
MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA KWA ASILIMIA 0.2 NDANI YA MWEZI
–
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi, Daniel Masolwa amesema mfumuko wa bei wa Taifa kwa Mwezi Juni, 2019 umeongezeka hadi asilimia 3.7 kutoka asilimia 3.5 kwa mwezi Mei, 2019
–
Amesema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Juni, 2019 imeongezeka ikilinganishwa na kasi ya iliyokuwepo kwa mwezi Mei, 2019
–
Amefafanua kuwa hali hiyo imechangiwa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Juni, 2019 zikilinganishwa na bei ya bidhaa za mwezi Mei, 2019
–
Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa mwezi Juni, 2019 ni pamoja na unga wa mahindi kwa 3.6%, Unga wa ngano kwa 4.4%, mtama kwa 4.9%, samaki wabichi kwa 27.3%, dagaa kwa 16.5%, mafuta ya kupikia kwa 9.5%, maharage 3.0%, mihogo kwa 16.6% na viazi mviringo kwa 18.8%
–
Aidha, baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa mwezi Juni, 2019 ni pamoja na dizeli kwa 11.4%, petroli kwa 4.9%, gharama za kulala kwenye nyumba za wageni kwa 5.8% na vitabu vya shule kwa 2.4%
–
Lakini pia, mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi mwezi Juni, 2019 umeongezeka hadi asilimia 2.3 kutoka asilimia 2.2 kwa mwezi Mei, 2019