

PSG: NEYMAR ANAWEZA KUONDOKA IWAPO OFA YA KUNUFAISHA PANDE ZOTE ITAPATIKANA
–
Mkurugenzi wa Michezo wa Klabu ya Paris St-Germain(PSG), Leonardo amesema hayo na kuongeza kuwa hawajapokea ofa yoyote kwa ajili ya Neymar ila kulikuwa na mawasiliano madogo sana na Barcelona
–
Mchezaji huyo raia wa Brazil mwenye miaka 27 ambaye amekuwa akihusishwa na kutaka kurudi Barcelona, alishindwa kuhudhuria mazoezi ya kujiandaa na msimu siku ya Jumatatu na PSG ilisema itachukua hatua stahiki
–
Alipoulizwa kama Neymar amewasilisha maombi ya kuondoka Klabuni hapo, Leonardo amesema “Iko wazi kwa kila mtu. Lakini kwenye mpira, unasema kitu kimoja leo na kingine kesho. Iko hivyo.”
–
Baba wa Neymar amesema kuwa Klabu hiyo ilikuwa inajua kuwa mwanaye atakosa mazoezi ya kwanza siku ya Jumatatu kutokana na masuala yake ya msaada katika Taasisi ya Neymar na kuwa atarudi PSG Julai 15
Je, unadhani Neymar atakuwa anachezea PSG au Barcelona msimu ujao?
















