

Beki wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Agrey Moris, anatarajia kuwa nje dimba kwa muda wa miezi miwili ijayo baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti nchini Misri juzi.
Moris aliumia kwenye mchezo wa kirafiki wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ dhidi ya Misri wakati ikijiandaa na michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) inayoendelea kutimua vumbi nchini Misri.
Kwa mujibu wa ripoti ya Daktari wa Azam FC, Dr. Mwanandi Mwankemwa, aliyewasili nchini misri kushugulikia matibabu yake inaeleza kuwa, beki huyo kisiki alikuwa na uvimbe kwenye kisahani kidogo juu ya goti (patella) na kuchanika kidogo kwa mtulinga wa pembeni wa goti lake..
#TPLUpdates

















