LIGI KUU BARA KUANZA AGOSTI 23. SIMBA NA YANGA KUKUTANA JANUARI 04 –

LIGI KUU BARA KUANZA AGOSTI 23. SIMBA NA YANGA KUKUTANA JANUARI 04

Bodi ya Ligi nchini imetangaza ratiba ya Ligi kuu soka Tanzania Bara msimu wa 2019/20 ambapo Agosti 23 pazia litafunguliwa rasmi kwa mchezo mmoja kati ya Simba SC na JKT Tanzania

Mchezo wa Ngao ya Jamii unatarajiwa kuchezwa Agosti 17, 2019 kati ya Bingwa wa Ligi Kuu, Simba SC na Azam FC, Bingwa wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports Federetion CUP

Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi, Boniphace Wambura leo amesema “Msimu huu tumezingatia ratiba zote za kimataifa na hatutarajii mabadiliko ya ratiba kwa sababu zizisokuwa za msingi”

Katika ratiba hiyo Yanga SC itaanza kurusha karata yake ya kwanza dhidi ya Ruvu Shooting Agost 28, Azam FC na KMC zinatarajiwa kucheza Agosti 29

Aidha, Simba na Yanga zitakutana kwenye mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu, January 04, 2020 ambao Simba ndio atakuwa mwenyeji

SHAMIMU NA MUMEWE WARUDISHWA RUMANDE, MAHAKAMA BADO INASUBIRI RIPOTI YA MKEMIA MKUU

SHAMIMU NA MUMEWE WARUDISHWA RUMANDE, MAHAKAMA BADO INASUBIRI RIPOTI YA MKEMIA MKUU

Kesi inayomkabili, Abdul Nsembo maarufu Abdulkandida(45) na mkewe, Shamim Mwasha(41) bado inasubiri majibu ya kielelezo kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali

Wakili wa Jamhuri, Simon Wankyo leo Julai 8 mbele ya Hakimu Kelvin Mhina amesema katika kesi hiyo kinachosubiriwa ni majibu ya kielelezo kutoka kwa Mkemia na hivyo akaomba tarehe nyingine ya kesi kutajwa

Wakili wa utetezi, Hajra Mungula amedai Washtakiwa wako ndani na hawana dhamana na kuutaka upande wa mashtaka kufuatilia kielelezo hicho ili majibu yapatikane kwa wakati

Hakimu Mhina baada ya kusikiliza maelezo ya hayo ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 22, 2019 kwa ajili ya kutajwa na Washitakiwa wamerudishwa rumande

Shamimu na mumewe wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 36/2019 ambapo Wanadaiwa kusafirisha #DawaZaKulevya aina ya Heroin zenye uzito wa gram 232.70

SINGIDA: WATU 7 WAKIWEMO WAFANYAKAZI WATANO WA AZAM TV WAFARIKI AJALINI

SINGIDA: WATU 7 WAKIWEMO WAFANYAKAZI WATANO WA AZAM TV WAFARIKI AJALINI

Wafanyakazi wengine watatu wamejeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori

Ajali hiyo imetokea leo Julai 8, 2019 eneo la Shelui wakati wakieleleka Wilayani Chato Mkoa wa Geita katika uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Chato-Burigi

Taarifa zinaeleza kuwa Wafanyakazi hao walikuwa 10 katika gari aina ya Coaster na kwamba madereva wawili wa magari hayo nao wamefariki dunia

MCHEZAJI WA AJAX, MATTHIJS DE LIGT KUJIUNGA NA JUVENTUS

MCHEZAJI WA AJAX, MATTHIJS DE LIGT KUJIUNGA NA JUVENTUS

Meneja wa Mchezaji huyo kinda, Mino Raiola amethibitisha kuwa beki huyo raia wa Uholanzi amefikia makubaliano binafsi na klabu ya Juventus ya Italia

Inaaminika De Ligt amekubali malipo ya Paundi Milioni 10.8(Tsh. 31,083,256,839) kwa mwaka, ambayo ni sawa na Paundi 230,000(Tsh. 661,958,247) kwa wiki na sasa zinasubiriwa Ajax na Juventus kukubaliana ada

Inadaiwa Ajax inataka ada ya Paundi Milioni 67.3 lakini Juventus inataka kutoa Paundi Milioni 49.3 pamoja na Paundi Milioni 9 za nyongeza kwa mchezaji huyo aliyehusishwa na kujiunga Barcelona awali

Je, unadhani De Ligt atafanikiwa zaidi akiwa Juventus kuliko angeenda Barcelona?

DKT. BASHIRU: JIMBO LA HAI SI NGOME YA CHADEMA

DKT. BASHIRU: JIMBO LA HAI SI NGOME YA CHADEMA

Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amesema hayo wakati akieleza sababu ya ziara yake Mkoani Kilimanjaro na kusema kuwa ameanzia Wilaya ya Hai kimkakati

Amesema “Katika Mkoa wa kilimanjaro nimepanga kupita Wilaya kwa Wilaya kwa sababu ya uzito na umuhimu. Nimeanzia Hai kimkakati na mahesabu yametumika kuamua kuanzia Hai.”

Ametoa kauli hiyo jana Jumapili Julai 7, 2019 katika kikao cha CCM kilichofanyika katika uwanja wa Sabasaba katika jimbo la Hai ambalo Mbunge wake ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe

Aidha, Katibu wa CCM-Kilimanjaro, Jonathan Mabihya amesema mwaka 2015 chama hicho kilipoteza majimbo kadhaa mkoani Kilimanjaro kutokana na makundi baada ya kumalizika kwa kura za maoni.

Katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, CCM iliibuka na ushindi katika majimbo mawili kati ya tisa mkoani humo na Viti vya Udiwani 52 kati ya 169

WATU 29 WAFARIKI KATIKA AJALI YA BASI, KASKAZINI MWA INDIA

WATU 29 WAFARIKI KATIKA AJALI YA BASI, KASKAZINI MWA INDIA

Ajali hiyo imetokea leo asubuhi ambapo basi walilokuwa wakisafiria lilitoka nje ya barabara na kupinduka karibu na mji wa Agra, Kilometa 336 kutoka mji mkuu wa jimbo la Uttar Pradesh, Lucknow

Basi hilo lilikuwa limebeba watu 50 na lilikuwa likitoka Lucknow kuelekea Mji mkuu wa India, New Delhi. Watu 20 waliojeruhiwa wameokolewa na Wananchi waliowahi kufika eneo la tukio

Taarifa zinadai dereva wa basi hilo ambalo ni la ghorofa moja alikuwa amesinzia kabla ya basi hilo kutoka nje ya barabara hiyo ambayo ndiyo barabara ndefu nchini humo yenye laini 6(Kilometa 165)

Kwa mujibu wa Mamlaka nchini India, ajali za barabarani hutokea kila mara, ikikadiriwa moja hutokea kila baada ya dakika 4 na tangu mwaka 2012 watu zaidi ya 900 wamefariki katika ajali za barabarani

IRAN YATANGAZA KUVUNJA MKATABA WA NYUKLIA

IRAN YATANGAZA KUVUNJA MKATABA WA NYUKLIA

Imesema itaanza kuvunja mkataba kuhusu kiwango cha kurututubisha madini ya uranium na kupindua kile kilichoafikiwa katika makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015

Imesema itaendelea kupunguza uzingatiaji wa mkataba huo baada ya kila siku 60 iwapo mataifa yaliyosaini mkataba huo hayatachukua hatua za kuilinda dhidi ya vikwazo vya Rais Trump

Hali ya wasiwasi ikiwa inaongezeka, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekosoa uamuzi huo wa Iran na kusema kwamba unakiuka makubaliano hayo ya nyuklia

Aidha, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema hatua hiyo ni ya hatari sana na amezitaka nchi za Ulaya kuiadhibu Iran kwa kuiwekea vikwazo

Kocha Mkuu wa Timu ya taifa ya DR Congo 🇨🇩, Florent Ibenge ametaja sababu za kufanya vibaya AFCON 2019

✍🏻 Kocha Mkuu wa Timu ya taifa ya DR Congo 🇨🇩, Florent Ibenge amefunga sababu za kufanya vibaya AFCON 2019 Ambapo wameondoshwa katika hatua ya 16 Bora ya Michuano.
.
✍🏻 Ibenge amesema kuwa, Si kazi rahisi kuwa kocha wa klabu na Timu ya taifa… “Nimekuwa nikifanya hivyo kwa miaka minne na sikuwahi kumuachia mtu yeyote”, “Inaniathiri mimi, Kwa miaka minne tu ninakuwa na siku 9 tu za kupumzika”. “”Pia siwezi kuzunguka sehemu Mbalimbali kuwachunguza wachezaji wa kuchezea Timu ya taifa… Alisema kocha huyo.
.
✍🏻 Kocha Ibenge amesema kuwa hapati muda wa kuchagua Wachezaji wa kulitumikia taifa la DR Congo, kwani yeye ni kocha wa klabu hivyo Hana muda wa kuacha Klabu mpaka Ligi inaisha na Michuano inakaribia anakuwa na siku chache tu, hivyo anakosa muda wa kuangalia vipaji nje ya DR Congo.
.
✍🏻 Ikumbukwe, DR Congo ina makocha Watatu wanaounda jopo la Makocha ambao pia wote Ni Makocha Wakuu wa Vilabu tofauti tofauti.. .
1️⃣. Florent Ibenge, Kocha Mkuu wa DR Congo na Kocha Mkuu wa Klabu ya AS Vita Club ya DR Congo.
2️⃣. Mwinyi Zahera, Kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya DR Congo na Kocha Mkuu wa Klabu ya Young Africans SC ya Tanzania 🇹🇿.
3⃣. Mihayo Kazembe, Kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya DR Congo na Kocha Mkuu wa Klabu ya TP Mazembe…
#AFCONUpdates #TotalAFCON2019
@Sokawaytz_

Design a site like this with WordPress.com
Get started