Beki Zana Coulibaly haamini kilichomtokea simba

Beki Zana Coulibaly ameachwa kwenye kikosi cha Simba baada ya kuitumikia timu hiyo kwa miezi sita tu

Beki huyo aliyetua Simba wakati wa usajili wa dirisha dogo alikuja nchini kwa lengo la kuanza maandalizi ya msimu mpya hata hivyo akakutana na barua ya kutupiwa virago

Licha ya usajili wake kupambwa na mbwembwe nyingi, Zana alishindwa kufikia matarajio ya wengi

Kama sio kutetewa na kocha Patrick Aussems, pengine mchezaji huyo angeondolewa mapema zaidi kwenye kikosi cha Simba

Kuachwa kwake kunamaanisha kuwa Simba inahitaji kusajili beki mwingine wa kulia ambaye atasaidiana na Shomari Kapombe aliyerejea kikosini baada ya kupona majeraha

Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori amesema watasajili mchezaji mmoja ambaye itakuwa sapraizi kwa mashabiki wa Simba

Je mchezaji huyo atakuwa mbadala wa Zana au Walter Bwalya anayetajwa kuja kuchukua nafasi ya Emmanuel Okwi? Tusubiri

Everton na RB Leipzig zimefikia makubaliano ya kuuziana winga wa Kimataifa wa Uingereza, Ademola Lookman;

– Everton na RB Leipzig zimefikia makubaliano ya kuuziana winga wa Kimataifa wa Uingereza, Ademola Lookman; Dili hilo linatajwa Kufikia £22.5m ndani ya Masaa 24, Nyota huyo atakuwa Mali ya Klabu hiyo ya Ujerumani.
.
– Lookman 21; alicheza kwa mkopo tangu mwishoni mwa msimu wa 2017/18 ndani ya Klabu hiyo ya Ujerumani, msimu uliopita alikuwa Everton na Kucheza game tatu tu za Ligi chini ya Kocha Mkuu, Marco Silva… Mchezaji huyo alitua viunga vya Goodison Park akitokea Charlton Mwaka 2017 na Kusaini Mkataba Mpaka Mwaka 2021… Winga huyu pia Ni Bingwa wa Kombe Dunia 2017 akiwa na timu yake ya taifa ya England U20..
#TransferNewsUpdates #EPLUpdates

KANYAGA TWENDE CHAN NA IDD NADO

🔥🔥🔥KANYAGA TWENDE CHAN NA IDD NADO

Ndayirigije baada ya kuwasili Azam FC kama kocha mkuu akitokea KMC , pendekezo lake la kwanza kabisa la usajili lilikuwa kiungo Mshambuliaji matata, Idd Seleman Ally ‘Iddy Nado ‘ Mtoto Iddy wa kuzua balaa,’ kutoka Mbeya City..
.
Maboss wa Azam FC hawakusita kumnyakua winga huyo aliyekuwa nguzo muhimu ya Mbeya City kwa msimu uliopita akifunga goli 10.
Ndayirigije kudhihirisha hakukosea kumwita kijana huyu mwenye nguvu , kasi na kipaji halisi cha soka, kamwita tena Taifa Stars #kanyaga_twende Nado.
Kama Taifa tumeamua jambo moja kwa pamoja, #TunakanyagaMpakaCHAN |🇹🇿
@kawambwa_jr
@pascal_kabombe
@jamestupatupa
@alikamwe
@giftmacha
@karim_boimanda
@charlesabel24
@2official6
@zechicharito1
@yossima_sports
@bill_shankly_1892
@anwarbinde
@fatmalikwata
@baraka_mpenja
@kichunafatma
@Abdulmkeyenge
@boiplusmedia
@bintisuleimani
@zechicharito1
@samuel_.samuel
@paulurio_barcelona

Ole Gunnar Soslkjaer amethibitisha kuwa Pogba haendi popote

Ole Gunnar Soslkjaer amethibitisha kuwa Pogba haendi popote. Ole amewaambia waandishi wa habari kuwa unapokuwa na mchezaji kama Pogba kwenye timu yako, lazima uijenge timu kumzunguka yeye.
:
✍️ Amedokeza kuwa ni lazima Pogba alindwe kutokana na kipaji alicho nacho, na njia pekee ya kumlinda Pogba ni kuhakikisha wote kwa pamoja wanapambana kupata mataji.
:
✍️ “Kucheza United pekee sio kitu kama hunyakui mataji. Hii inaleta hofu ndio maana hata wachezaji wenyewe wanaweza kutamani kuondoka”-Ole Gunnar
:
Alipoulizwa pia kuhusu usajili, amekiri klabu yake kuhitaji wachezaji wawili au hata watatu. Lakini ametoa tahadhari kuwa, kuja kwa wachezaji wapya itabidi kuambatane na baadhi ya wachezaji kuondoka.
:
Wachezaji ambao inasadikika wapo mbioni au karibu sana kutua United.
:
❓ Bruno Fernandes
❓Harry Maguire
:
Wanaosemekana kusepa
✍️ Romelu Lukaku
✍️ Erick Bailey

Kocha mkuu wa Tottenham, Mauricio Pochettino, lel amekamilisha usajili wa Maurizio Pochettino. Ambaye ni mwanae wa kumzaa.

📝 DEAL DONE: Kocha mkuu wa Tottenham, Mauricio Pochettino, lel amekamilisha usajili wa Maurizio Pochettino. Ambaye ni mwanae wa kumzaa. Maurizio atajiunga na kikosi cha vijana cha Spurs.

Design a site like this with WordPress.com
Get started