CECAFAKagameCup – Mpaka muda huu, Jijini Kigali nchini Rwanda, zimewasili timu Saba (7) tayari kwa mshike mshike wa Michuano ya CECAFA Kagame Cup 2019.

#

CECAFAKagameCup
– Mpaka muda huu, Jijini Kigali nchini Rwanda, zimewasili timu Saba (7) tayari kwa mshike mshike wa Michuano ya CECAFA Kagame Cup 2019. Timu zilizowasili ni Green Eagles, Proline FC, KMC FC, Atlabara, Azam FC, KCCA na AS Ports… Timu zote hizo zimetua kwa usafiri wa ndege, isipokuwa Mabingwa wa Uganda, Klabu ya KCCA FC ambayo imewasili kwa usafiri wa Gari (Bus).
:
– Kwa Taarifa ni kwamba Klabu ya DC Motema Pembe ya Kinshasa, DR Congo imeondoshwa katika Michuano hii ya CECAFA Kagame Cup 2019, tayari CECAFA imetuma mualiko kwa Klabu nyingine ya nchini humo ya AS Maniema Union kutoka mjini Kindu Kama mbadala wa Klabu hiyo iliyoondolewa..
#CECAFAKagameCup
@Sokawaytz_

VIONGOZI 3 WATUHUMIWA KUTAFUNA FEDHA ZA MAUZO YA DHAHABU –

VIONGOZI 3 WATUHUMIWA KUTAFUNA FEDHA ZA MAUZO YA DHAHABU

Viongozi wa kikundi cha wachimbaji dhahabu cha Winima Group kilichopo katika mgodi wa Kitunda Wilayani Sikonge wako hatiani kukamatwa kwa tuhuma za kutafuna Tsh milioni 342 za mauzo ya kilo 1.549 za dhahabu

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Shabani Seifu amesema Machi 27, 2019 watuhumiwa hao walikwenda Wilayani Nzega kwa ajili ya kufanya mauzo ya kilo 1.5 za dhahabu zikiwa ni mali ya wanakikundi hao lakini baada ya kuuza dhahabu hiyo hawakukabidhi fedha za mauzo

Viongozi wanaotuhumiwa ni Mwenyekiti wa kikundi, Japhet Mbwilo, Katibu wa kikundi Godfrey Mwaniwiti na Meneja wao, Bazilio Bazilio

Wanakikundi hao wamemuomba Waziri wa Madini, Doto Biteko aingilie kati ili waweze kupata haki yao na Jeshi la Polisi lisaidie kukamatwa wahusika na kufikishwa katika vyombo vya sheria

TAKWIMU KIWANGO CHA UMASIKINI: MKOA WA RUKWA WAONGOZA

TAKWIMU KIWANGO CHA UMASIKINI: MKOA WA RUKWA WAONGOZA

Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema mikoa inayoongoza kwa wananchi wake kuwa masikini Tanzania bara kwa mwaka 2017/2018 ni mkoa wa Rukwa kwa 45%, Simiyu 39.2%, Geita 37.5%, Lindi 36% na Kigoma 34.5%

Kwa mujibu wa Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi 2017/18 umasikini wa mahitaji ya msingi umepungua kutoka asilimia 28.2 mwaka 2011/12 hadi asilimia 26.4 mwaka 2017/18

Matokeo ya Utafiti yanaonesha kuwa umasikini wa mahitaji ya msingi ni mkubwa kwa maeneo ya vijijini kwa 31.3% ikilinganishwa na maeneo ya mijini kwa 15.8%

Aidha, matokeo ya Utafiti huo yanaonesha kuwa mkoa wa Dar es Salaam una kiwango kidogo cha umasikini wa mahitaji ya msingi cha asilimia 8.0

Kwa upande mwingine, kiwango cha umasikini wa chakula kimepungua kutoka asilimia 9.7 mwaka 2011/12 na kufikia asilimia 8.0 mwaka 2017/18

Umasikini wa chakula ni mkubwa maeneo ya vijijini kwa asilimia 9.7 ikilinganishwa na maeneo ya mijini asilimia 4.4
Mgawanyo wa Watu Maskini

Mgawanyo wa watu masikini Tanzania Bara kwa kuzingatia umasikini wa mahitaji ya msingi unaonesha kuwa asilimia 81 ya watu masikini wanaishi maeneo ya vijijini ikilinganishwa na asilimia 84.1 mwaka 2011/12

ENGLAND: FRANK LAMPARD KOCHA MPYA WA CHELSEA FC

ENGLAND: FRANK LAMPARD KOCHA MPYA WA CHELSEA FC

Frank Lampard ambaye ni miongoni mwa Wachezaji waliowahi kuichezea Klabu hiyo kwa mafanikio makubwa ametangazwa rasmi kuwa kocha mpya baada ya tetesi za muda mrefu

Chelsea FC imemteua Lampard baada ya aliyekuwa kocha wake, Mauruzio Sarri kutimkia katika Klabu ya Juventus akiwa ameifundisha Chelsea FC kwa msimu mmoja

Lampard baada ya kustaafu soka alianza kazi ya ukocha katika timu ya Derby County aliyodumu nayo kwa msimu mmoja

UN: SHAMBULIO LA WAHAMIAJI LIBYA LAWEZA KUWA NI UHALIFU WA KIVITA

UN: SHAMBULIO LA WAHAMIAJI LIBYA LAWEZA KUWA NI UHALIFU WA KIVITA

Afisa wa Umoja wa Mataifa amesema, shambulio lililofanywa dhidi ya kituo cha kuwahifadhi wahamiaji nje ya mji wa Libya na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 44 linaweza kuwa ni uhalifu wa kivita

Karibu watu 130 walijeruhiwa katika shambulio hilo ambalo Serikali ya Libya inadai lilitekelezwa na vikosi vya Jenerali Khalifa Haftar huku vikosi vya Jenerali Haftar vikiilaumu Serikali kwa kushambulia kituo hicho

Wengi wa waliouawa wanaaminiwa kuwa watu wa asili ya Kiafrika kutoka eneo la jangwa la Sahara ambao wamekuwa wakijaribu kuingia Ulaya kupitia Libya na hii ni mara ya pili kwa kituo hicho kushambuliwa

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres ameelezea kusikitishwa kwake na ripoti hiyo na kuomba kufanywe uchunguzi huru ili kuhakikisha waathiriwa wanapata haki

NDUGU WA WALIOFARIKI KWENYE AJALI ZA NDEGE YA BOEING 737 MAX KULIPWA FIDIA

NDUGU WA WALIOFARIKI KWENYE AJALI ZA NDEGE YA BOEING 737 MAX KULIPWA FIDIA

Kampuni ya Boeing imetenga kiasi cha zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 230 kwa ajili ya kuwalipa fidia waliopoteza ndugu zao katika ajali za ndege aina ya Boeing 737 Max

Fidia hiyo imepangwa kulipwa kwa familia 346 za watu waliopoteza ndugu zao katika ajali za Ndege ya aina hiyo iliyotokea nchini Indonesia Oktoba 2018 na ajali iliyotokea Ethiopia Machi 2019

Kampuni hiyo ya Seattle nchini Marekani imepanga kushirikiana na Asasi za Kiraia katika nchi husika ili kufanikisha zoezi hilo la fidia

Hatua hii ni baada ya watu wengi waliofiwa na ndugu zao kufungua kesi wakiishtaki kampuni hiyo kufuatia vifo vya ndugu zao

M

NIGERIA: LORI LA MAFUTA LALIPUKA, WATU 35 WAPOTEZA MAISHA

NIGERIA: LORI LA MAFUTA LALIPUKA, WATU 35 WAPOTEZA MAISHA

Watu 35 wamefariki na wengine 101 kujeruhiwa baada ya lori ya mafuta ya Petroli kulipuka Kusini mwa Nigeria katika kijiji cha Ahumbe katika jimbo la Benue

Janga hilo lilitokea jana baada ya lori hilo kupoteza uelekeo na kuanguka kabla ya kushika moto huku watu kadhaa wakijaribu kuchota mafuta yaliyokuwa yakivuja

Watu hao waliendelea kuchota mafuta hadi wakati basi aina ya Toyota lilipogonga lori hilo na kusababisha mlipuko wa kwanza ambapo watu 14 waliokuwa kwenye basi hilo walifariki papo hapo

Mlipuko wa pili ambao ulisababisha vifo vingi ulitokea dakika chache baadaye

Klabu ya Juventus ipo tayari kuwapa Manchester Utd kiasi cha €70m pamoja na mshambuliaji wake Paulo Dybala kama chambo ya kumpata kiungo wa kati Paul Pogba.

Klabu ya Juventus ipo tayari kuwapa Manchester Utd kiasi cha €70m pamoja na mshambuliaji wake Paulo Dybala kama chambo ya kumpata kiungo wa kati Paul Pogba.
.
.
Licha ya ofa hiyo bado mabosi wa Utd wanataka dau la €150m ili kumuachia (Star)

KMC FC imemsajili kiungo Mkabaji wa Kimataifa wa DR Congo, Melly Sivirwa. Kiungo amesajiliwa kutoka Klabu ya Vital’O

– KMC FC imemsajili kiungo Mkabaji wa Kimataifa wa DR Congo, Melly Sivirwa. Kiungo amesajiliwa kutoka Klabu ya Vital’O ya Burundi kwa kandarasi ya miaka miwili..
#TPLTransferUpdates

MATOKEO YA SOKA JANA JUMATANO NA RATIBA YA HII LEO: :

– Copa America – Semi-Final.
FT Chile 0 – 3 Peru
.
– World Cup Women – Semi-Final.
AET Netherlands 1 – 0 Sweden
.
– International – Club Friendlies.
FT Bregel Sport 1 – 10 Genk
FT OB 1 – 1 Holstein Kiel
FT Silkeborg 3 – 0 Vendsyssel FF
FT Lyngby 1 – 0 FC Helsingoer
FT Jong FC Utrecht 2 – 4 FC Nordsjaelland
FT Standard Liege 1 – 1 SoenderjyskE
FT Livingston 0 – 1 Paksi SE
FT Vitesse 3 – 4 FC Midtjylland
FT Basel 4 – 0 1. FC Nürnberg
FT CSKA Moscow 1 – 2 FC Rostov
FT FC Stade Lausanne-Ouchy 2 – 0 Servette
FT ND Triglav 2 – 2 FC Krasnodar
FT Slovan Bratislava 2 – 0 SKN St. Poelten
FT Gyori ETO 0 – 3 Spartak Moscow
FT Admira Moedling 4 – 1 ASK-BSC Bruck/Leitha
FT Heracles 0 – 1 Club Brugge
FT Salzburg 0 – 1 PFC CSKA-Sofia
FT AZ Alkmaar 1 – 0 PAOK Thessaloniki FC
FT Cercle Brugge 2 – 3 Zulte Waregem
FT Dinamo Bucuresti 3 – 0 Kilmarnock
FT Fortuna Sittard 5 – 1 Aris Thessaloniki
FT Luzern 3 – 0 Aarau
FT MSV 19 0 – 9 FC Utrecht
FT Sion 0 – 0 PSV Eindhoven
FT Strasbourg 2 – 1 FC Zuerich
FT KSK Heist 0 – 0 KV Mechelen
FT Svelta Melsele 0 – 7 Waasland-Beveren
FT UR La Louviere Centre 0 – 2 Sporting Charleroi
FT Glentoran 1 – 1 St. Johnstone
FT Arbroath 3 – 2 Hibernian
FT Stalybridge 0 – 5 Barnsley
FT Peterhead 0 – 2 Aberdeen
:
RATIBA YA HII LEO ALHAMISI.
Europa League – Qualification:: Preliminary round.
20:30 Cardiff Met University
FC Progres Niedercorn
20:30 UE Engordany
La Fiorita Montegiardino
21:00 NSI Runavik
Ballymena United
21:30 Europa FC
Sant Julia
21:45 Cliftonville
Barry Town
21:45 Tre Fiori
Klaksvik
.
– International – Club Friendlies
19:00 Spartak Moscow
FC Krasnodar
19:30 RSV Weyer
Fortuna Düsseldorf
19:45 DJK Bad Homburg
Eintracht Frankfurt
20:00 Charlton Athletic
Gaz Metan Medias
20:00 Rolder Boys
FC Emmen
21:30 Raith Rovers
Hamilton Academical
#fixtures #Updates
@Sokawaytz_

Design a site like this with WordPress.com
Get started