BODI YA LIGI YAWAPA ONYO WAAMUZI WATATU

Bodi ya ligi (TPLB) imetoa onyo kwa waamuzi watatu kutokana na kushindwa kufuata sheria 17 za mpira wa miguu katika mechi walizo chezesha.

Mwamuzi Florentina Zablon aliyechezesha mchezo namba 17 kati ya Mbeya City dhidi ya Yanga katika uwanja wa Sokoine amepewa onyo kali kutokana na kushindwa kutafsiri sheria licha ya uwanja kujaa maji kutokana na mvua kubwa kunyesha jijini Mbeya.

Mwamuzi Jonesi Rukya na msaidizi wake Soud Lilla nao wamepewa onyo kali baada ya kushindwa kuona baadhi ya matukio katika mchezo kati ya Simba dhidi ya Yanga uliopigwa uwanja wa Taifa, Januari 4.

Maamuzi hayo yametangazwa mbele ya vyombo vya habari na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya ligi, Ibrahim Mwanyela katika ofisi za Shirikisho la soka Tanzania (TFF) zilizopo Karume, Dar es Salaam.

@tanfootball @tplboard

#wapendasokaupdates

DAKIKA 90 SIMBA VS NAMUNGO

.
Inaandikwa na @danirito_thomson
.
Simba iliendelea na 4-2-3-1na Namungo walicheza 4-3-3 pia 4-1-4-1
.
Namungo walicheza open football, hawakukaa nyuma kama timu nyingi zikicheza na Simba, walitupa soka zuri
.
Namungo walinza na goal kick fupi kwa beki za kati wakati mabeki wa pembeni wanarikaribia eneo la kati na kuwafanya Simba kuto kupress juu, holding midfielder anaungana na mabeki wa kati na wanatoka kwa pasi fupi ila kabla ya kuvuka nusu ya uwanja walicheza sana long balls
.
Walipiga long balls kwenye half space katikati ya Nyoni na Zimbwe nadhani wameelewa wana faida ya ganzi ya miguu ya Nyoni ambae amekuwa sio mwenye kasi sana
.
Bao la pili la Namungo, mpira mrefu ulipigwa kwenye pembe ya box katikati ya Kapombe na Wawa (half space), na ikagongwa kichwa mpira ukaangukia eneo ambalo ni uzembe ukiwa na viungo wawili wakabaji wote kutokuwepo, Shiboub na Mkude wote walikua likizo, second ball ikatua kwa Kikoti, bang what a screamer 2-2
.
Dilunga amekuwa na faida sana kimfumo, lile goli alidrible kutoka nafasi ya winga akaenda kushoot eneo la namba10, vyote si anaweza bana na anakupa katika ubora uleule ang’avu wa HD, amerudia alichofanya dhidi ya Mbao
.
Siri ya Sven kimbinu kwa wing zake mbili, Kahata anakua ndani ya box mpira ukiwa winga ya kulia, Dilunga anaingia mpira ndani ya box na kupiga low cross maji marefu muachie Kapombe, Dilunga kama mpira upo winga ya Kahata anasimama kama namba10, Kagere anakaa post ya chini tayari kwa krosi ndefu
.
Kahata kile kichwa uwa anapiga mwanangu Chicharito, pure pocher
.
Mkude aliendelea kuwa bora sana akiwa na mpira, aliachia kwa wakati sahihi
.
Rotation ya Chama na Ajibu, kama beki ama kiungo mkabaji hii sub inakupa wakati mgumu, jana walicheza vizuri sana
.
John Bocco alibadilisha sura ya timu, huyu ndie aliwapa wakati mgumu Namungo japo kwa muda mfupi
.
Simba wana tatizo kuwa sehemu sahihi wakati wa kukaba, hii si sawa
.
Kapombe alikuwa katika kiwango bora sana, anamwaga maji sana huyu kiumbe kama SIMTANK bovu
.
Goli la Kagere ni clear offside, uzembe waamuzi unawapa lawama mbaya TFF na kuna muda unaweza sema hizi Simba na Yanga zinahonga kumbe ni uzembe wao binafsi
.
#sokaplaceUPDATES

Kamata Ratiba Ya Soka Leo

:
👉Vodacom Premier League
16:00 Azam Fc vs Mtibwa Sugar
:
👉Spain – Copa del Rey
21:00 Barcelona vs Leganes
23:00 Mirandes vs Sevilla
:
👉France – Cup
22:55 Nice vs Lyon
:
👉International – Club Friendlies
15:00 Ull/Kisa vs Vaalerenga
16:00 Austria Wien vs Zemplin Michalovce
16:00 FC Midtjylland vw Fredericia
17:00 Altach vs Ruzomberok
19:30 Austria Wien vs SC Dnipro-1
23:00 Nashville SC vs Elfsborg
:
👉Egypt – Premier League
18:00 Ismaily SC vs El Entag El Harby
20:30 Al-Ittihad Al-Sakandary vs Smouha SC
:
Prepared by @officialchristz
#SokaplaceUPDATES
@danirito_thomson

Kamata Matokeo Ya Soka Jana

:
👉VodacomPrimierLeague 🇹🇿
FT Simba Sc 3-2 Namungo Fc
FT Polisi Tz 1-0 Tz Prisons
:
👉England – Premier League
FT West Ham United 0 – 2 Liverpool
:
👉England – EFL Cup
FT Manchester City 0 – 1 Manchester United
:
👉Spain – Copa del Rey
FT Leonesa 0 – 0 Valencia
P (2-4)
FT Rayo Vallecano 0 – 2 Villarreal
FT CD Badajoz 2 – 3 Granada
FT Real Sociedad 3 – 1 Osasuna
FT Real Zaragoza 0 – 4 Real Madrid
:
👉Italy – Coppa Italia
FT Inter 2 – 1 Fiorentina
:
👉France – Cup
FT Epinal 2 – 1 Lille
FT Pau 0 – 2 Paris Saint-Germain
FT Marseille 3 – 1 Strasbourg
:
👉Belgium – First Division A
FT Sporting Charleroi 0 – 0 Club Brugge
:
👉Egypt – Premier League
FT Al Masry 1 – 2 El Gounah
FT FC Masr 1 – 2 Pyramids FC
:
👉Kenya – Premier League
FT Zoo FC 2 – 2 Mathare United
FT Gor Mahia 2 – 1 Sofapaka
:
👉Tunisia – Ligue I
FT Sportif de Chebba 1 – 2 Esperance
:
Prepared by @officialchristz
#SokaplaceUPDATES
@danirito_thomson

YANGA YAPELEKA MALALAMIKO BODI YA LIGI JUU YA FAINI WALIZOPIGWA

Uongozi wa klabu ya Yanga umepeleka malalamiko Bodi ya ligi (TPLB) juu ya faini walizopewa katika mechi zao zilizochezwa mwezi uliopita kutokana na kutoridhishwa na jinsi hatua hizo zilivyo chukuliwa dhidi yao.

Ofisa habari wa klabu hiyo, Hassan Bumbuli amesema kuhusu kupigwa faini ya shilingi laki tano kutokana na kuto wasilisha majina ya wachezaji katika kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting) katika mchezo dhidi ya Tanzania Prisons msemaji huyo amebainisha kuwa walipeleka kwa kuchelewa kwakua mechi ilihamishwa ghafla kutoka uwanja Sokoine kwenda Samora, Iringa baada ya kutokuwa tayari kuchezewa baada ya mvua kunyesha.

Kuhusu faini ya shilingi laki mbili kwa kutoingia kwenye vyumba rasmi katika mchezo dhidi ya Simba msemaji huyo alisema walipeleka malalamiko Bodi ya ligi kuwa vyumba vyao havikuwa salama na wakaruhusiwa kuingia katika vyumba vya timu B lakini wameshangaa kuona wamepigwa faini hiyo.

Pia kuhusu mashabiki wao kurusha chupa za maji katika mchezo huo ni kutokana na wao kupeleka malalamiko Bodi ya juu ya mambo mbalimbali ambayo wanaona wanaonewa.

Bumbuli ameongeza kuwa wanashangaa Bodi hiyo kuzuia pesa kutoka kwa mdhamini Vodacom bila kufanya majadiliano na klabu hiyo kitu ambacho ni kinyume na kanuni ambazo wameziweka wenyewe.

@yangasc @tanfootball @tplboard

#wapendasokaupdates

kocha mkuu wa Asto villa Dean Smithn aweka rekodi mpya jana

1 – Dean Smith kocha mkuu wa Aston villa anakuwa meneja wa kwanza wa Kiingereza kufikia fainali ya Kombe la Ligi tangu Phil Parkinson akiiongoza Bradford City mnamo 2012-13:
:
🙌 Wakati huo huo, Dean ni Mwingereza wa kwanza kufika fainali ya Michuano hiyo akiwa na Klabu ya Premier League tangu Harry Redknapp alipo iongoza Tottenham mnamo 2008-09..
#CarabaoCup #ASTLEI
@Harunlugoyah

#dailysporttz

Design a site like this with WordPress.com
Get started