

OFFICIAL | Mshambuliaji wa Kimataifa wa DR Congo, Deo Kanda Á Mukok amewasili nchini tayari kujiunga na Klabu ya Simba SC kwa mkopo Akitokea Miamba wa Soka kutoka Lubumbashi, DR Congo Klabu ya TP Mazembe.
.
– Mukok 29; Ambaye ni Bingwa wa Afrika Mara Moja 2010, Pia kawahi kucheza Kombe La Dunia kwa Vilabu akiwa na TP Mazembe na Raja Club Casablanca ya Morocco, anatarajia kukipiga kwa mkopo ndani ya Mabingwa wa Tanzania kuanzia msimu ujao.
.
– Mukok Alianza Rasmi kuitumikia Mazembe mwaka 2009 baada ya kutimka DC Motema Pembe, Alicheza mpaka 2013 na kwenda kufanya majaribio ndani ya Klabu ya Al Ahly ya Misri lakini dili lilifeli na kutua Raja Casablanca ya Morocco kwa Mkataba wa miaka mitatu lakini alicheza msimu mmoja na kurejea DRC katika Klabu ya AS Vita Club alicheza msimu mmoja na kutimkia AEL FC (Athilitiki Enosi Larissa) ya Ugiriki msimu mmoja nako akatimka… February mpaka Novemba 2015 hakuwa na timu Baada ya kutoka Ugiriki, kisha akatua tena TP Mazembe na kutolewa kwa mkopo January 2016 kwenda 4 De Abril FC ya Angola, Oktoba 2016 akarejea na mpaka Sasa anatua @simbasctanzania.
#TPLTransferUpdates
@sokawaytz_