

Leo kwenye tutashuhudia game kali ya 16 bora ya #NdondoCup2019, ni vita ya wageni kwenye @ndondo_cup kuwania kucheza robo fainali kwa mara ya kwanza…hatari tupu!! .
.
Toroli Kombaini kutoka pande za Keko uso kwa macho na Goba Ham United kutoka Goba, hizi timu zote ni ngeni kwenye michuano hii…zimeingia mwa mara ya kwanza na kutusua hadi 16 bora.
Zimetoka na moto kuanzia hatua ya awali kabisa ya mashindano haya, zikavuka hatua ya makundi lakini leo timu moja itaenda robo fainali nyingine itabaki.
Goba Ham kwenye hatua ya AWALI ilishinda mechi mbili na sare moja ikamaliza pointi sawa na Ukwamani lakini ikabaki nafasi ya pili kwa wastani wa magoli.
KUNDI D
Ukwamani pointi 7
Goba Ham pointi 7
Taswa FC pointi 1
Rangers pointi 1
Toroli Kombaini ilitwanga mechi zake zote za hatua ya awali na kukusanya pointi zote na hatimaye kufuzu ikiwa kinara wa kundi lake.
KUNDI H
Toroli Kombaini pointi 9
Mafundi Ujenzi pointi 4
Tandika Kombaini pointi 3
Mwandege City pointi 1
HATUA YA MAKUNDI
Katika hatua ya makundi, Toroli ilifuzu tena kwa kishindo kwa kuongoza kundi baada ya kushinda mechi zake mbili na sare moja na kukusanya pointi 7 mbele ya vigogo Misosi na Keko Fenicha.
KUNDI A
Toroli Kombanini pointi 7
Misosi FC pointi 7
Keko Fenicha pointi 1
Mamu Pharmacy pointi 1
Goba Ham ilisubiri hadi siku ya mwisho ya mechi za kundi lake kujua hatma yake, ikafanikiwa kusonga mbele kwa tofauti ya magoli dhidi ya Misosi FC mabingwa wa Ndondo Cup 2017
KUNDI D
UV Temeke pointi 5
Goba Ham pointi 4
Mpakani Kombaini pointi 4
Ukwamani pointi 2
Toroli Kombaini vs Goba Ham, nani anaenda robo fainali nani anabaki?