‘Taifa Stars’ kumkosa kiungo wake mahiri, Mudathir Yahya kwenye mchezo wa mwisho wa kundi C dhidi ya Algeria,

– Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kitamkosa kiungo wake mahiri, Mudathir Yahya Abbas kwenye mchezo wa mwisho wa kundi C dhidi ya Algeria, Julai Mosi kutokana na kiungo huyo kutumikia adhabu ya kadi mbili za njano.
.
– Kadi ya njano ambayo Mudathir alipata mnamo dakika ya 49 kwenye mechi ya jana dhidi ya Kenya ni ya pili kwake baada ya kupata nyingine mchezo dhidi ya Senegal jambo ambalo kikanuni linamlazimisha kutumikia adhabu ya kukosa mchezo mmoja unaofuata, ambao ni dhidi ya Algeria ambao @taifastars_ itakuwa inakamilisha ratiba ya Michuano ya AFCON.
#AFCONUpdates

Beki Tairone Santos da Silva (30) amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba Sc akitokea Atlético Cearense FC ya nchini kwao Brazil.

#

DealDone Beki Tairone Santos da Silva (30) amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba Sc akitokea Atlético Cearense FC ya nchini kwao Brazil.

BUNGENI: , Bunge la Tanzania lilipitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Namba 3)

BUNGENI: Jana, Bunge la Tanzania lilipitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Namba 3) wa 2019 unaogusa sheria takribani 8 ikiwemo Sheria ya Asasi za Kiraia, Makampuni na Vyama vya Kijamii

Serikali imekubali kufanya marekebisho kadhaa ikiwemo kuweka utaratibu wa kujisajili kwa Makampuni na Asasi za Kiraia zitakazoshindwa kuhamisha usajili kutoka kuwa Makampuni yenye hisa au ya dhamana kwenda Asasi za Kiraia ndani ya miezi miwili iliyotolewa na Sheria

Kufanya mabadiliko kuruhusu Taasisi za Imani/za kueneza Imani kuendelea kusajiliwa na kuratibiwa na Sheria ya Vyama vya Kijamii na kufanyia mabadiliko kifungu namba 25 cha Sheria ya Asasi za Kiraia ambayo inafafanua maana ya Asasi ya Kiraia ili kukidhi wigo wa Asasi zilizopo

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walihoji kuhusu uhalali wa sheria hiyo kupitishwa haraka kwa hati ya dharura bila kutoa muda wa kutosha kwa wadau kuupitia na mapendekezo yao kufanyiwa kazi

Mbunge Salome Makamba alisema kumekuwa na desturi ya Bunge kutunga sheria zisizotekelezeka na hivyo kurudishwa Bungeni katika kipindi kifupi ili kufanyiwa marekebisho

Naye Zitto Kabwe alisema yeye anafahamu marekebisho hayo yameletwa kwasababu Serikali inahangaika na Kampuni ya Acacia. Ameitaka Serikali kwenda kupambana na kampuni hiyo kwa utaratibu wa kiutawala badala ya kuharibu nchi kwa ugomvi wa kampuni moja

ACACIA YAKATAA KUUZA HISA ZAKE KWA BARRICK

ACACIA YAKATAA KUUZA HISA ZAKE KWA BARRICK

Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Acacia imekataa dau la Mwanahisa wake mkuu, Barrick Gold kwa madai kuwa bei tajwa haiakisi thamani yake halisi

Barrick ambayo inamiliki asilimia 63.9 ya Acacia ilipendekeza kuinunua Acacia kwa mfumo wa hisa kwa hisa ambapo kwa kila hisa moja ya Acacia watatoa hisa 0.153 ya Barrick

Hii ni moja ya hatua katika juhudi za kusuluhisha mgogoro kati ya Acacia na Serikali ya Tanzania. Barrick imesema Acacia ina thamani ya dola za kimarekani milioni 979 kutoka Dola za kimarekani milioni 787 ilizopendekeza Mei, 2019 kutokana na hisa za Barrick kuongezeka kwa asilimia 27.

Acacia imekataa bei hiyo ikiituhumu Barrick kuchochea kuni kwenye mgogoro wake na Tanzania ili iinunue kwa bei ya kutupwa

Design a site like this with WordPress.com
Get started