ✔🔜🔴.
#EPLTransfersUpdates
@Sokawaytz

Mchezaji wa Leicester City na Uingereza, Harry Maguire, anatarajiwa kuwa beki ghali zaidi duniani wiki hii

Mchezaji wa Leicester City na Uingereza, Harry Maguire, anatarajiwa kuwa beki ghali zaidi duniani wiki hii wakati atakapojiunga na Manchester City kwa dau la £80m baada ya kukataa kujiunga na Manchester United.
.
– Mlinzi huyo mahiri ameripotiwa kwamba kaipiga chini ofa ya @manchesterunited na yupo tayari kutua kwa majirani zao @mancity ambapo wamempa ahadi ya kuwa atapokea mshahara wa £280k kwa wiki… Ikiwa usajili utatimia basi atakuwa beki ghali Duniani Baada ya Uhamisho wa Virjil Van Dijk kutua @liverpoolfc akitokea @southamptonfc kwa £75m..
#PremierLeagueUpdates #EPLTransfersUpdates

#BURUDANI… Washindi wa Waliotangazwa katika tuzo za #BETAwards ni..

#BURUDANI… Washindi wa Waliotangazwa katika tuzo za #BETAwards ni..
⭕️Kundi Bora: Migos
⭕️HipHop Mwanaume: Nipsey Hussle
⭕️HipHop Mwanamke: Cardi B
⭕️Video Bora: Childish Gambino -This Is America
⭕️Msanii Chipukizi: Lil Baby
⭕️Muigizaji wa Kike: Regina King
⭕️Muigizaji wa Kiume: Michael Jordan
⭕️Filamu Bora: Blackkklansman
⭕️Mchezaji wa Kike: Serena Williams
⭕️Mchezaji wa Kiume: Stephen Curry
⭕️Mwongoza Video Bora: Karena Evans
⭕️Ushirikiano Bora: Travis Scott Ft. Drake-Sicko Mode
⭕️R&B/Pop Mwanaume: Bruno Mars
⭕️R&B/Pop Mwanamke: Beyoncé
⭕️Albamu Bora: Cardi B- Invasion Of Privacy.
#Updates #betawards

Colombia 🇨🇴 imeshinda kila Mchezo wao katika mechi zote tatu za Hatua ya Makundi ya Copa America,

Colombia 🇨🇴 imeshinda kila Mchezo wao katika mechi zote tatu za Hatua ya Makundi ya Copa America, Wameshinda dhidi ya Uruguay, Argentina na Qatar… Ni Kwa mara ya kwanza wanashinda mechi zote za Makundi tangu mwaka 2001, walipomaliza kwa kuwa Mabingwa… Wanafuzu kucheza Robo fainal ambapo wanamsubiri mpinzani wao atakaemaliza nafasi ya Pili kutoka Kundi C..
#CopaAmericaUpdates
@Sokawaytz

– Lionel Messi 🇦🇷 aweka rekodi Copa America,

– Lionel Messi 🇦🇷 amecheza michezo 24 ya Copa America, amekuwa mchezaji wa kumi katika orodha ya Wachezaji waliocheza michezo mingi katika historia ya mashindano… Messi amekuwa mechi sawa na Teodoro Fernández wa Peru na José Bustamante wa Bolivia… HAPPY BIRTHDAY @leomessi 👑🎂🎉
#CopaAmericaUpdates
@Sokawaytz

Sergio Agüero ni mchezaji wa tatu wa kufunga magoli 40 kwa timu ya Taifa ya Argentina…

– Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Argentina, Sergio Agüero ni mchezaji wa tatu wa kufunga magoli 40 kwa timu ya Taifa ya Argentina… Amefanya hivyo katika mechi yake ya 93 kuitumikia Argentina… Goli hilo Moja lililofanya atimize Magoli 40 alifunga jana katika mechi ya Copa America wakishinda 2-0 dhidi ya Qatar.
.
– Ni Goli lake La Nane kufunga ndani ya Michuano hii inayoendelea kwa muda wotee akiitumikia Argentina ikiwa yeye Mchezo wa jana kwake ni wa 17… Ni Wachezaji watatu tu wa timu ya Taifa ya Argentina wamefanikiwa kufunga Magoli 40+..
🇦🇷 Lionel Messi (68)
🇦🇷 Gabriel Batistuta (54)
🇦🇷 Sergio Agüero (40).
#CopaAmericaUpdates
@Sokawaytz

Design a site like this with WordPress.com
Get started