MFANYABIASHARA ADAIWA KUTEKWA JIJINI DAR –

MFANYABIASHARA ADAIWA KUTEKWA JIJINI DAR

Mfanyabiashara Raphael O. Ongangi anadaiwa kutekwa siku ya Jumatatu tarehe 24 Juni, 2019 na watu wenye silaha akiwa anaelekea nyumbani kwake maeneo ya Masaki

Mke wake aliyejulikana kwa jina la Veronica anaelezwa kutoa taarifa Polisi na kuujulisha Ubalozi wa Kenya kuhusu tukio hilo ambalo hadi sasa sababu yake haijajulikana

Balozi wa Kenya nchini, Dan Kazungu amethibitisha kupokea taarifa hiyo na amesema wanashirikiana na Polisi katika kushughulikia suala hilo na kuwa watatoa taarifa kila hatua itakayofikiwa

Aidha, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar, Lazaro Mambosasa amesema kuwa Jeshi la Polisi linachunguza tukio hilo

Ongangi anayeendesha biashara za kusafirisha mizigo katika maeneo ya Dar es Salam, DRC Congo, Zambia and Rwanda, alikuwa mshauri wa karibu wa ndugu Zitto Kabwe kabla ya Uchaguzi Mkuu 2015

SERIKALI YATOA MAPENDEKEZO YA KUBADILI SHERIA KWA TBS NA TFDA

SERIKALI YATOA MAPENDEKEZO YA KUBADILI SHERIA KWA TBS NA TFDA

Serikali imependekeza marekebisho ya sheria ya viwango sura 130 ili kuhamisha majukumu ya kusimamia masuala ya chakula na vipodozi kwa Shirika la Viwango Tanzania(Tanzania Bureau of Standards-TBS) kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa(Tanzania Food and Drugs Association-TFDA) ambayo inasimamia majukumu hayo kwa sasa

Kutokana na mapendekezo hayo, imependekezwa kuwa badala ya kuitwa TFDA iitwe Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba(TMDA)

Kufuatia pendekezo hili, TBS itachukua jukumu la kuunganisha utaratibu wa usajili wa majengo, bidhaa, udhibiti wa bidhaa na udhibiti wa bidhaa kutoka nje

Hayo yameelezwa leo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji wakati akiwasilisha bungeni muswada wa sheria ya fedha mwaka 2019

Takwimu za Wachezaji katika Mechi za Mazunguko wa kwanza wa hatua ya Makundi ya Kombe La Mataifa ya Afrika “AFCON”.

– Takwimu za Wachezaji katika Mechi za Mazunguko wa kwanza wa hatua ya Makundi ya Kombe La Mataifa ya Afrika “AFCON”… Mlinda lango wa @taifastars_, Aishi Manula ndiye kipa Pekee aliye okoa Michomo mingi zaidi ya Makipa wote.
#AFCONUpdates

NAPOLI KUITAFUTA SA8NI YA JAMES RODRIGUES

– Klabu ya Napoli huenda ikaanza kuitumia jezi nambari 10 ya aliyekuwa nyota wa Argentina Diego Maradona wakijaribu kumshawishi mshambuliaji wa Real Madrid na Colombia James Rodriguez kujiunga na timu hiyo; James amekuwa hafahamu wapi atacheza msimu ujao ujao kwa mkopo wake ndani ya @fcbayern umemalizika na Hana nafasi ndani ya Real Madrid…. Majogoo Liverpool nao wanatajwa kumwanja Nyota huyo..
#TransferNewsUpdates

CLATOUS CHAMA ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI KATIKA KLABU YA SIMBA

#Repost from @simbasctanzania
Mfungaji wa magoli ya mwisho ambayo yalitupeleka kwenye hatua ya makundi na robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Clatous Chota Chama (Triple C) bado yupo sana Msimbazi. Mwamba wa Lusaka ataendelea kuwa sehemu ya kikosi cha Mabingwa baada ya kusaini mkataba mpya wa miaka miwili. #nguvumoja
#TPLTransferUpdates

Design a site like this with WordPress.com
Get started