CHINA NA UINGEREZA ZAZOZANA KUHUSU MASUALA YA HONG KONG

CHINA NA UINGEREZA ZAZOZANA KUHUSU MASUALA YA HONG KONG

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Uingereza Jeremy Hunt, ameahidi kuendelea kuishinikiza China kuhusu njia za nguvu inazotumia dhidi ya waandamanaji mjini Hong Kong huku mzozo wa kidiplomasia ukiongezeka

Hunt amerejelea kuwa kutakuwa na athari iwapo China itakiuka makubaliano yalioafikiwa kuhusu haki mjini Hong Kong wakati Uingereza ilipoikabidhi udhibiti

Wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ya China imejibu kwa kumshtumu Hunt kwa kujiingiza katika nadharia za kikoloni

Balozi wa China nchini Uingereza, Liu Xiaoming alizungumza na waandishi wa habari na kuitaka Uingereza kukoma kuingilia masuala ya ndani ya Hong Kong

POLISI: TUNACHUNGUZA KUTEKWA KWA RAPHAEL NA KUKUTWA JIRANI NA NYUMBA YA SHANGAZI YAKE

POLISI: TUNACHUNGUZA KUTEKWA KWA RAPHAEL NA KUKUTWA JIRANI NA NYUMBA YA SHANGAZI YAKE

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema Jeshi la Polisi nchini kwa kushirikiana na Interpol nchini Kenya, linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini ni namna gani, Raphael Ongangi alitekwa na kufikishwa Mombasa

Wanaendelea na uchunguzi huo kwa kuwa hata taarifa zilizotolewa awali zilitolewa kwa mashaka, ambapo ameongeza kuwa miaka 2 iliyopita, mtoa taarifa ameshawahi kutoa taarifa za uzushi kwamba anataka kutekwa

Amesema “Haiwezekani mtekaji akuteke Tanzania akuchukue hadi Mombasa, tena karibu na nyumba ya shangazi yako! Bila shaka huyo mtu atakuwa anakupeleka nyumbani”

Amesema watakapohakikisha pengine taarifa hizi zilikuwa za kutengeneza mhusika naye atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria

Raphael Ongangi ambaye ni mfanyabiashara raia wa Kenya alitekwa Juni 24, na kupatikana Mombasa, karibu na nyumbani kwa shangazi yake Julai 2

DODOMA: WATATU WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUBAKA NA KULAWITI

DODOMA: WATATU WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUBAKA NA KULAWITI

Jeshi la Polisi linawashikilia watu watatu kwa makosa ya ulawiti na ubakaji wa watoto na wazee huku mtuhumiwa mmoja akiuawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kukutwa akimbaka mwanafunzi wa miaka nane

Kamanda Giless Muroto ametoa taarifa hiyo ambapo mojawapo ya matukio hayo manne yaliyotendeka kwa nyakati tofauti ni pamoja na kijana wa miaka 28 aliyemlawiti mama yake mzazi

Alimlawiti mama yake mzazi ambaye ana umri wa miaka 56 kwa kumvizia na chanzo kinaaminika kuwa ulevi au imani za kishirikina

MWALIMU ANUSURIKA KIFO AKITAKA KUJIUA KUTOKANA NA UGUMU WA MAISHA

MWALIMU ANUSURIKA KIFO AKITAKA KUJIUA KUTOKANA NA UGUMU WA MAISHA

Mwalimu wa Shule ya Msingi Rung’abure Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Godfrey Tarimo (35) amenusurika kifo baada ya kujikata shingo kwa chupa, huku ikidaiwa ni kwasababu ya ugumu wa maisha

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu amesema tukio hilo limetokea jana Jumatano Julai 3 na mwalimu huyo amelazwa katika hospitali teule ya Nyerere wilayani humo anakoendelea na matibabu

Mganga mkuu wa hospitali hiyo,Tanu Warioba amesema Tarimo alifikishwa hospitalini hapo akiwa anavuja damu lakini hakupata athari yoyote katika mfumo wake wa upumuaji

Kiungo wa Kimataifa wa Kenya Francis Kahata Amesaini Mkataba wa Miaka Miwili kuitumikia Klabu ya Simba SC. .

OFFICIAL | Haijalala!! Mara Moja Baada ya kuwasili Nchini jioni hii, Kiungo wa Kimataifa wa Kenya Francis Kahata Amesaini Mkataba wa Miaka Miwili kuitumikia Klabu ya Simba SC.
.
– Kahata mwenye umri wa Miaka 27; Ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kucheza eneo la kiungo, kwasasa akiwa sehemu ya wachezaji wanaounda kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya, msimu ujao atavaa jezi ya Mabingwa hao Tanzania Bara.
.
– Amejiunga Msimbazi akitokea Gor Mahia ya Kenya ambapo akiwa kwenye klabu hiyo alishinda Kombe la Ligi Kuu mara tatu, kiungo bora wa mwaka wa Ligi Kuu ya Kenya mara mbili na mchezaji bora wa msimu 2018/2019 wa Gor Mahia.
#TPLTransferUpdates

HISTORIA: FAHAMU KUHUSU ASILI YA KABILA LA WAKURYA –

HISTORIA: FAHAMU KUHUSU ASILI YA KABILA LA WAKURYA

Abakuria au Wakurya ni kabila la watu wanaoishi katika Wilaya ya Rorya, Tarime na Serengeti Mkoa wa Mara, Kaskazini mwa Tanzania, na katika Wilaya za Magharibi na Mashariki mwa Mkoa wa Nyanza katika sehemu ya Kenya

Mnamo mwaka 2005, idadi ya Wakurya ilikadiriwa kuwa 690,000, ikiwa ni 430,000 wanaoishi nchini Tanzania na 260,000 nchini Kenya na wote lugha yao ni Kikurya

Shuguli zao kubwa ni Kilimo na Ufugaji, huku Wakurya wa Kenya wakiegemea sana kwenye kilimo na Tanzania wakiegemea sana kwenye ufugaji

Kilimo cha asili walikuwa wanalima ulezi, mtama na viazi kwa ajili ya kutengeneza Togwa (obosara) na Pombe. Mazao mengine yalianza kulimwa miaka ya 1900 baada ya wajerumani kuhimiza kilimo

Wakurya hawapendi kutawaliwa wala kuonewa hivyo walikuwa na saiga lika ya vijana kwa ajili ya ulinzi na usalama hivyo utumwa haukuwaathiri sana. Ila kwa kupenda kwao vita walijiunga sana na jeshi K.A.R (King African Rifle) kupigana vita ya kwanza na ya pili na ya Uganda

Kwa Wakurya, Nyumba nthobhu ni mwanamke aliyezaa watoto wa kike tu na ili atakapokufa baadae nyumba yake isitoweke huamua kuoa binti wa kuendeleza uzao wa nyumba yake.
Nyumba mboke ni kama mwanamke hakuzaa kabisa, huyu huoa ili apate uzao

CHATO: RAIS MAGUFULI KUZINDUA HIFADHI YA BURIGI JULAI 9, 2019 –

CHATO: RAIS MAGUFULI KUZINDUA HIFADHI YA BURIGI JULAI 9, 2019

Hifadhi ya Taifa ya Burigi iliyopo Wilayani Chato Mkoani Geita itazindulia siku ya Jumanne baada ya kupandishwa hadhi hivi karibuni

Hapo awali hifadhi hiyo ilikuwa ikijulikana kama Pori la Akiba la Burigi. Siku hiyo Rais Magufuli atakabidhi vibali na hati kwa wawekezaji mbalimbali

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamis Kigwangala amesema hifadhi hiyo itafungua saketi ya Uhifadhi na Utalii Kaskazini-Magharibi mwa Tanzania badala ya ule wa Kaskazini pekee uliozoeleka

Ratiba ya Ligi Kuu nchini Hispania, @laliga msimu mpya wa 2019/20, Imetangazwa.. hizi ndio game za ufunguzi wa Ligi.

OFFICIAL: Ratiba ya Ligi Kuu nchini Hispania, @laliga msimu mpya wa 2019/20, Imetangazwa.. hizi ndio game za ufunguzi wa Ligi.

Celta Vigo vs. Real Madrid
Mallorca vs. Eibar
Atletico Madrid vs. Getafe
Espanyol vs. Sevilla
Alaves vs. Levante
Valencia vs. Real Sociedad
Real Betis vs. Real Valladolid
Leganes vs. Osasuna
Bilbao vs. Barcelona
Villarreal vs. Granada
:
✍️ 2019/20 Ratiba ya El Clásico
Jumapili 27 October 2019:
FC Barcelona vs. Real Madrid
:
Jumapili 01 March 2020:
Real Madrid vs. FC Barcelona
:
✍️ 2019/20 Ratiba ya Madrid Derby:
Jumapili 29September 2019:
Atletico Madrid vs. Real Madrid
:
Jumamosi 02 February 2020:
Real Madrid vs. Atletico Madrid
#Updates #fixtures #Laliga

Uhamisho ghali zaidi uliofanya na vilabu Barani Ulaya Msimu huu wa Dirisha la Usajili

✍️ Uhamisho ghali zaidi uliofanya na vilabu Barani Ulaya Msimu huu wa Dirisha la Usajili.
🇵🇹 Joao Felix (£113m)
🇧🇪 Eden Hazard (£88.5m)
🇫🇷 Lucas Hernandez (£68m)
🇳🇱 Frenkie de Jong (£65.3m)
🇪🇸 Rodri (£62.6m)
#TransferNewsUpdates

“Kuna Ofisi ilichangisha fedha kwa ajili ya Taifa Stars, hata hivyo fedha hiyo haikufika kwenye Timu, na badala yake waliitumia kwa matumizi yao ikiwemo Utalii

“Kuna Ofisi ilichangisha fedha kwa ajili ya Taifa Stars, hata hivyo fedha hiyo haikufika kwenye Timu, na badala yake waliitumia kwa matumizi yao ikiwemo Utalii, nawataka hiyo fedha waiwasilishe kwenye Baraza la Michezo la Taifa, BMT, vinginevyo hatutaelewana”. Mkuu wa mkoa wa DSM, Paul Makonda, na Mwenyekiti wa Hamasa Taifa Stars kwenye mashindano ya AFCON akizungumza mchana huu mara baada ya Taifa Stars kuwasili ‘airport’ ikitokea nchini Misri.

Design a site like this with WordPress.com
Get started