Fundi wa soka, Samir Nasri amejiunga na Klabu ya RSC Anderlecht ya Ligi Kuu Nchini Ubelgiji πŸ‡§πŸ‡ͺ

OFFICIAL | Fundi wa soka, Samir Nasri amejiunga na Klabu ya RSC Anderlecht ya Ligi Kuu Nchini Ubelgiji πŸ‡§πŸ‡ͺ kwa uhamisho huru baada ya kuondoka West Ham ya Uingereza.

Anarudiana tena na jamaa yake waliecheza wote Man City, ambaye Sasa Ni kocha Mchezaji wa RSCA, Vincent Kompany… Samir na Kompany walishinda mataji manne wakiwa wote @mancity
πŸ† 2 Premier League
πŸ† 1 League Cup
πŸ† 1 FA Community Shield
#TransferNewsUpdates

Wachezaji wapya wa Klabu ya Yanga SC, Mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda, Juma Balinya

– Wachezaji wapya wa Klabu ya Yanga SC, Mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda, Juma Balinya @officialbalinya Beki wa Kimataifa wa Burundi, Moustafa Selemani wametua Nchini Tanzania tayari kuanza majukumu ya kuitumikia Klabu yao Mpya Kwa msimu Mpya wa 2019/20..
.
– Wachezaji wa Kimataifa wa Yanga SC wanatarajia kuanza kuwasili Nchini hi Leo mpaka Jumapili ambapo wataanza Maandalizi ya wiki ya Wananchi Julai 21 ambapo mashabiki na wanachama wa Yanga watafanya kazi mbalimbali za kijamii kabla ya kilele Julai 27.
#TPLTransferUpdates

Mtandao wa Goal umeripoti kuwa golikipa wa Bandari Fc ya Kenya Farouk Shikalo amekanusha taarifa za kujiunga na Yanga Sc

Mtandao wa Goal umeripoti kuwa golikipa wa Bandari Fc ya Kenya Farouk Shikalo amekanusha taarifa za kujiunga na Yanga Sc huku klabu yake ikisisitiza kuwa bado ina mkataba wa mda mrefu na golikipa huyo. .
.
Shikalo amesema yalikuwepo mazungumzo kati yake na Yanga lakini hakusaini kama ilivyoripotiwa awali.

MISENYI, KAGERA: WALIOMTEKA MWANAFUNZI WA DARASA LA PILI WAHUKUMIWA MIAKA 5 JELA

MISENYI, KAGERA: WALIOMTEKA MWANAFUNZI WA DARASA LA PILI WAHUKUMIWA MIAKA 5 JELA

Mahakama imewahukumu kifungo hicho, Khalifa Ahmed(19) na Jonas Deogratias(19) kwa hatia ya kumteka Levis Respicius alikokuwa akitoka shuleni

Wawili hao walimteka Mtoto huyo kwa lengo la kumtumia kama njia ya kumshinikiza Baba yake, Respicius Aron awape kiasi cha Tsh. Milioni 15

Walitenda kosa hilo mnamo Mei 13, 2019 ambapo baada ya kumteka Mtoto Levis walimficha ndani ya chumba kwa siku 3 kabla ya kuokolewa na Jeshi la Polisi –
Mtoto huyo alikutwa akiwa amewekwa kitambaa mdomoni ili kumzuia asipige kelele na kufungwa miguu na mikono

SERIKALI: HATUJAZUIA MAKONTENA KWENDA BANDARI KAVU

SERIKALI: HATUJAZUIA MAKONTENA KWENDA BANDARI KAVU

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema Serikali haijazuia makontena kwenda bandari kavu bali taarifa zilizokuwa zikidai imezuia zililenga kuchafua biashara ya Bandari ya Dar es Salaam

Amesema kilichofanyika ni marekebisho ya sheria ambayo inatamka anayeamua kontena liende wapi ni mteja kwa kushirikiana na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari na si vinginevyo

Kamwelwe alisema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara wa madini kutoka nchi mbalimbali, ambao walitoa changamoto zinazowakabili

AMUUA MWENZAKE AKIMTUHUMU KUIBA PANGA MWAKA 2018 –

AMUUA MWENZAKE AKIMTUHUMU KUIBA PANGA MWAKA 2018

Jeshi la Polisi Wilaya ya Lindi linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Rondo Ntene, Aisha Mshamu (65) kwa tuhuma za kumuua Zainabu Mikumbi (80) akimtuhumu kwa wizi wa panga lililopotea 2018

Kamanda wa Polisi, ACP Prodansiana Protas amethibitisha kuwepo kwa taarifa ya mauaji hayo na kutaja chanzo kuwa ni ugomvi uliotokana na Zainabu kupoteza panga la Aisha mwezi Disemba 2018

Juni 29, Zainabu alienda mashambani na kukutana na Aisha ndipo ulipozuka ugomvi ambapo Aisha alifanikiwa kuchukuwa Jembe la Zainabu na kumpiga nalo kichwani na Shingoni

SUDAN: JESHI NA WANANCHI WAKUBALIANA KUUNDA SERIKALI YA MPITO

SUDAN: JESHI NA WANANCHI WAKUBALIANA KUUNDA SERIKALI YA MPITO

Viongozi wa Jeshi na Muungano wa upinzani wamekubaliana na kuundwa kwa Serikali ya mpito ambayo itatoa njia kwa kurejeshwa utawala wa kiraia

Umoja wa Afrika umesema pande hizo zimeahidi kuunda Serikali huru itakayoongozwa kitaalamu pamoja na kuchunguza machafuko ya hivi karibuni yaliyosababisha watu wengi kuuawa

Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yaliyoanza mapema wiki hii yalifanyika jijini Khartoum kupitia usuluhishi ulioongozwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia na wajumbe wa Umoja wa Afrika

Design a site like this with WordPress.com
Get started