









Magazeti ya #Tanzania leo July 4, 2019










Magazeti ya #Tanzania leo July 4, 2019



MKE WA MTAWALA WA DUBAI AKIMBILIA UINGEREZA NA KUOMBA HIFADHI YA UKIMBIZI
–
Haya bint Hussein ambaye ni Mtoto wa aliyekuwa Mfalme wa Jordan, ametoroka nchini humo pamoja na Watoto wake wawili na kukimbilia nchini Uingereza akimtuhumu mumewe kumnyanyasa
–
Haya ni Mke wa Sheikh Mohammed bin Rashid al-Maktoum ambaye ni mtawala wa Dubai na Waziri Mkuu wa Muungano wa Falme za Kiarabu(UAE)
–
Taarifa zinaeleza kuwa Haya ametoroka kwa msaada wa Mwanadiplomasia wa Ujerumani na kwa sasa yuko kwenye jumba la kifahari huko Kensington, England
–
Mbali na kuomba hifadhi kama mkimbizi Haya pia amefungua kesi nchini Uingereza akiishtaki Familia ya Kifalme ya mumewe
–
Mgogoro kati ya Haya na Mumewe ulidhihirika hivi karibuni baada ya Haya kuweka shairi katika akaunti yake ya Instagram shairi ambalo lililomchukiza mumewe


– Wachezaji wapya wa Kimataifa wa Yanga SC wanatarajiwa kuwasili nchini Ijumaa tayari kwa maandalaiizi ya Wiki ya Wananchi itakayofikia kilele Julai 27… Mwenyekiti wa Yanga, Dk Mshindo Msolla alisema wachezaji hao watawasili Julai 5 na Julai 7 watakwenda Mkoani Morogoro kambini.
:
— “Tayari tumekwisha watumia tiketi wachezaji wote na wote watawasili nchini Julai 5,” alisema Msolla.
.
– Akizungumzia maandalzi ya wiki ya Wananchi, Msolla alisema sherehe zitaanza Julai 21 ambapo mashabiki na wanachama wa Yanga watafanya kazi mbalimbali za kijamii kabla ya kilele Julai 27.
—- “Tutatembelea na kutoa misaada katika vituo vya watoto Yatima, kuchangia damu na kufanya usafi katika maeneo mbalimbali nchini,” alisema Msolla.
:
– Wachezaji Wakimataifa wa Yanga SC ni mabeki, Lamine Moro (Ghana) na Mustapha Seleman (Burundi). Washambuliaji, Sadney Ukhob (Namibia), Issa Bigirimana (Burundi), Patrick Sibomana (Rwanda), Juma Balinya (Uganda) na Kalengo Maybin (Zambia).
#TPLUpdates
#TPLTransferUpdates


OFFICIAL | Shirikisho La Soka Barani Afrika, @caf_online limetangaza Kikosi Bora cha hatua ya Makundi ya Fainali za Mataifa ya Afrika 2019.. Hatua ya Makundi ya Michuano hii imehitimishwa siku ya jana na Siku ya Ijumaa ya wiki hii hatua ya 16 bora itaanza kutimua vumbi..
#AFCONUpdates #TotalAFCON2019


Angel Di Maria amefikisha mechi 100 akiwa na timu ya Taifa ya Argentina. Swali : Amefunga mabao mangapi na pasi za mabao ngapi mpaka sasa? #BRAxARG #Argentina #Brazil #DaniAlves #Messi #ArgentinavsBrazil #BrazilvsArgentina #CopaAmerica2019 #CopaAmerica #DiMaria #Otamendi #Firmino #Coutinho #Aguero #VamosArgentina #alissonbecker


#DealDone Klabu ya Kagera Sugar imefanikiwa kuinasa saini ya Frank Ikobela kutoka Mbeya City.


#DealDone Aliyekuwa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar Kelvin Sabato “Kiduku” amejiunga na Gwambina Fc inayoshiriki Ligi daraja la kwanza Tanzania FDL kwa mkataba wa mwaka mmoja.
.
.
Nyota wengine ni Ibrahim Job kutoka Lipuli Fc pamoja Raizin Hafidh akitokea Coastal Union wote wakisaini mwaka mmoja.


MUSIBA APEWA SIKU 7 KUWASILISHA MAJIBU KUHUSU MADAI YA MEMBE
–
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imempa siku 7 mmiliki, Cyprian Musiba na wachapishaji wa gazeti la Tanzanite wawe wamewasilisha majibu dhidi ya madai ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe anayetaka kulipwa Tsh bilioni 10 kwa kuchafuliwa
–
Uamuzi huo umetolewa leo, mbele ya Jaji Joaquine Demelo baada ya kupitia maombi ya wajibu maombi ya kutaka waongezewe muda wa kuwasilisha utetezi na majibu kinzani
–
Jaji Demelo amesema wajibu maombi walitakiwa kuwasilisha utetezi na majibu kinzani ndani ya siku 21 baada ya shauri kufunguliwa Desemba mwaka jana lakini hawakufanya hivyo ambapo Musiba kupitia Wakili wake Majura Magafu waliomba kuongezewa muda japo wadai walipinga maombi hayo wakitaka yasikubaliwe


KENYA: MWANAHABARI ZA MTANDAONI ALIYETUHUMIWA KUSHIRIKIANA NA AL-SHABAAB AACHIWA KWA DHAMANA
–
Robert Alai Onyango alieshtakiwa kwa makosa mawili likiwemo la kuvujisha siri kwa nia ya kuwasaidia Wanamgambo wa Al-Shabaab na kuvuruga uchunguzi wa Polisi
–
Alai Onyango amekana tuhuma hizo dhidi yake na kuachiwa kwa dhamana iliyohusisha kiasi cha Shilingi za Kitanzania 11,163,165
–
Anatuhumiwa kwa kufanya makosa hayo mnamo Juni 17, 2019 ambapo ndani ya siku hiyo inaelezwa kuwa aliweka picha ya Askari Polisi aliyefariki kupitia mtandao wa WhatsApp
–
Aidha, inaelezwa kuwa aliweka picha hiyo kupitia akaunti yake ya Twitter kitendo kinachoelezwa ni kuharibu Uchunguzi wa Vyombo vya Dola
–
Kesi hii imeahirishwa hadi Julai 16, 2019


RAIS KENYATTA AKERWA NA KAULI YA ‘JAGUAR’, AMTUMIA UJUMBE RAIS MAGUFULI
–
Ujumbe huo wa Rais wa Kenya, umeelezea msimamo wa Serikali yake kuhusu kukerwa na matamshi ya Mbunge jimbo la Starehe, Charles Njagua Kanyi maarufu kwa jina la Jaguar
–
Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki alitoa kauli iliyowalenga raia wa nje(wakiwemo Watanzania) wanaofanya biashara nchini Kenya akiwataka waondoke la si hivyo ataamuru Wananchi wawapige
–
Alidai kuwa wafanyabiashara kutoka nje akizitaja nchi za Tanzania na Uganda kuwa wamekuwa wakichukua fursa za biashara katika eneo lake
–
Kufuatia kauli hiyo, Serikali ya Kenya kwa nyakati kadhaa ilieleza kuwa kauli hiyo si msimamo wake na baadaye vyombo vya usalama vilimkamata Mbunge huyo
–
Aidha, ujumbe wa Rais Kenyatta umewasilishwa leo (Jumanne, Julai 02, 2019) na Balozi wa Kenya nchini, Dany Kazungu na kupokelewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais Magufuli