Mzee Hamis Kilomoni sio mdhamini tena wa klabu ya Simba.

Hizi ni barua zilizotoka kwa Kabidhi Wasii Mkuu wa Serikali kwenda kwa wakili wa aliyekuwa mdhamini wetu, na pia barua ya Mahakama kwenda kwa wakili huyo zinazothibitisha mdhamini huyo Mzee Hamis Kilomoni sio mdhamini tena wa klabu yetu ya Simba.

Taarifa hii ilitolewa leo na Afisa Mtendaji Mkuu, Crescentius Magori kwenye mkutano wake na wanahabari. #NguvuMoja

F

Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori ametolea ufafanuzi suala la Juuko Murshid

Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori ametolea ufafanuzi suala la Juuko Murshid ambaye inatajwa ameonesha utovu wa nidhamu ndani ya klabu ya Simba akiwa ndani ya mkataba na klabu hiyo unaomalizika mwezi Desemba mwaka huu.
:
“Wakati timu imeenda Kanda ya Ziwa, alisema anaumwa (kweli aliumia) akabaki Dar akiuguza majeraha, timu ilivyorudi Dar tayari alikuwa ametoroka ameenda Uganda hakuwepo kwenye kambi ya timu. Tukacheza mechi za mwisho akiwa hayupo, hakutoa taarifa kwa kocha, meneja wala uongozi.”
:
“Baada ya siku chache tukasikia yupo kambini na timu ya taifa ya Uganda anafanya mazoezi. Tukamwandikia barua ajieleze ni kwa nini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuondoka kwenye kituo chake cha kazi bila ruhusa ya mwajiri hata kuongoea na kocha wala meneja. Hiyo barua hakuijibu hadi leo.”
:
“Juzi tumemwandikia barua wakati Simba inaanza kambi tukamwambia aripoti kituo chake cha kazi kabla ya Julai 15 lakini bado hajaripoti.”
:
“Juuko anafikiri kwamba anaweza kulazimisha kihama, hawezi kulazimisha. Na kwa sababu alitoroka kazini, mshahara wa mwezi wa Mei na Juni hatukumlipa. Tunamlipaje mtu ambaye hayupo kazini?
:
“Kama kuna timu amepata aje hiyo timu ije izungumze na Simba .”

Klabu ya Arsenal imekubaliwa na klabu ya Gremio kulipa dau la Β£36m ili kumsajili mshambuliaji wake raia wa Brazil Everton Soares (The Sun)

Klabu ya Arsenal imekubaliwa na klabu ya Gremio kulipa dau la Β£36m ili kumsajili mshambuliaji wake raia wa Brazil Everton Soares (The Sun)

Baada ya mazoezi ya asubuhi wachezaji wa Mabingwa wa nchi wanapata chakula kizuri cha mchana na baada ya hapo wanapumzika kujiandaa na mazoezi ya jioni

Baada ya mazoezi ya asubuhi wachezaji wa Mabingwa wa nchi wanapata chakula kizuri cha mchana na baada ya hapo wanapumzika kujiandaa na mazoezi ya jioni. #NguvuMoja

Nyota 13 waliotemwa simba

Simba imetangaza kuwaacha wachezaji wake 13, akiwemo mfungaji bora wa Uganda katika fainali za Afcon, Emmanuel Okwi.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori alisema kati ya wachezaji hao, sita wametolewa kwa mkopo na saba wamemaliza mikataba.

“Waliomaliza mikataba klabu haikuhitaji kuendelea nao, isipokuwa Asante Kwasi ambaye mkataba wake unamalizika Novemba.

“Kwasi amepata timu na klabu tumeamua kuachana naye baada ya makubaliano ya pande zote mbili ili akaendelee na maisha mengine,” alisema Magori.

Aliwataja wachezaji wengine walioachwa rasmi kuwa Haruna Niyonzima, Emmanuel Okwi, Nicholaus Gyan, Zana Coulibaly, James Kotei na Salim Mbonde.

Wachezaji waliowatoa kwa mkopo ni Mohamed Ibrahim (Mo), Marcel Kaheza, Mohamed Rashid, Adam Salamba, Paul Bukaba na Abdul Athumani wa timu ya vijana ya

IJUMAA HII YA Date 19/7/2019 KUTAKUWA NA MECHI KALI KATI YA WASANII WA @bongoflavafc Vs @mwananchi_

IJUMAA HII YA Date 19/7/2019 KUTAKUWA NA MECHI KALI KATI YA WASANII WA
@bongoflavafc Vs @mwananchi_official Siku ya Ijumaa ktk Uwanja wa LEADERS CLUB Kuanzia saa 10 Jioni..HAKUNA KIINGILIO Sio Kushika MIC tu,Hata Gemu Tunaliweza
@bongoflavafc Tunakaribisha mechi za kirafiki au mashindano sehemu tofauti tofauti
Kwa maelezo zaidi tucheck dm au piga namba +255713424943 …MICHEZO NI FURAHA

Mwamuzi Victor Gomes ala shavu kuchezesha mchezo wa fainali ya AFCON 2019

Mwamuzi Victor Gomes ala shavu kuchezesha mchezo wa fainali ya AFCON 2019

Jumanne mchana ilitoka story kwamba mwamuzi Bamlak Tessema Weyesa kutoka Ethiopia ndio atachezesha mchezo wa fainali ya AFCON 2019 (Senegal vs Algeria). Usiku wa siku hiyohiyo ikatoka taarifa nyingine kutoka CAF kwamba mwamuzi atakayechezesha fainali ni Victor Gomes kutoka Afrika Kusini.

Moja kati ya vitu ambavyo vinampa upinzani mkubwa Rais wa CAF Ahmad Ahmad ni vitendo vyake vya kutaka kutolea mamaamuzi kila kitu.

Mfano ishu inayozungumzwa sana ni waamuzi kubadilishwa mara kwa mara kwenye mashindano ya AFCON mwaka huu.

Kwenye mchezo wa Madagascar dhidi ya DR Congo mwamuzi alibadilishwa masaa matano kabla ya mchezo husika. Kitendo hiki kililalamikiwa sana na wacongoman, tulimsikia Zahera Mwinyi akilalamika lakini wabongo tukachukulia poa lakini alikuwa anahoja ya msingi sana kuhusiana na mambo yanavyofanyika ndivyo sivyo.

Kwa hiyo moja kati ya story kubwa hapa Cairo ni kamati ya waamuzi kuingiliwa na kutokuwa huru kupanga waamuzi kama kawaida, inasemekana Boss wa juu wa shirikisho anaingilia maamuzi na wakati mwingine anapendekeza waamuzi ambao anadhani wanastahili kuchezesha baadhi ya mechi.

Kwa hiyo mimi sishangai kuona jina la mwamuzi aliyetangazwa awali kubadilishwa na kupewa mtu

MATOKEO YA SOKA JANA JUMANNE NA RATIBA YA HII LEO

M

MATOKEO YA SOKA JANA JUMANNE NA RATIBA YA HII LEO.
:
– Champions League – Qualification
FT KF Shkendija 1 – 2 Nomme JK Kalju
FT Saburtalo 1 – 3 FC Sheriff
FT HB Torshavn 2 – 2 HJK
FT Valletta 1 – 1 F91 Dudelange
FT FK Crvena Zvezda 2 – 1 Suduva
FT Feronikeli 0 – 1 TNS
.
– Europa League – Qualification.
FT FC Banants 0 – 5 Cukaricki
FT Klaksvik 0 – 0 FK Riteriai
FT OFK Titograd 0 – 0 PFC CSKA-Sofia
.
– International – Club Friendlies.
FT Malagueno 0 – 0 Reading
FT Genclerbirligi 1 – 1 Antalyaspor
FT TOP Oss 0 – 1 Waalwijk
FT FC Wacker 0 – 7 Genoa
FT Metz 2 – 1 Sporting Charleroi
FT Paris FC 0 – 1 Dijon
FT SC Herz Pinkafeld 0 – 9 Rapid Wien
FT Eintracht Northeim 1 – 4 SC Paderborn 07
FT Aves 2 – 0 RD Agueda
FT FC Groningen 2 – 2 FC Emmen
FT Heracles 0 – 2 Excelsior
FT Raeren 1 – 7 Eupen
FT Straelen 1 – 2 VVV-Venlo
FT Zulte Waregem 1 – 1 Oostende
FT CF Peralada 0 – 6 Espanyol
FT Extremadura 0 – 1 Reading
FT Bournemouth 3 – 2 Wimbledon
FT Chorley 0 – 2 Preston
FT Millwall 1 – 2 SC Braga
FT Dynamo Dresden 1 – 6 PSG
FT Boreham Wood 2 – 1 QPR
FT Scunthorpe United 0 – 1 Leicester City
FT Northampton Town 0 – 4 Sheffield Wednesday
FT Olympiacos 3 – 0 Nottingham Forest
FT Barnet 6 – 2 Crystal Palace
FT Burton Albion 2 – 1 Sheffield United
FT Yeovil Town 1 – 6 Swansea City
FT FC Porto 1 – 0 Fulham
.
– Africa – Kagame Cup:: Quarter finals.
FT TP Mazembe 1 – 2 Azam FC
FT KCCA FC 2 – 1 Rayon Sport
:
RATIBA YA HII LEO JUMATANO.
– Africa Cup of Nations – 3rd/4th place.
22:00 Tunisia
Nigeria
.
– Champions League – Qualification.
19:30 Rida FC
Dundalk FC
20:00 AIK
Ararat Armenia
20:00 Qarabag FK
Partizani
20:00 Rosenborg
Linfield
20:30 Ludogorets Razgrad
Ferencvaros
21:00 Piast Gliwice
BATE Borisov
21:45 Celtic
FK Sarajevo
.
– England – Premier League Asia Trophy.
13:00 Newcastle
Wolves
15:30 Manchester City
West Ham
.
– Africa – Kagame Cup:: Quarter finals.
17:00 Gor Mahia
Green Eagles
19:30 APR FC
Maniema Union
#Updates #fixtures
@Sokawaytz_

limetangaza vyungu vitano ambavyo vitapangwa Katika Makundi ya kuwania Kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika AFCON Mwaka 2021

– Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limetangaza vyungu vitano ambavyo vitapangwa Katika Makundi ya kuwania Kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika AFCON Mwaka 2021 Nchini Cameroon πŸ‡¨πŸ‡²… Shirikisho hilo litafanya mkutano mkuu Julai 18 katika Ukumbi wa Aida Ballroom, wa Hoteli ya Marriott, Cairo, Misri na moja ya ajenda ni kupanga ratiba ya kusaka kufuzu kwa AFCON ya Cameroon 2021.
:
– Tanzania imepangwa katika chungu cha tatu pamoja na Madagascar, Zimbabwe, Central Africa Republic (CAR), Namibia, Sierra Leone, Msumbiji, Guinea Bissau, Angola, Malawi, Togo, na Sudan… Nchi hizo hazitapangwa kukutana Katika Kundi moja.
:
– Pia, Nchi hizo zimepangwa katika vyungu vitano kwa kuangalia orodha ya viwango vya ubora wa FIFA iliyotoka Juni 14, 2019. Cameroon itakuwa wenyeji fainali hizo za 2021, ikiwa ni mara ya kwanza tangu ilipofanya hivyo 1972 (miaka 49 iliyopita)… Kutakuwa na Makundi 13 yenye Jumla ya timu Nne..
#TotalAFCON2021 #AFCON2021
@Sokawaytz_

FULL-TIME : KCCA 2-1 Rayon Sport FC [Kizza Mustafa,33’, Jackson Nunda,66’|Herve Rugwiro,48] :

FULL-TIME : KCCA 2-1 Rayon Sport FC
[Kizza Mustafa,33’, Jackson Nunda,66’|Herve Rugwiro,48]
:
– Kwa Ushindi huo, Mabingwa wa Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬, KCCA wanafuzu Kucheza Nusu fainali ya Michuano hii ya Kombe la CECAFA Kagame, watamjua mpinzani wao kesho ambapo Ni Mshindi Kati ya GOR Mahia ya Kenya πŸ‡°πŸ‡ͺ au Green Eagles FC ya Zambia πŸ‡ΏπŸ‡²..
#CECAFAKagameCup #KagameCup2019

Design a site like this with WordPress.com
Get started